Ushauri: Nimebaki na Tsh. 10,000/- tu baada ya kupokea mshahara, nifanyaje?

Chief Kumbyambya

JF-Expert Member
Jun 16, 2022
490
1,461
Wasalaam ndugu zangu, aisee ama kweli pombe sio chai.

Juzi Ijumaa katika mazingira yetu ya kazi wakatuzingatia ile posho ambayo tunayoipataga kila ufikapo mwisho wa mwezi, sasa hizi posho zinazaombatana na weekend sio nzuri kabisa ndugu zangu.

Sasa si nikaenda kulewa! Nimeamka Jumaatatu leo asubuhi mfukoni nina 10,000/= tu na sina salio lingine zaidi ya hii teni! Naombeni ushauri wazee, nasavaivu vipi na hii teni mpaka tarehe za mwishoni mwa mwezi ujao? Maana nimewaza mpaka naanza kunyonyoka nywele na kuilaumu mitungi.

Pia ni kwa namna gani nitaacha mitungi. Hapo naombea gesi isiishe geto maana nilivyoamka asubuhi nikajaribu kutingisha mtungi wa gesi ni mwepesi balaa, ila bado haijaisha lakini itakata tu ndani ya wiki hii.

Naanza kuukumbuka ule wimbo wa msondo ngoma, "Kuzaliwa mwanaume kila kitu kwako kitakuwa ni taabu tu!"

Wazee nitafika Septemba tarehe kama hizi kwa balance ya 10,000/= mfukoni? Nikisema nitoe buku nikabeti mpira au tatu mzuka si ndio watapita nayo yote? Au niuze simu?

Mitungi sio, aliyegundua na kuitengeneza mitungi atakuwa hana akili fresh, maana inamaliza hela vibaya, akili inarudi wakati ushapukutika mifuko myeupe.

Pia na hizi kampani za hovyo hovyo za mitungi niachane nazo, maana naweza kufa kwa mawazo. Yaani mimi nabaki na teni wakati leo ndiyo kwanza tarehe 28 August? Sasa tarehe 28 September nitafika kweli? Naombeni ushauri niishi nayo vipi hiyo teni.

Maana wanasema ukikwama shirikisha na wengine, ila mitungi sio wazee.
 
Nipo mbeya boss
Sasa rasmi wewe ni rafiki yangu , nilikuwa natafuta rafiki mlevi kama mimi ili sasa tuukatae ulevi tuweke misingi .

Njoo sasa Mbeya Carnival tunywe kidogo nitalipa mimi ila tukimaliza tuanze mada ya kuacha pombe tuzipambanie ndoto zetu .

Note , nitakukopa kidogo ili ufike siku ya posho ila usipolipa sitaona shida kuja kukuchamba huku jukwaani , njoo rafiki yangu

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Sasa rasmi wewe ni rafiki yangu , nilikuwa natafuta rafiki mlevi kama mimi ili sasa tuukatae ulevi tuweke misingi .

Njoo sasa Mbeya Carnival tunywe kidogo nitalipa mimi ila tukimaliza tuanze mada ya kuacha pombe tuzipambanie ndoto zetu .

Note , nitakukopa kidogo ili ufike siku ya posho ila usipolipa sitaona shida kuja kukuchamba huku jukwaani , njoo rafiki yangu

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Hapo itakuwa safi ila nikisema nizimue ndiyo zitaniongezea mawazo maana akili itakuwa ikikumbuka tu kuwa mfukoni nina teni itanipa msongo. Walau ningebaki hata na fifte ingekiwa safi,ila teni aiseeeee duuh! Upo Mbeya maeneo gani mzee
 
Cha ushamba na ulimbukeni wakupata pesa na kukimbilia bar, weka ulevi kama burudani kwako siyo kipaumbele yani utakunywa pombe pindi ambapo umeshafanyqa mambo yako yote ya msingi mfano uhakika wa chakula wew bunafsi mwezi mzima uhakika wa afya yako endapo utaugua uhakika wa kutatua changamoto ndogo ndogo mfano ukipata tatizo ambalo linaitaji pesa furani je unayo akiba kama huna je kuna sehemu au mtu unaweza ukapiga sm mmoja tu ukaipata hiyo pesa

Ukiona hayo mambo yapo sawa kesha bar, siyo unaenda bar na laki asubuhi unamka na buku ujui utaishije huo ni upuuzi na ujinga zaidi ya utoto
 
Cha ushamba na ulimbukeni wakupata pesa na kukimbilia bar, weka ulevi kama burudani kwako siyo kipaumbele yani utakunywa pombe pindi ambapo umeshafanyqa mambo yako yote ya msingi mfano uhakika wa chakula wew bunafsi mwezi mzima uhakika wa afya yako endapo utaugua uhakika wa kutatua changamoto ndogo ndogo mfano ukipata tatizo ambalo linaitaji pesa furani je unayo akiba kama huna je kuna sehemu au mtu unaweza ukapiga sm mmoja tu ukaipata hiyo pesa

Ukiona hayo mambo yapo sawa kesha bar, siyo unaenda bar na laki asubuhi unamka na buku ujui utaishije huo ni upuuzi na ujinga zaidi ya utoto
Nimekupata vyema sana, ila hakuna anaependa hii hali ni basi tu sijui kwa nini inatokea..
 
Back
Top Bottom