Ushauri: Ndugu yangu hakubaliani na hali ya mtoto wake ilhali mtoto wake ashaikubali, pesa zinapotea na ni mwepesi kudanganyika, kipi kifanyike ?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
huyu ni mama mdogo wangu na nipo karibu sana na mtoto wake ambae huwa ananiambia vitu vingi.

Ni kwamba mtoto wa mama mdogo alipokuwa mdogo akiwa na umri wa miaka 9 aliumwa malaria, hali yake ilikuwa mbaya sana ikabidi apigwe sindano za quinine (kwinini)

Hii dawa kama mtakumbuka hapo zamani kwa waliowahi kutumia hii dawa ilikuwa inaziba masikio kwa kiasi flani lakini kesho yake yanarudi, ila kwa wengine hasa wale wanaochoma sindano edapo kipimo kikizidi hii kwinini ishafanya wawe viziwi kabisa ama kuwa na usikivu hafifu unaozidi kufifia kadri miaka inavyoenda.

ndicho kilichomkuta mtoto wa mama mdogo, akiwa na miaka 9 ndio alipigwa hizo sindano, alipofika darasa la saba tukaanza kuona hasikii fresh, na hapo ndipo napowaletea mkasa wangu.

ni tangu kipindi hicho hadi sasa kwa miaka takribani 10 mama mdogo anaamini kijana wake kaaminishwa kwamba kijana wake karogwa na kapitia mengi sana akiwa kama mama na hili nami naujua uchungu wa mama lakini imefika steji kwamba na mimi nmeamini wanawake ni rahisi sana kudanganyika.

Hopitalini huko alishaambiwa chanzo walimpa dawa lakini hazikumsaidia - Muhimbili, Kcmc, nairobi, india, Uingereza

yeye mtoto kashakubali hali yake, wana vikundi vyao vya wenye tatizo hilo na ana shughuli zake lakini shughuli ipo kwa mama yake.

Wachungaji feki

Mama mdogo akisikia tu kuna mchungaji mkubwa kaja mkoa anaoishi anaenda kwa wachungaji kuwapa hela hizi laki 2 hadi laki 5 kwajili ya kumuombea mtoto wake,, nilikuwa siamini haya mambo lakini hapo mwaka jana tu kuna mchungaji maarufu kabisa alikuja huo mkoa, kuna maombi maalum ya mtu moja moja ndani ya hema ni shilingi laki 4 kwa mtu moja.

Wachungaji baadhi yao wanafanya mazingaombwe ya wazi wazi nae mama mdogo anaamini kirahisi, kuna mmoja alienda nyumbani kwao huwa inasemekana anatembea na kemikali flani anachovyakwenye vidole, akianza kukuosha sehemu yoyote ya mwili maji yanabadilika rangi yanakuwa ya zambarau, yani hapa mama mdogo akili zilimruka akiamini ni uchawi unatoka, mme wake alipoona hivyo akardi chumbani kumwambia hayo mazingaombwe lakini wapi.

Mashehe wanaopandisha majini

Hapa ilibidi wasafiri kabisa kwenda huko Tanga, huyo shehe ni mshirikina anapandisha majini anaanza kumshirikisha Mungu kwenye tabibu zake, niliambiwa kila ikifika jioni kuna kufushwa dawa, hii ilikuwa kwa wiki nzima,

Waganga wa kienyeji:

Hapa palishafanyika hadi tambiko kkupigia magoti mizimu ilhali ni watu hao hao wanaenda nyumba za ibada

...............................................................

MUHIMU: Kijana kaniomba wazo la biashara, nipeni mawazo yenu >> hapa <<
 
Ni ngumu sana kwa wamama kugive up kwa watoto wao na hii inadhihirisha jinsi gani wana upendo wa kweli. Sijui kama itakuwa rahisi kumtoa huko alipo.

Kuna bi mkubwa mmoja mwanae ni jizi muuaji ila akiwekwa ndani mama yake anampambania mpaka anatoka licha ya kuwa tabia zake sio na hazikubaliki kijamii na kisheria. Ndugu zake wa kuzaliwa wote wamemtenga ila mama yake ndie anamuhangaikia anaamini ipo siku atabadilika.
 
kwa wengine hasa wale wanaochoma sindano edapo kipimo kikizidi hii kwinini ishafanya wawe viziwi kabisa ama kuwa na usikivu hafifu unaozidi kufifia kadri miaka inavyoenda.
Hakuanzia hospitalini? Kama vipi mchukue huyo dogo ww mwenyewe muende CCBRT akafanyiwe vipimo vizuri.
Kama inawezekana anaweza kupata hearing aid.
Pale buguruni chama(kwenye ile shule ya viziwi) walikuwa wanazitoa bure.
 
Kwahio sasahivi hasikii kabisa au ni kwa tabu?
Bora upambane ujue mambo yamekwama kuliko kuacha na kujilaumu,
......pengine ningefanya hiki, ....ningeenda kulee....

Sema yeye naye anachanganya imani, angeamua moja.
 
Mama hawezi kukata tamaa kwa mtoto wake.

Kuna akina mama watoto wao ni wezi lakini mpaka anaingia kaburini anamtetea mtoto wake, ndio iwe ugonjwa?

Akina baba ndio wazee wa kukubali matokeo, wazee wa 'big picture'. Kama baba mdogo yupo amsaidie kumpunguza kasi mama.
 
Ni wamama wanao give up kwa watoto wao na hii inadhihirisha jinsi gani wana upendo wa kweli. Sijui kama itakuwa rahisi kumtoa huko alipo.
Shida Ni kwamba Ana pesa za kuwapa hao wachungaji, Kama Ni ninyi mnampa Basi msitishe kumpa pesa hizo, Kama Ni yake hamna kitu mtamwambia atawasikiliza.
Ndivyo ilivyo. Walimwengu hawana huruma. Shida yako ndio mtaji kwao.
Usiombe yakukute.
Hakuanzia hospitalini? Kama vipi mchukue huyo dogo ww mwenyewe muende CCBRT akafanyiwe vipimo vizuri.
Kwahio sasahivi hasikii kabisa au ni kwa tabu?
Bora upambane ujue mambo yamekwama kuliko kuacha na kujilaumu,
Sijawahi kuona au kusikia kuwa limetibika kwa njia hiyo.
Kama ana pesa wacha atumie anavyotaka akiamua kutoa sadaka wacha atoe. Akiamua kula bata kazzi ni kwake
Duh! Mama mdogo na yeye ameshapata tatizo la kisaikolojia.
Akina baba ndio wazee wa kukubali matokeo, wazee wa 'big picture'. Kama baba mdogo yupo amsaidie kumpunguza kasi mama.
pitieni hapa pia

 
Ni wamama wanao give up kwa watoto wao na hii inadhihirisha jinsi gani wana upendo wa kweli. Sijui kama itakuwa rahisi kumtoa huko alipo.
Kuna bi mkubwa mmoja mwanae ni jizi muuaji ila akiwekwa ndani mama yake anampambania mpaka anatoka licha ya kuwa tabia zake sio na hazikubaliki kijamii na kisheria. Ndugu zake wa kuzaliwa wote wamemtenga ila mama yake ndie anamuhangaikia anaamini ipo siku atabadilika.
Umenigusa mkuu

Kuna kipindi nakumbuka niliugua sana muda huo mama alikua anamalizia nyumba nyingine na mzee yupo kwenye nyumba nyingine, nikaumwa sana nikiwa na mzee nikatembea hospital nyingi nikiwa mwenyewe sikua na mtu wa kunipa kampani

Ukafika muda mzee akaniambia mama yako anakuita ameshamaliza kujenga nenda ukaishi nae amesema utapona, nilienda kwa mama mara ya kwanza ananiona alimwaga uchozi akalia sana mwanangu imekuaje shida nini hospital wamesemaje? Analia maana miguu ilikua imevimba ukibonyeza inabonyea km ngano inayokandwa, akasema utapona akaanza kunihangaikia huku na huku nakumbuka alitumia pesa nyingi ili TU nipone kuna mtu alikuja kunikagua akijifanya ni mtu wa tiba mbadala nakumbuka mama ilimtoka zaidi ya 800k ili TU Mimi nipate dawa nipone,

Misosi misosi kila asubuhi mchana jioni kula sana kuku na bata wa mama ili nipone, supu ya kuku asubuhi alikua anaenda shamba anavuna Nazi na madafu, maembe, machungwa, machenza, mananasi ananifungia ananiletea, anachumia na kunitengenezea dawa za kuongeza Kinga ya mwili km mlonge, komamanga zipo shambani ananitengenea ananipa ninywe juice yake, kisha anaangalia maendeleo yangu

Mama ni Mama na uchungu wa mtoto anaujua Mama yake, sio Baba ingawa wanasema Mwana Mpumbavu ni Mzigo kwa Mamaye Ila Mwana mwenye Hekima humfurahisha Babaye

Nisiseme mengi ila

Mama atabaki kua Mama
 
Umenigusa mkuu

Kuna kipindi nakumbuka niliugua sana muda huo mama alikua anamalizia nyumba nyingine na mzee yupo kwenye nyumba nyingine, nikaumwa sana nikiwa na mzee nikatembea hospital nyingi nikiwa mwenyewe sikua na mtu wa kunipa kampani

Ukafika muda mzee akaniambia mama yako anakuita ameshamaliza kujenga nenda ukaishi nae amesema utapona, nilienda kwa mama mara ya kwanza ananiona alimwaga uchozi akalia sana mwanangu imekuaje shida nini hospital wamesemaje? Analia maana miguu ilikua imevimba ukibonyeza inabonyea km ngano inayokandwa, akasema utapona akaanza kunihangaikia huku na huku nakumbuka alitumia pesa nyingi ili TU nipone kuna mtu alikuja kunikagua akijifanya ni mtu wa tiba mbadala nakumbuka mama ilimtoka zaidi ya 800k ili TU Mimi nipate dawa nipone,

Misosi misosi kila asubuhi mchana jioni kula sana kuku na bata wa mama ili nipone, supu ya kuku asubuhi alikua anaenda shamba anavuna Nazi na madafu, maembe, machungwa, machenza, mananasi ananifungia ananiletea, anachumia na kunitengenezea dawa za kuongeza Kinga ya mwili km mlonge, komamanga zipo shambani ananitengenea ananipa ninywe juice yake, kisha anaangalia maendeleo yangu

Mama ni Mama na uchungu wa mtoto anaujua Mama yake, sio Baba ingawa wanasema Mwana Mpumbavu ni Mzigo kwa Mamaye Ila Mwana mwenye Hekima humfurahisha Babaye

Nisiseme mengi ila

Mama atabaki kua Mama
Mkuu pole sana ila hawa mama zetu wanatufanyia mengi sana mema ambayo hatuwezi kuyalipa. Tuzidi kuwaonesha upendo na kuwajali tuna mengi sana ya kushukuru Mungu kwa ajili ya hawa mama zetu kwa wanavyojali na kutuhangaikia hasa kwenye vipindi vigumu kimaisha. Ni kina mama wachache sana huwa hawajali watoto wao.
 
Mkuu pole sana ila hawa mama zetu wanatufanyia mengi sana mema ambayo hatuwezi kuyalipa. Tuzidi kuwaonesha upendo na kuwajali tuna mengi sana ya kushukuru Mungu kwa ajili ya hawa mama zetu kwa wanavyojali na kutuhangaikia hasa kwenye vipindi vigumu kimaisha. Ni kina mama wachache sana huwa hawajali watoto wao.
Mzee alinisihi kitu kimoja kwamba unapofanya kazi ukipata chochote mtumie mama yako Mimi unaweza usinipe chochote Ila mama yako mpe, huna Cha kumlipa kwa aliyokufanyia amekufanyia mengi mema Ila kwa kidogo utachompatia atafarijika kusema angalau na Mimi mwanangu amenikumbuka na baraka zake huanzia hapo
 
Mzee alinisihi kitu kimoja kwamba unapofanya kazi ukipata chochote mtumie mama yako Mimi unaweza usinipe chochote Ila mama yako mpe, huna Cha kumlipa kwa aliyokufanyia amekufanyia mengi mema Ila kwa kidogo utachompatia atafarijika kusema angalau na Mimi mwanangu amenikumbuka na baraka zake huanzia hapo
Mzee alikushauri vyema kabisa
 
Back
Top Bottom