USHAURI: Mnaotaka kufunga ndoa kwa sherehe kubwa zingatieni haya kuepuka lawama za watu

Kibosho1

JF-Expert Member
Dec 12, 2017
2,491
3,998
Wachumba, Marafiki nawapa salaam kwenu.
Kwa wakristo nashauri tusome Luk 14:28 ili twende sawa. Kwa dini nyingine na wasiokuwa na dini twendeni na msamiati huu.
"Ukitaka cha uvunguni sharti uiname"
Nimehudhiria baadhi ya harusi nyingi sana hasa mwaka huu lakini mambo siyo ya kuridhisha kabisa.
Mambo yanaenda enda tu bila mipango kutokana na mambo sio powa kwa raia kwenye swala la kiuchumi changanya na covid-19 tena.

KASORO KASORO ZA KUKUMBUKWA

1. Unaenda kwenye harusi, ukumbi mzuri,mapambo mazuri lakini chakula kimeisha😬😬
2. Wanandoa wamependeza chakula cha kutosha,Bia zimeisha (kila mtu 1 tu)😔😔
3. Vinywaji vya kutosha,vyakula vyote mc& music vya kuunga unga🙄🙄
4. Maandalizi yote yako sawa lakini pesa ya Video shooting na picha haitoshi "atakopwa🙈"🤔🤔

Kukosekana kwa kimojawapo kati ya hivyo ni rahisi sana kuharibu shughuli yote na kukumbukwa na wahudhuriaji.

MASWALI YA KUJIULIZA KABLA YA MIPANGO
Bajeti yangu inatosha kufanya sherehe hii?
Jiangalie wewe kama wewe je nina shilingi ngapi?
Kama kuna michango je itanitosha?
Kama isipotosha nawezaje kufanikisha hii?

Kuboronga kwa shughuli nyingi kunatokana na mipango mibovu na tamaa ya waandaaji bila kuzingatia kiasi halisi kinachoweza kupatikana.

Kutokana na tamaa hiyo inapigwa bajeti kubwa na wakati vikao vikiendelea baadhi ya mahitaji yanaanza kutolewa malipo ya awali. Mpaka kufika kwa shughuli hela haijapatikana yote na malipo ya awali yaliyolipiwa hayawez kurudishwa. Nini kinachofuata? KASORO KASORO

NB. Sikupangii jinsi ya kuandaa shughuli yako lakini si lazma ifanane au izidi ya mtu fulani. Shughuli ikiharibika hakuna anajua wanakamati! Bwana na bibi harusi ndio mnajulikana kwa hiyo lawana mtapewa nyie.
Ni hayo tu
 
Kuna ulazima wa kubadilisha huu utamaduni wa kuchangishana michango ya harusi.

Mtu ukitaka kuoa jiandae mwenyewe kifedha kisha halika ndugu na baadhi ya marafiki zako waje wahudhurie bila kuwachangisha michango.
Ukubwa wa sherehe uendane na maandalizi ya uwezo wako.
 
We umehudhuria harusi..
Kula kikichopo.. kunywa kilichopo
Wape maharusi zawadi. Piga picha..timua..


Wewe unakagua kasoro kwani unaandaa documentary ya kasoro za harusi??..

Mbona zipo harusi zina kila kitu lakini
Waalikwa hamji na zawadi..mnaishia kuwapa mikono Tu maharusi..??
 
Wachumba, Marafiki nawapa salaam kwenu.
Kwa wakristo nashauri tusome Luk 14:28 ili twende sawa. Kwa dini nyingine na wasiokuwa na dini twendeni na msamiati huu.
"Ukitaka cha uvunguni sharti uiname"
Nimehudhiria baadhi ya harusi nyingi sana hasa mwaka huu lakini mambo siyo ya kuridhisha kabisa.
Mambo yanaenda enda tu bila mipango kutokana na mambo sio powa kwa raia kwenye swala la kiuchumi changanya na covid-19 tena.

KASORO KASORO ZA KUKUMBUKWA

1. Unaenda kwenye harusi, ukumbi mzuri,mapambo mazuri lakini chakula kimeisha
2. Wanandoa wamependeza chakula cha kutosha,Bia zimeisha (kila mtu 1 tu)
3. Vinywaji vya kutosha,vyakula vyote mc& music vya kuunga unga
4. Maandalizi yote yako sawa lakini pesa ya Video shooting na picha haitoshi "atakopwa"

Kukosekana kwa kimojawapo kati ya hivyo ni rahisi sana kuharibu shughuli yote na kukumbukwa na wahudhuriaji.

MASWALI YA KUJIULIZA KABLA YA MIPANGO
Bajeti yangu inatosha kufanya sherehe hii?
Jiangalie wewe kama wewe je nina shilingi ngapi?
Kama kuna michango je itanitosha?
Kama isipotosha nawezaje kufanikisha hii?

Kuboronga kwa shughuli nyingi kunatokana na mipango mibovu na tamaa ya waandaaji bila kuzingatia kiasi halisi kinachoweza kupatikana.

Kutokana na tamaa hiyo inapigwa bajeti kubwa na wakati vikao vikiendelea baadhi ya mahitaji yanaanza kutolewa malipo ya awali. Mpaka kufika kwa shughuli hela haijapatikana yote na malipo ya awali yaliyolipiwa hayawez kurudishwa. Nini kinachofuata? KASORO KASORO

NB. Sikupangii jinsi ya kuandaa shughuli yako lakini si lazma ifanane au izidi ya mtu fulani. Shughuli ikiharibika hakuna anajua wanakamati! Bwana na bibi harusi ndio mnajulikana kwa hiyo lawana mtapewa nyie.
Ni hayo tu
Mkuu unapigiania haki ya kula na kunywa kwenye sherehe za harusi...

Hongera mzamiaji nguli
 
We umehudhuria harusi..
Kula kikichopo.. kunywa kilichopo
Wape maharusi zawadi. Piga picha..timua..


Wewe unakagua kasoro kwani unaandaa documentary ya kasoro za harusi??..

Mbona zipo harusi zina kila kitu lakini
Waalikwa hamji na zawadi..mnaishia kuwapa mikono Tu maharusi..??
Umetoa lak 2 ukute kuna kasoro kesho utachanga tena?
 
Makanisa mengi yana kumbi tatizo lao sherehe mwisho saa sita usiku na mengine hawataki Pombe. Ukumbi wa kanisa huwa ni bei nafuu.
Wakatoliki maranyingi ni waelewa sana katika swala la pombe.

Watu 100 ni rahisi kwahudumia. Unaweza kuwa na cateraar wawili wa muda tofauti na vyakula tofauti. Kabla ya kumaliza harusi cateraar wa suop na mtori. Watu mia unaweka meza 10 kila meza watu 10. Kila meza unaweka mzinga wa brandy, bia mchanganyiko 5, wine 🍷 na soda. Kila mtu anywe anachopenda.
 
Hongera kama unachukua michango ya harusi afu unaboronga
Anayechangia harusi kama kiingilio anakosea na ukiandaa harusi kama Event za akina Kiba unauza tiketi unamakosa. :)

Wewe na mchumba wako.. mnachumbiana miaka miwili.. mnapanga januari kwamba ikifika octoba tutafunga ndoa. Na kufanya harusi yakusherehekea ndoa yenu.

Mnajua Mnamaswahiba wangapi, wanafamilia wangapi.. na mnapanga kuifanyia wapi. Kwa bajeti gani.

Kisha mnaangalia sources, mnashirikiana na jamaa wa karibu na familia kuraise funds kwa namna isiyoumiza.. mkiona bajeti inagonga sana mnashusha viwango..

Maana lengo ni kujumuika na kufurahia na sio kuonesha watu ufahari. Ukileta ufahari unakuwa siku ya harusi paji la uso limekung'ara kama kioo, jasho linalowesha tu shati, huna amani na uso umekuchujuka kwa stress..

Be in your means make it memorable by experience nzuri sio kwa stress ...kwako na kwa wadau ambao mpaka unagombana nao na kuwachukia kisa hawajakuchangia unasahau shida haijifichi.. huenda mtu anauguza kijijini... Anakupaje pesa ya ubwabwa wakati kuna mtu anataka dawa apone!?

Own your happiness.. na harusi sio nyama choma even kwamba tunalipa kiingilio... Na ukichanga kwa watu uchangie out of the goodness of heart.. sio unatoa halafu unaenda kuangalia wamekusevia nini harusini .. its pathetic.
 
Anayechangia harusi kama kiingilio anakosea na ukiandaa harusi kama Event za akina Kiba unauza tiketi unamakosa. :)

Wewe na mchumba wako.. mnachumbiana miaka miwili.. mnapanga januari kwamba ikifika octoba tutafunga ndoa. Na kufanya harusi yakusherehekea ndoa yenu.

Mnajua Mnamaswahiba wangapi, wanafamilia wangapi.. na mnapanga kuifanyia wapi. Kwa bajeti gani.

Kisha mnaangalia sources, mnashirikiana na jamaa wa karibu na familia kuraise funds kwa namna isiyoumiza.. mkiona bajeti inagonga sana mnashusha viwango..

Maana lengo ni kujumuika na kufurahia na sio kuonesha watu ufahari. Ukileta ufahari unakuwa siku ya harusi paji la uso limekung'ara kama kioo, jasho linalowesha tu shati, huna amani na uso umekuchujuka kwa stress..

Be in your means make it memorable by experience nzuri sio kwa stress ...kwako na kwa wadau ambao mpaka unagombana nao na kuwachukia kisa hawajakuchangia unasahau shida haijifichi.. huenda mtu anauguza kijijini... Anakupaje pesa ya ubwabwa wakati kuna mtu anataka dawa apone!?

Own your happiness.. na harusi sio nyama choma even kwamba tunalipa kiingilio... Na ukichanga kwa watu uchangie out of the goodness of heart.. sio unatoa halafu unaenda kuangalia wamekusevia nini harusini .. its pathetic.
👏👏
 
Mm kuna mjomba wangu mpaka Leo ameninunia kisa ckumchangia kwenye harusi yake na lift hanipag tena

Ila majuzi nilimuona kwenye daladala na yeye nahisi ni madeni ya harusi yanamtoa jasho tu

Mjomba nisamehe bure
Harusi siku hizi zimekuwa kero badala ya furaha
 
Makanisa mengi yana kumbi tatizo lao sherehe mwisho saa sita usiku na mengine hawataki Pombe. Ukumbi wa kanisa huwa ni bei nafuu.
Wakatoliki maranyingi ni waelewa sana katika swala la pombe.

Watu 100 ni rahisi kwahudumia. Unaweza kuwa na cateraar wawili wa muda tofauti na vyakula tofauti. Kabla ya kumaliza harusi cateraar wa suop na mtori. Watu mia unaweka meza 10 kila meza watu 10. Kila meza unaweka mzinga wa brandy, bia mchanganyiko 5, wine na soda. Kila mtu anywe anachopenda.
ukipata kadi ya mualiko wa harusi inayo-organiziwa kma unavosema tafadhali sana naomba unishtue!.
 
kinachonikera mimi ni kua nikirudi kuongeza msosi wananinyooshea vidole qmmke!..

Harusi yangu nitajitahidi 70% ya michango na maandalizi itoke kwetu wenyewe, na michango ya wengine iwe extra yaani wachangie kudumisha umoja tu na ndugu jamaa na marafiki watahudhuria hta kma mtu hajachangia..
 
Back
Top Bottom