Ushauri kwa Serikali kuhusu utaratibu wa kutumia kadi ya kieletroniki Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,754
Tangu jana tarehe 20 Februari 2023 serikali imeweka utartibu mpya kwenye kituo cha mabasi cha Kimataifa cha Magufuli Bus Terminal pale Mbezi; ambao kimantiki ni utaratibu mujarabu unaoleta tija kwa jamii. Utaratibu wa kutumia kadi ya kieletronic ya N-Card kwa wananchi wanaoingia ndani.

Mantiki yake kama nionavyo mimi Msanii Mkuu wa Taifa ni:-
  1. Ufanisi wa kutunza muda wa wananchi wanaolazimika kupanga foleni kwa wakatisha tiketi pale kwenye mageti ya kuingilia
  2. Udhibiti wa upotevu wa mapato ya serikali unaotokana na kukosekana kwa usimamizi thabiti wa tiketi zinazotumika kuingilia ambapo inarahisisha wahuni kuchapisha zao na kutafuna pesa ya umma
  3. Kuondoka kwa wakandarasi wa kukusanya mapato ya kiingilio ambao walikuwa wanagawana na serikali kwa kila shilingi inahokusanywa ukiondoa zile zinazoingia mifukoni mwao moja kwa moja.
  4. Kuithaminisha N-Card ambayo kimsingi ni matokeo ya utafiti wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambao ilianzia kutumika Sabasaba, vivuko vya Kigamboni, kuingilia kwenye viwanja vya soka na sasa inaendelea kuunganishwa na huduma nyingi za umma hivyo kuleta urahisi wa upataji huduma kwenye maeneo ya umma.
Hata hivyo, hakuna maendeleo yasiyoambatana na changamoto ambazo zinaweza kuwa za kijamii au upande wa wasimamizi.

Serikali kupitia maelezo yake imesema matumizi ya kadi hizo ni kwa majaribio au uangalizi wa wiki kadhaa kuangalia utendaji wake na ufanisi wake. Sambamba na hilo imeweka utaratibu mpya wa kila anayeingia yaani wasindikizaji na abiria atalazimika kulipia kiingilio ambapo watalazimika kununua kadi au kutumia kadi za papo hapo ili waweze kuingia ndani ya kituo. Lengo zuri la serikali kukusanya mapato kama tulivyoiagiza kupitia sheria ya fedha iliyopitishwa na wawakilishi wetu Bungeni linaweza pia kuleta ukakasi kwenye utekelezaji wake. Hapa yanahitajika maelezo ya kina kutuelewesha wenye nchi mantiki ya utaratibu mpya wa abiria ambaye anakata tiketi yake kwa njia ya kieletronic na kulipia kodi ya serikali na pia ambaye kimantiki waendesha huduma za usafiri wanalipia kuingia pale kituoni kwa kuwachukua abiria ambao tayari kupitia tiketi zao wameshachangia pato la nchi.

Inawezekana lengo la serikali ni kutumia mapato yatokanayo na stendi kuu kuboresha huduma za jamii ikiwemo stendi husika. Lakini hii fractional collection iliyobuniwa inazidi kuleta ukakasi kwa wanaouangalia uchumi wetu kwa uwiano na vipato vya wananchi.

Katika hili ningependa kutoa ushauri wangu kwa serikali:-
  1. Serikali itafakari upya hili suala la abiria wenye ticketi zao mkononi kulipia tena kuingilia kituo kikuu cha Magufuli. Hapo awali abiria walikuwa hawalipii lakini kuanzia tarehe 20 Februari wameanza kulipia na imezua manung'uniko makubwa. Tunaamini mkoa ndiyo wanaosimamia mapato ya pale hivyo wwtaalam watafakari namna ya kumpunguzia mzigo wa makato abiria ama wananchi wanaotumia kituo kikuu.
  2. Katika mapato yanayotokana na viingilio vya maeneo ya umma kama vile Kituo Kikuu cha Magufuli, Daraja la Nyerere na Kivuko cha Magogoni; serikali itenge asilimia 20% ya kila mapato ya siku iingie kwenye fungu la maboresho ya eneo husika. Nalisema hili kwa sababu mapato makubwa yanayokusanywa maeneo hayo hayalingani hadhi ya mapato yanayokusanywa. Leo ukipita daraja la Kigamboni utaona mkundombinu inayohitaji ukarabati wa mara kwa mara, ukienda fery ndiyo kabisaa hali si nzuri kwa sababu yale majengo ya kusubiria abiria ni hatarishi hayana escape safe plan endapo dharura itajitokeza. Pia msongamano unawezesha magonjwa ya maambukizo kwa njia ya hewa. Vivuko yaani pantoni hazifanyiwi ukarabati wa kikalenda ambapo hupelekea hasara kubwa kwa serikali kugharimia matengenezo makubwa ambapo ukararabati wa kawaida ungeweza kuepusha hasara kwa fedha za umma. Maeneo yote yanahitaji maboresho ambapo serikali ikiamua kutenga asilimia 20% ya mapato ya kila siku na kusimamia vyema itawezesha maeneo yetu kuwa na mwonekano wa kimataifa
  3. Serikali ione umuhimu wa N-Card kutumiwa kwenye maeneo mengi ya huduma za umma kama vile TANAPA, UDART yaani mabasi ya Mwendokasi na zitumike kwenye malipo ya huduma za kumwona daktari hospitali za umma kwa wananchi wasio na bima ya Afya.
  4. Serikali kupitia BOT kuanzisha dirisha la N-Card kwenye mabenki ili kuwezesha wananchi kurefill cards zao kwa urahisi. Benki nyingi zinaendesha huduma za uwakala mitaani hivyo wananchi hawatolazimika kupanga foleni ndefu kurefill cards zao kwenye mageti ya huduma husika.
  5. Serikali itoe elimu kwa umma bila kuchoka kuhusu umuhimu na manufaa ya matumizi ya electronic cards kwenye huduma za umma.
  6. Serikali iweke uangalizi
Mimi ni muumini wa maendeleo hususani maendeleo yanayonasibisha na ukuaji wa kisayansi na teknolojia.

Nawasilisha
 
Wazo zuri. Bila shaka serikali italichukulia kwa marefu na mapana yake ktk kudhibiti upotevu wa mapato na kuboresha huduma kwa maana ya sustainable development.

Haiwezekani nchi yetu kongwe na yenye vyanzo kedekede vya mapato idharaulike kimataifa kwa comparison na viinchi uchwara kama Rwanda kwenye maswala ya ustaarab na maendeleo!
 
👍👍 Ila wasiwasi wangu watanzania Kwa wizi wanaweza alibu ikawa kama mwanzo mashine za mwendokasi
 
Wazo zuri. Bila shaka serikali italichukulia kwa marefu na mapana yake ktk kudhibiti upotevu wa mapato na kuboresha huduma kwa maana ya sustainable development.

Haiwezekani nchi yetu kongwe na yenye vyanzo kedekede vya mapato idharaulike kimataifa kwa comparison na viinchi uchwara kama Rwanda kwenye maswala ya ustaarab na maendeleo!
Tanzania tumewekeza kwenye siasa ndo maana kura zinanunuliwa
 
Tangu jana tarehe 20 Februari 2023 serikali imeweka utartibu mpya kwenye kituo cha mabasi cha Kimataifa cha Magufuli Bus Terminal pale Mbezi; ambao kimantiki ni utaratibu mujarabu unaoleta tija kwa jamii. Utaratibu wa kutumia kadi ya kieletronic ya N-Card kwa wananchi wanaoingia ndani.

Mantiki yake kama nionavyo mimi Msanii Mkuu wa Taifa ni:-
  1. Ufanisi wa kutunza muda wa wananchi wanaolazimika kupanga foleni kwa wakatisha tiketi pale kwenye mageti ya kuingilia
  2. Udhibiti wa upotevu wa mapato ya serikali unaotokana na kukosekana kwa usimamizi thabiti wa tiketi zinazotumika kuingilia ambapo inarahisisha wahuni kuchapisha zao na kutafuna pesa ya umma
  3. Kuondoka kwa wakandarasi wa kukusanya mapato ya kiingilio ambao walikuwa wanagawana na serikali kwa kila shilingi inahokusanywa ukiondoa zile zinazoingia mifukoni mwao moja kwa moja.
  4. Kuithaminisha N-Card ambayo kimsingi ni matokeo ya utafiti wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambao ilianzia kutumika Sabasaba, vivuko vya Kigamboni, kuingilia kwenye viwanja vya soka na sasa inaendelea kuunganishwa na huduma nyingi za umma hivyo kuleta urahisi wa upataji huduma kwenye maeneo ya umma.
Hata hivyo, hakuna maendeleo yasiyoambatana na changamoto ambazo zinaweza kuwa za kijamii au upande wa wasimamizi.

Serikali kupitia maelezo yake imesema matumizi ya kadi hizo ni kwa majaribio au uangalizi wa wiki kadhaa kuangalia utendaji wake na ufanisi wake. Sambamba na hilo imeweka utaratibu mpya wa kila anayeingia yaani wasindikizaji na abiria atalazimika kulipia kiingilio ambapo watalazimika kununua kadi au kutumia kadi za papo hapo ili waweze kuingia ndani ya kituo. Lengo zuri la serikali kukusanya mapato kama tulivyoiagiza kupitia sheria ya fedha iliyopitishwa na wawakilishi wetu Bungeni linaweza pia kuleta ukakasi kwenye utekelezaji wake. Hapa yanahitajika maelezo ya kina kutuelewesha wenye nchi mantiki ya utaratibu mpya wa abiria ambaye anakata tiketi yake kwa njia ya kieletronic na kulipia kodi ya serikali na pia ambaye kimantiki waendesha huduma za usafiri wanalipia kuingia pale kituoni kwa kuwachukua abiria ambao tayari kupitia tiketi zao wameshachangia pato la nchi.

Inawezekana lengo la serikali ni kutumia mapato yatokanayo na stendi kuu kuboresha huduma za jamii ikiwemo stendi husika. Lakini hii fractional collection iliyobuniwa inazidi kuleta ukakasi kwa wanaouangalia uchumi wetu kwa uwiano na vipato vya wananchi.

Katika hili ningependa kutoa ushauri wangu kwa serikali:-
  1. Serikali itafakari upya hili suala la abiria wenye ticketi zao mkononi kulipia tena kuingilia kituo kikuu cha Magufuli. Hapo awali abiria walikuwa hawalipii lakini kuanzia tarehe 20 Februari wameanza kulipia na imezua manung'uniko makubwa. Tunaamini mkoa ndiyo wanaosimamia mapato ya pale hivyo wwtaalam watafakari namna ya kumpunguzia mzigo wa makato abiria ama wananchi wanaotumia kituo kikuu.
  2. Katika mapato yanayotokana na viingilio vya maeneo ya umma kama vile Kituo Kikuu cha Magufuli, Daraja la Nyerere na Kivuko cha Magogoni; serikali itenge asilimia 20% ya kila mapato ya siku iingie kwenye fungu la maboresho ya eneo husika. Nalisema hili kwa sababu mapato makubwa yanayokusanywa maeneo hayo hayalingani hadhi ya mapato yanayokusanywa. Leo ukipita daraja la Kigamboni utaona mkundombinu inayohitaji ukarabati wa mara kwa mara, ukienda fery ndiyo kabisaa hali si nzuri kwa sababu yale majengo ya kusubiria abiria ni hatarishi hayana escape safe plan endapo dharura itajitokeza. Pia msongamano unawezesha magonjwa ya maambukizo kwa njia ya hewa. Vivuko yaani pantoni hazifanyiwi ukarabati wa kikalenda ambapo hupelekea hasara kubwa kwa serikali kugharimia matengenezo makubwa ambapo ukararabati wa kawaida ungeweza kuepusha hasara kwa fedha za umma. Maeneo yote yanahitaji maboresho ambapo serikali ikiamua kutenga asilimia 20% ya mapato ya kila siku na kusimamia vyema itawezesha maeneo yetu kuwa na mwonekano wa kimataifa
  3. Serikali ione umuhimu wa N-Card kutumiwa kwenye maeneo mengi ya huduma za umma kama vile TANAPA, UDART yaani mabasi ya Mwendokasi na zitumike kwenye malipo ya huduma za kumwona daktari hospitali za umma kwa wananchi wasio na bima ya Afya.
  4. Serikali kupitia BOT kuanzisha dirisha la N-Card kwenye mabenki ili kuwezesha wananchi kurefill cards zao kwa urahisi. Benki nyingi zinaendesha huduma za uwakala mitaani hivyo wananchi hawatolazimika kupanga foleni ndefu kurefill cards zao kwenye mageti ya huduma husika.
  5. Serikali itoe elimu kwa umma bila kuchoka kuhusu umuhimu na manufaa ya matumizi ya electronic cards kwenye huduma za umma.
  6. Serikali iweke uangalizi
Mimi ni muumini wa maendeleo hususani maendeleo yanayonasibisha na ukuaji wa kisayansi na teknolojia.

Nawasilisha
Hivi kama mama anasafiri na watoto wake zaidi ya moja, hawawezi kutumia N-Kadi moja ya mama kuwapitisha hapo ?
 
Kuhusu wananchi waliokata tiketi kulipia hio gharama ya kiingilio nimemsikiliza msemaji wa wilaya ya Ubungo anasema stend ni mali ya halmashauri na pale kwenye tiketi hakuna mgao wowote unaoenda kwa halmashauri hivyo wao kama halmashauri ambao ndo wanakazi ya kutunza ile stand wanakuwa wanapata hasara

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Hivi kama mama anasafiri na watoto wake zaidi ya moja, hawawezi kutumia N-Kadi moja ya mama kuwapitisha hapo ?
Sidhani kama watoto wanalipidhwa, however, hizi mambo za double taxation zinaudhi sana....honestly
 
Tangu jana tarehe 20 Februari 2023 serikali imeweka utartibu mpya kwenye kituo cha mabasi cha Kimataifa cha Magufuli Bus Terminal pale Mbezi; ambao kimantiki ni utaratibu mujarabu unaoleta tija kwa jamii. Utaratibu wa kutumia kadi ya kieletronic ya N-Card kwa wananchi wanaoingia ndani.

Mantiki yake kama nionavyo mimi Msanii Mkuu wa Taifa ni:-
  1. Ufanisi wa kutunza muda wa wananchi wanaolazimika kupanga foleni kwa wakatisha tiketi pale kwenye mageti ya kuingilia
  2. Udhibiti wa upotevu wa mapato ya serikali unaotokana na kukosekana kwa usimamizi thabiti wa tiketi zinazotumika kuingilia ambapo inarahisisha wahuni kuchapisha zao na kutafuna pesa ya umma
  3. Kuondoka kwa wakandarasi wa kukusanya mapato ya kiingilio ambao walikuwa wanagawana na serikali kwa kila shilingi inahokusanywa ukiondoa zile zinazoingia mifukoni mwao moja kwa moja.
  4. Kuithaminisha N-Card ambayo kimsingi ni matokeo ya utafiti wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambao ilianzia kutumika Sabasaba, vivuko vya Kigamboni, kuingilia kwenye viwanja vya soka na sasa inaendelea kuunganishwa na huduma nyingi za umma hivyo kuleta urahisi wa upataji huduma kwenye maeneo ya umma.
Hata hivyo, hakuna maendeleo yasiyoambatana na changamoto ambazo zinaweza kuwa za kijamii au upande wa wasimamizi.

Serikali kupitia maelezo yake imesema matumizi ya kadi hizo ni kwa majaribio au uangalizi wa wiki kadhaa kuangalia utendaji wake na ufanisi wake. Sambamba na hilo imeweka utaratibu mpya wa kila anayeingia yaani wasindikizaji na abiria atalazimika kulipia kiingilio ambapo watalazimika kununua kadi au kutumia kadi za papo hapo ili waweze kuingia ndani ya kituo. Lengo zuri la serikali kukusanya mapato kama tulivyoiagiza kupitia sheria ya fedha iliyopitishwa na wawakilishi wetu Bungeni linaweza pia kuleta ukakasi kwenye utekelezaji wake. Hapa yanahitajika maelezo ya kina kutuelewesha wenye nchi mantiki ya utaratibu mpya wa abiria ambaye anakata tiketi yake kwa njia ya kieletronic na kulipia kodi ya serikali na pia ambaye kimantiki waendesha huduma za usafiri wanalipia kuingia pale kituoni kwa kuwachukua abiria ambao tayari kupitia tiketi zao wameshachangia pato la nchi.

Inawezekana lengo la serikali ni kutumia mapato yatokanayo na stendi kuu kuboresha huduma za jamii ikiwemo stendi husika. Lakini hii fractional collection iliyobuniwa inazidi kuleta ukakasi kwa wanaouangalia uchumi wetu kwa uwiano na vipato vya wananchi.

Katika hili ningependa kutoa ushauri wangu kwa serikali:-
  1. Serikali itafakari upya hili suala la abiria wenye ticketi zao mkononi kulipia tena kuingilia kituo kikuu cha Magufuli. Hapo awali abiria walikuwa hawalipii lakini kuanzia tarehe 20 Februari wameanza kulipia na imezua manung'uniko makubwa. Tunaamini mkoa ndiyo wanaosimamia mapato ya pale hivyo wwtaalam watafakari namna ya kumpunguzia mzigo wa makato abiria ama wananchi wanaotumia kituo kikuu.
  2. Katika mapato yanayotokana na viingilio vya maeneo ya umma kama vile Kituo Kikuu cha Magufuli, Daraja la Nyerere na Kivuko cha Magogoni; serikali itenge asilimia 20% ya kila mapato ya siku iingie kwenye fungu la maboresho ya eneo husika. Nalisema hili kwa sababu mapato makubwa yanayokusanywa maeneo hayo hayalingani hadhi ya mapato yanayokusanywa. Leo ukipita daraja la Kigamboni utaona mkundombinu inayohitaji ukarabati wa mara kwa mara, ukienda fery ndiyo kabisaa hali si nzuri kwa sababu yale majengo ya kusubiria abiria ni hatarishi hayana escape safe plan endapo dharura itajitokeza. Pia msongamano unawezesha magonjwa ya maambukizo kwa njia ya hewa. Vivuko yaani pantoni hazifanyiwi ukarabati wa kikalenda ambapo hupelekea hasara kubwa kwa serikali kugharimia matengenezo makubwa ambapo ukararabati wa kawaida ungeweza kuepusha hasara kwa fedha za umma. Maeneo yote yanahitaji maboresho ambapo serikali ikiamua kutenga asilimia 20% ya mapato ya kila siku na kusimamia vyema itawezesha maeneo yetu kuwa na mwonekano wa kimataifa
  3. Serikali ione umuhimu wa N-Card kutumiwa kwenye maeneo mengi ya huduma za umma kama vile TANAPA, UDART yaani mabasi ya Mwendokasi na zitumike kwenye malipo ya huduma za kumwona daktari hospitali za umma kwa wananchi wasio na bima ya Afya.
  4. Serikali kupitia BOT kuanzisha dirisha la N-Card kwenye mabenki ili kuwezesha wananchi kurefill cards zao kwa urahisi. Benki nyingi zinaendesha huduma za uwakala mitaani hivyo wananchi hawatolazimika kupanga foleni ndefu kurefill cards zao kwenye mageti ya huduma husika.
  5. Serikali itoe elimu kwa umma bila kuchoka kuhusu umuhimu na manufaa ya matumizi ya electronic cards kwenye huduma za umma.
  6. Serikali iweke uangalizi
Mimi ni muumini wa maendeleo hususani maendeleo yanayonasibisha na ukuaji wa kisayansi na teknolojia.

Nawasilisha
Rwanda utaratibu umekomaa wa kutumia kadi
 
Kuhusu wananchi waliokata tiketi kulipia hio gharama ya kiingilio nimemsikiliza msemaji wa wilaya ya Ubungo anasema stend ni mali ya halmashauri na pale kwenye tiketi hakuna mgao wowote unaoenda kwa halmashauri hivyo wao kama halmashauri ambao ndo wanakazi ya kutunza ile stand wanakuwa wanapata hasara

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
Mkuu rejea kwenye andiko langu.
Nimesema asilimia 20% ya mapato ya siku ni pendekezo la kuiacha pale Halmashauri kwa minajili ya kutunza kituo kile.

Naelewa sana mfumo wa serikali kuu kumiliki vyanzo vya mapato ambavyo kimsingi ilipaswa kushirikiana na Halmashauri zetu...
 
Tangu jana tarehe 20 Februari 2023 serikali imeweka utartibu mpya kwenye kituo cha mabasi cha Kimataifa cha Magufuli Bus Terminal pale Mbezi; ambao kimantiki ni utaratibu mujarabu unaoleta tija kwa jamii. Utaratibu wa kutumia kadi ya kieletronic ya N-Card kwa wananchi wanaoingia ndani.

Mantiki yake kama nionavyo mimi Msanii Mkuu wa Taifa ni:-
  1. Ufanisi wa kutunza muda wa wananchi wanaolazimika kupanga foleni kwa wakatisha tiketi pale kwenye mageti ya kuingilia
  2. Udhibiti wa upotevu wa mapato ya serikali unaotokana na kukosekana kwa usimamizi thabiti wa tiketi zinazotumika kuingilia ambapo inarahisisha wahuni kuchapisha zao na kutafuna pesa ya umma
  3. Kuondoka kwa wakandarasi wa kukusanya mapato ya kiingilio ambao walikuwa wanagawana na serikali kwa kila shilingi inahokusanywa ukiondoa zile zinazoingia mifukoni mwao moja kwa moja.
  4. Kuithaminisha N-Card ambayo kimsingi ni matokeo ya utafiti wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambao ilianzia kutumika Sabasaba, vivuko vya Kigamboni, kuingilia kwenye viwanja vya soka na sasa inaendelea kuunganishwa na huduma nyingi za umma hivyo kuleta urahisi wa upataji huduma kwenye maeneo ya umma.
Hata hivyo, hakuna maendeleo yasiyoambatana na changamoto ambazo zinaweza kuwa za kijamii au upande wa wasimamizi.

Serikali kupitia maelezo yake imesema matumizi ya kadi hizo ni kwa majaribio au uangalizi wa wiki kadhaa kuangalia utendaji wake na ufanisi wake. Sambamba na hilo imeweka utaratibu mpya wa kila anayeingia yaani wasindikizaji na abiria atalazimika kulipia kiingilio ambapo watalazimika kununua kadi au kutumia kadi za papo hapo ili waweze kuingia ndani ya kituo. Lengo zuri la serikali kukusanya mapato kama tulivyoiagiza kupitia sheria ya fedha iliyopitishwa na wawakilishi wetu Bungeni linaweza pia kuleta ukakasi kwenye utekelezaji wake. Hapa yanahitajika maelezo ya kina kutuelewesha wenye nchi mantiki ya utaratibu mpya wa abiria ambaye anakata tiketi yake kwa njia ya kieletronic na kulipia kodi ya serikali na pia ambaye kimantiki waendesha huduma za usafiri wanalipia kuingia pale kituoni kwa kuwachukua abiria ambao tayari kupitia tiketi zao wameshachangia pato la nchi.

Inawezekana lengo la serikali ni kutumia mapato yatokanayo na stendi kuu kuboresha huduma za jamii ikiwemo stendi husika. Lakini hii fractional collection iliyobuniwa inazidi kuleta ukakasi kwa wanaouangalia uchumi wetu kwa uwiano na vipato vya wananchi.

Katika hili ningependa kutoa ushauri wangu kwa serikali:-
  1. Serikali itafakari upya hili suala la abiria wenye ticketi zao mkononi kulipia tena kuingilia kituo kikuu cha Magufuli. Hapo awali abiria walikuwa hawalipii lakini kuanzia tarehe 20 Februari wameanza kulipia na imezua manung'uniko makubwa. Tunaamini mkoa ndiyo wanaosimamia mapato ya pale hivyo wwtaalam watafakari namna ya kumpunguzia mzigo wa makato abiria ama wananchi wanaotumia kituo kikuu.
  2. Katika mapato yanayotokana na viingilio vya maeneo ya umma kama vile Kituo Kikuu cha Magufuli, Daraja la Nyerere na Kivuko cha Magogoni; serikali itenge asilimia 20% ya kila mapato ya siku iingie kwenye fungu la maboresho ya eneo husika. Nalisema hili kwa sababu mapato makubwa yanayokusanywa maeneo hayo hayalingani hadhi ya mapato yanayokusanywa. Leo ukipita daraja la Kigamboni utaona mkundombinu inayohitaji ukarabati wa mara kwa mara, ukienda fery ndiyo kabisaa hali si nzuri kwa sababu yale majengo ya kusubiria abiria ni hatarishi hayana escape safe plan endapo dharura itajitokeza. Pia msongamano unawezesha magonjwa ya maambukizo kwa njia ya hewa. Vivuko yaani pantoni hazifanyiwi ukarabati wa kikalenda ambapo hupelekea hasara kubwa kwa serikali kugharimia matengenezo makubwa ambapo ukararabati wa kawaida ungeweza kuepusha hasara kwa fedha za umma. Maeneo yote yanahitaji maboresho ambapo serikali ikiamua kutenga asilimia 20% ya mapato ya kila siku na kusimamia vyema itawezesha maeneo yetu kuwa na mwonekano wa kimataifa
  3. Serikali ione umuhimu wa N-Card kutumiwa kwenye maeneo mengi ya huduma za umma kama vile TANAPA, UDART yaani mabasi ya Mwendokasi na zitumike kwenye malipo ya huduma za kumwona daktari hospitali za umma kwa wananchi wasio na bima ya Afya.
  4. Serikali kupitia BOT kuanzisha dirisha la N-Card kwenye mabenki ili kuwezesha wananchi kurefill cards zao kwa urahisi. Benki nyingi zinaendesha huduma za uwakala mitaani hivyo wananchi hawatolazimika kupanga foleni ndefu kurefill cards zao kwenye mageti ya huduma husika.
  5. Serikali itoe elimu kwa umma bila kuchoka kuhusu umuhimu na manufaa ya matumizi ya electronic cards kwenye huduma za umma.
  6. Serikali iweke uangalizi
Mimi ni muumini wa maendeleo hususani maendeleo yanayonasibisha na ukuaji wa kisayansi na teknolojia.

Nawasilisha
Unapoandika Kituo cha Kimataifa
Ulikuwa unamaanisha Nini??
 
Kuhusu wananchi waliokata tiketi kulipia hio gharama ya kiingilio nimemsikiliza msemaji wa wilaya ya Ubungo anasema stend ni mali ya halmashauri na pale kwenye tiketi hakuna mgao wowote unaoenda kwa halmashauri hivyo wao kama halmashauri ambao ndo wanakazi ya kutunza ile stand wanakuwa wanapata hasara

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
Kwani wamiliki wa mabaki hawalipi ushuru wa stendi?
Kama wanalipa ushuru wa stendi, hizo pesa zinatoka wapi kama sio kwa wasafiri wanaonunua tiketi za kusafiri?
 
Mkuu rejea kwenye andiko langu.
Nimesema asilimia 20% ya mapato ya siku ni pendekezo la kuiacha pale Halmashauri kwa minajili ya kutunza kituo kile.

Naelewa sana mfumo wa serikali kuu kumiliki vyanzo vya mapato ambavyo kimsingi ilipaswa kushirikiana na Halmashauri zetu...
Hiyo 20% ikiachwa pale itaishia mifukoni kwa wajanja na hakuna maboresho yoyote yatatokea.
 
Hiyo 20% ikiachwa pale itaishia mifukoni kwa wajanja na hakuna maboresho yoyote yatatokea.
Tukiwa na akili au mawazo aina hii ni wazi hatutafika popote.

Je hizo zinazokusanywa una uhakika gani kama haziliwi?


Kikubwa ni Katiba mpya isimamie uwajibikaji tena uwajibikaji kwa vitendo
 
Back
Top Bottom