Ushauri kwa mamlaka kuhusu sukari iliyoagizwa toka nje ya nchi

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
380
763
Tunaishukuru Serikali kwa kusikia kilio cha Wananchi na hatimaye kuweza kuagiza sukari toka nje ya nchi kufidia upungufu uliojitokeza. Ninaishauri Serikali kuwa sukari yote iliyoagizwa kwanza ipimwe na TBS kabla haijaingia sokoni ili kuridhika na ubora wake ndipo wananchi waanze kuuziwa. Kuna mfano wa nchi jirani. wafanyabiashara wachache wajanja waliagiza sukari iliyoisha muda wake na baadaye sana ndo Serikali ikaja ikagundua na tayari sehemu kubwa iliishauziwa wananchi. Nashauri tusifikie hapo. Lindeni kwanza afya za Watanzania na tusije tukaingizwa chaka.
 
Back
Top Bottom