Mzalendo_Mwandamizi
JF-Expert Member
- Dec 12, 2007
- 1,116
- 4,773
Wameamua kuja huku mitandaoni kwa kujua wanachokifanya mkuu, wasilolijua tu ni namna wanavyochimbia kaburi lao kwa namna yapekee kabisa. Mihemuko inaanza kuongoza watu na wao wanaongoza watu wengine.
Naandaa makala ambayo nitaimwaga hapa hapa ukumbini!
Yaani mkuu, kila nikilisoma hilo bandiko la Mheshimiwa Lema natamani kuhisi kuwa labda ID yake hapa JF imekuwa hijacked lakini yaelekea ni yeye mwenyewe. Sadly, baadhi ya viongozi/wanaharakati wa Chadema (nimewaona kama wawili hivi kwenye bandiko hili) wanaonekana kushabikia uamuzi huu usio na manufaa kwa Chma chao Hofu yangu si kusambaratika kwa Chadema kwani hata kwenye Biblia tunafundishwa kuwa "Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe na "acheni wafu wazike wafu wenzao." Kinachonitatiza ni kuona chama ambacho angalau kilianza kuonekana kama mbadala wa keli didi ya CCM kikiingia kwenye utoto mbaya zaidi ya tunaoushuhudia huko CCM.
Kwa hakika inasikitisha sana