Zitto sio size yako we kilaza,mipango mikubwa ya kumwangamiza Zitto imeshindwa tena ikiratibiwa ns watu wenye akili zao.mfano ni siku mlipo mzushia kuwa amehongwa na mafisadi ili kukwamisha bajeti ya Nishati na madini, Mlimsema,mkamkejeli ,mkamsimanga kwa hoja za uongo na uzushi,kila aliesimama alidai anao ushahidi usio na shaka,lkn mwisho wa siku kila alieitwa kutoa ushahidi alikosa cha kusema na kudai eti alisoma gazeti,wengine mkasema mlinogewa na mjadala.hivyo mwisho wa siku Tanzania nzima ikajuwa kuwa zitto ni mwadilifu na ni mfano bora wa kuigwa kwa kila mwenye mapenzi mema na nchi.
Hamkuishia hapo mmekua mkifanya kila kinachowezekana kumchafua Zitto ikiwa no pamoja na kutumia magazeti yenu ya Mwanahalisi,mawio na Tanzania daima,lkn imeshindikana maana nyota yake inang`aa na hiziwiliki.sasa mawio wamekugeuka na wameanza kukuona mwengawazimu usiejua ulitendalo,toleo la juzi umeonywa lkn naona kichwa chako ni kama kofia tuu.
Sasa tazama singo uliyokuja nayo,yote hii lengo umprovoke zitto ili mpate pakuanzia.mbaya zaidi huna kikosi kazi chanye akili zaidi ya kushauriana na watu waliokata tamaa ya maisha kama aki na kilewo na saa nane.wakati Zitto akiwaza namna ya kuwakomboa watanzania ,ninyi mnawaza namna ya kukwamisha ili asipate umaarufu.
Slaa na Mbowe kukaa kwenu kimya juu ya haya yanayoendelea ni uthibitisho tosha kuwa ninyi ndio mnaoratibu mpango huu haramu,Tumewavumilia sasa tumechoka,chama si mali ya Mtei tena bali ni mali ya wanachadema ambao wengi hawatoki kilimanjaro na Arusha.kama yote haya lengo nikutaka mbaki ktk uongozi bila ridhaa ya wanachama waliowengi basi jueni kuwa mnakosea sana,mlichelewa sana kwa kuwa kufanya hivyo kutatufanya kila mtu kuondoka na fito yake.chama hakiwezi baki salama.
Zitto endelea kuwajibika kuwatumikia watanzania waliokutuma,Shughulika na mambo ya kitaifa,waache hawa wavuta bangi waimbe taarabu maana hawana kazi ya kufanya,maana tumeshaambiwa kuwa Elimu ya mjinga ni majungu.
Chapa kazi MANDELA wa Tanzania usiependa kuona wanafiki wakigomabania posho huku watanzania wakiwa hawana huduma za msingi.