Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Status
Not open for further replies.
acha kujitoa ufahamu! Wenye akili timamu tunajua zitto ndo mlengwa. Halaf ben tafuta level yako zitto haumwuzezi kwani hata dr na mwenyekiti wamemshndwa wanabaki kulilia pembeni!

Vijana wa mjini wanamwita zitto jinni siasa vijana wote wenye majina kawaliza kisiasa katika miaka mitatu , kuanzia na Kafulila,Mchange Mwampamba,Shonza hata kurasa za mbele za magazeti tena hakuna wala kwenye TV yeye bado yumo duh jamaa anajua kufyonza
 
Mh Lema nakuunga mkono mia kwa mia bora kuwa na wanachama / viongozi 10 hai kuliko kuwa na mizigo 100.hata siku moja huwezi kuacha ngano na magugu yaote pamoja au huwezi na hakuna haja ya kuwa na shamba kubwa la mizabubu isiyo zaa.kama niwakati wa maamuzi ndiyo sasa. Ila busara ni bora zaidi kuliko jazba tafakarini kwa umakini na Tumwombe Mungu kwa hili kwani mwendo karibia tunaumaliza
 
Acha siasa za majungu na fitina hauna uwezo wa kumshinda zitto hata akiamua agombee jimbo la Arusha mjini anashinda.
uchaguzi wa mwandiga 2010 alimshinda mbunge wa CCM kwa kura 120 wakati Lema alimuacha Batilda kwa kura 35,000 utamlinganishaje huyo jamaa
 
Chadema lazima kijipime, kijiweke Kwenye mzani, fukuzafukuza Na timuatimua sio dawa. Na tena pia kukaa Na msaliti Na mnajua ni joka hapo tena ni dhambi kabisa. Kama CDM haina mashinary ya kubomoa Na kutengeneza hawa binaadam inayoamini ni wasaliti hili litakuwa gego kubwa Lenye Pengo la udhaifu Kwa Chama kinachoamini kina ndoto chanya ya kushika hatamu Za uongozi Wa dola.

HAKUNA Nasema tena HAKUNA Chama Chenye uwezo wa kuwatimua manyoka(informers) Na wasaliti wote Ndani yake. Kufanya hivyo ni Kama kumtimua shetani Duniani, wasaliti wapo na wataendelea kuwepo tupende -tusipende. Cha muhimu ni mashinary Za Chama kuwatendea Kwa akili watu hawa Kwa mustakabali wa Chama Hadi pale watakapoasi wazi wazi wenyewe.
 
[
QUOTE=St.Apolinary;7717497]Wazo lako ni zuri sana ndugu mh.

Lakini kwanini umeamua kuleta hoja hii katika jamiiforums ilihali kuna vikao halali vya chama.
unajisema si ndio kazi yako
 
Sasa mambo yameanza kuiva, Lema huu ushauri naomba Dr Slaa auzingatie sana, manake yeye ndo mlengwa namba moja. Watu wote wanaojiusisha na Dr kwa ukaribu wafuatiliwe!!

Kuhusu Zitoo, nilishawahi kuweka thread hapa ikafutwa. Mnahitaji busara, hekima na akili. Zitto hawezi kuwashinda kumshughulikua. Kinachompa kiburi ni kitu kimoja tu. "CCM". Huyu jamaa hanatofauti na Wassira au Mwigulu au Kigwagalla. Tofauti yake ni moja, anafanya siasa za kimakundi in ccm ndani ya chadema. Harakati za Zitto hazina tija katika kukijenga cdm.

Wazo langu, tafuteni mtu mbadala wa Zitto, kazi yake kubwa ni kuja na hoja za kuneutralize hoja za Zitto, huyo mtu anaweza kuwa mshauri au mwanasiasa. Zitto hana hoja za msingi, ni mtu mwenye hoja za cheap popularity kwa watu wajinga au wasioelewa.

Mpigeni chini tu, uone ccm watakavyo mmmwaga!!
 
Chadema what is this? Mnataka kusema mmeshindwa kumaliza hili hadi hasira zinahamia huku?
Huu ni udhaifu kitaasisi!!

JF kila mtu analeta mada jadilini mada sio kugeneralise chadema imekuwa Lema duh threats hizo
 
Kua na hekima hata kidogo ndugu,sidhani kama tunataniana hapa,hata kama ni uhuru wa kutoa maoni uwe na kiwango sio uliopitiliza kama huu wa kwako.
Mkuu Deo Corleone a.k.a Mafia, kasema ukweli mtupu,hao wanaosema hawataki usaliti inabidi wapewe vitu live, na vya kiwango chao.
 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa napita tu, ila nikayakubali maoni ya huyu jamaa anaitwa "TUKO" NIMEYAKOPI NA KUYA - PASTE, MH. LEMA PLEASE YASOME TENA HAPA CHINI:


"Mimi nakukubali katika harakati za ukombozi wa taifa hili. Lakini naomba kukushauri kitu kimoja: Katika siasa kubali kutofautiana na watu fikra. Na sio kila mara unaotofautiana nao fikra basi ni maadui zako. Ni wazi kabisa kwamba Mwenyekiti wetu Mbowe angesema nawachukulia kama maadui wale wote anaotofautiana nao kifikra, CHADEMA isingekuwa hapo ilipo.

Kila shilingi ina pande mbili. Sio sahihi kumjudge mtu kwa kuangalia weakness zake peke yake. Naamini CHADEMA imefika hapo ilipo kwa juhudi kubwa za viongozi wake WOTE na wanachama wake. Na ninaposema wote nina maana ya WOTE. Sio vyema mtu mmoja au kikundi cha watu kujiona kuwa wao ni bora zaidi ya wengine. Kila mtu anayo madhaifu yake kama alivyo na mazuri yake. Hakuna mtu aliyekamilika, sio CDM, sio CCM na sio popote.

Wanasema mbwa ukishamjua jina hakusumbui Lema.... Tafakari braza..."
 
Is this real Godbless Lema?.

Mimi nilidhani Godbless Lema ni kamanda shujaa kumbe ni wale wale tunanaowasikia kila siku ambao wanafanya mawindo ya kisiasa kwa kuvizia.

CHADEMA muwe Jasiri kama sungusumgu na wakali kama simba. Kuja kulalama hapa bila hata ya kupata ujasili wa kumtaja huyo kiongozi wa wasaliti ndani ya chama huku ukiwataka CHADEMA wachukue maamuzi wakati wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu ni udhaifu wa kiwango cha juu kabisa. Ni bora hata yule anayekaa kimya.

Nani atachukua maamuzi magumu iwapo hata wajumbe wa kikao cha juu kabisa cha chama wanaogopa hata kulitaja tu jina la mkuu wa usaliti ndani ya chama.

Bandiko lako limekaa kimajungu badala ya ukweli kwa sababu unazunguka kwa hasira lakini unashindwa hata kumgusa anakukasilisha kisiasa.

Take stand, mention the culprit name and let the world know kwa sababu hii siyo puzzle game. It's real. He/she is here!.

Majungu na fitina zitaimaliza CHADEMA.
Mkuu leo sisi wa Lumumba tuekaa viti vya VIP tukitazama mpambano na myukano ndani ya zizi la CHADEMA.
Mie naenda agiza popcorn na kuangalia episode hii inaendeleaje.
Tumeaonya kutofua nguo za ndani hadharani kwa afya hawasikii.
Sasa ndio inadhihirika hawa F4F wakikamata nchi, patakuwepo na idara maalum ya Majungu.
 
Kwa mtu yeyote mnafiki na mzandiki lazima ataona Lema amepotoka. Hao hawana tofauti na huyu mnafiki tunayemjadili.

Mungi kama umenielewa utagundua napinga njia anayo hitumia Godbless J Lema maana hizi tuhuma alitakiwa azipeleke kwenye chama, yeye ni mjumbe wa kamati kuu.
Ulishamuona kiongizi wa chadema anakuja humu kutoa tuhuma kama hizi?

Kwanini katika hili tusikubaliane lema amepotoka?
hivi ni kweli chadema imeshindwa kuwashughulikia wasaliti?
Nakama chama kimeshindwa ina maana hakuna ushahidi wa kutosha.

Lema amepotoka kwenye hili lazima ajue.
 
Last edited by a moderator:
Kila siku tulisema kuwa nguzo ya CHADEMA niya kilaghai lakini kuna watu walikuwa bado hawajaelewa somo vizuri. Mwl. Nyerere alishawahi kusema "Ukweli una tabia ya kutopenda kupuuzwa". Ukweli kwa sasa umeanza kupambana na uwongo na matokeo yake ndiyo haya.

Hata wale waliokuwa wanajenga mnara wa Babeli walionekana wana akili waliopoanza lakini ukweli ulipoanza kuopambana nao matokeo yake yanaeleweka.

Mwenyezi Mungu ana ufunuo wake. Mwenyezi Mungu ameanza kuwafunulia pia wananchi wengine ili watambue true colour ya hawa matapeli wanaojiita wakombozi.

CHADEMA siyo chama cha siasa ndani ya demokrasia kwa manufaa ya demokrasia bali ni private-owned enterprise through political project.

Chama kilichojengwa kwa misingi ya kilaghai hata uendeshaji wake utakuwa niwa kilaghai.

Test ndogo tu ya kuacha kupokea posho kuonyesha kama kweli wanawapigania wananchi walalahoi imewashinda na sasa wameanza kunyosheana vidole kwa kuitana wasaliti.

These people are just political profiteers
 
Chadema what is this? Mnataka kusema mmeshindwa kumaliza hili hadi hasira zinahamia huku?
Huu ni udhaifu kitaasisi!!

Kama Mwigamba alisimamishwa uongozi kwa kutoa maoni na mtazamo wake kuhusu chadema tena kwa kutumia jina bandia, iweje huyu Lema ambaye mara zote anamwandama Zitto na sasa anataka afukuzwe kupitia JF naye asichukuliwe hatua za kinidhamu? au mkuki kwa Nguruwe? ina maana maoni ya Lema hayawezi kutolewa kwenye vikao halali vya chama?
 
Kamanda ,atakayeshindwa kukielewa ulichokiandika hata ukimuuliza yeye ni nani atashindwa kujieleza...Maelezo yanajitosheleza na asiye elewa ameamua hivyo kwa makusudi na haitaji kueleweshwa zaidi ni kupoteza muda kazi hiyo ni muhimu na ifanyike haraka sana iwezekanavyo ..Usimpe mbwa chakula cha watoto Kamanda..

Ina maana unata kusema analo fanya lema lina jenga chama? umepotoka kabisa.
 
Tatizo tamaa ya madaraka MTU HAJALALA MAHABUSU HATA SIKU MOJA anataka uenyekiti,urais huku umri hauruhusu na hajaenda vijijini sana kukijenga chama

maneno yako makali wee, hiv kwel ajalala jela? Zana za kilimo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom