Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Status
Not open for further replies.
Karibu jamvini Lema.

Kwanza nikupongeze kwa kujiunga na na JF, lakini pia nikupe tahadhari kidogo ninajua unamzungumzia nani na ninajua pia wanajamvi wakongwe wanafahamu kinachoendela CDM. Mpaka sasa chama chako kiko kwenye right track hapana sababu ya kukurupuka katika kuchukua maamuzi lazima maamuzi magumu yaambatane na tahadhari kubwa unaweza kuchukua hatua stahiki leo lakini ukajikuta unakirudisha chama hatua kadhaa nyuma.

Pili wewe ni kiongozi mkubwa nina amini unaingia kwenye vikao vya maamuzi ningependa kukushauri mawazo na ushauri wako ni bora ukaupeleka katika vikao husika na si kwenye mitandao ya kijamii. Kufanya hivo ni kuwapatia maadui wa chama chako nafasi ya kuzidi kukihujumu zaidi.

Natumaini utaufuata ushauri wangu.
 
Lawyer wangu naona unapindisha uhalisia. Kwanza huyo msaliti anatakiwa ajue kuwa watu wanamjua. Sasa kama atajitaja mwenyewe kama Mwigamba ruksa. akikataa atatajwa kwa lazima.
Hii pia ni elimu muhimu kwa siasa ya Tanzania. Kwa maana kila msaliti ndani ya chama cha siasa ana lengo, either ametumwa na chama ambacho inaona chama kingine ni threat kwake, ama kwa utashi wake wa kisiasa. All in all usaliti ni usaliti.
Kusema kwamba kwanini asitajwe inajenga taswira tofauti na maudhui ya mtoa mada.


Ninacho pingana na yeye ni kuja kulalama humu, hivi huyo msaliti kamjua leo?
Hivi kwa nini asipeleke ushahidi hili achukuliwe hatua?
Mimi naamini lema ana nafasi kubwa ya kupeleka malalamiko yake kwenye chama si humu.
Mungi lazima tukubali njia anayo hitumia lema si sahihi, hizi ni vurugu.

Mungi kwa pamoja tuseme hapana kwenye hili lema amepotoka.
 
Last edited by a moderator:
Godbless J Lema,
Mimi nakukubali katika harakati za ukombozi wa taifa hili. Lakini naomba kukushauri kitu kimoja: Katika siasa kubali kutofautiana na watu fikra. Na sio kila mara unaotofautiana nao fikra basi ni maadui zako. Ni wazi kabisa kwamba Mwenyekiti wetu Mbowe angesema nawachukulia kama maadui wale wote anaotofautiana nao kifikra, CHADEMA isingekuwa hapo ilipo.

Kila shilingi ina pande mbili. Sio sahihi kumjudge mtu kwa kuangalia weakness zake peke yake. Naamini CHADEMA imefika hapo ilipo kwa juhudi kubwa za viongozi wake WOTE na wanachama wake. Na ninaposema wote nina maana ya WOTE. Sio vyema mtu mmoja au kikundi cha watu kujiona kuwa wao ni bora zaidi ya wengine. Kila mtu anayo madhaifu yake kama alivyo na mazuri yake. Hakuna mtu aliyekamilika, sio CDM, sio CCM na sio popote.

Wanasema mbwa ukishamjua jina hakusumbui Lema.... Tafakari braza...
remarkable advice!! Kama lema ni muelewa ataufanyia kazi
 
Last edited by a moderator:
Your hero is an unguided missile. Linaweza kuharibu kwa adui au hata kwa ndugu na jamaa. Tazama anavyo quote watu na kujaribu kutumia misemo utadhani kiwete anayejaribu kutumia miguu yake kutembea.

baada ya kukesha usiku wa leo ukimshambulia, gaya kawajibu sasa..
 
NCCR mageuzi ilianzaga hivi hivi....kuwapa matumaini makubwa watanzania, just to find out kuwa ilikuwa a bunch of traitors na wote tunawajua. More than a decade ya serious politics za CDM, naona tunataka kurudishwa kule kule kwa 1995!
 
Lema huna lolote, wewe ni mnafiki tu, wewe si mtetezi wa wanchi, wewe huna uchungu wa wananchi, unachokipata sasa n kwa kuwa wanchi wameichoka CCM na bahati mbaya hawana uwezo mkubwa wa kupambanua mambo.

Kudhihirisha wewe ni mnafiki, kwa nini usimtaje huyo kiongozi???? Hata TANU walikuwa na ahadi zao na ahadi mojawapo ni NITASEMA KWELI DAIMA, FITINA KWANGU MWIKO, sasa wewe kama washindwa kumtaja kiongozi wa juu wa CHADEMA kuna tofauti gani na kufanya fitina na kuleta unafiki????

Ni aibu kwa kiongozi kama wewe kujitokeza hadharani nyakati kama hizi ambazo chama chako kimetoka kumsimamisha Samsoni Mwigamba kwa tuhuma za kuwasema viongozi wake, kwenye mitandao, je wewe unachomkifanya sasa kina tofauti gani na cha Mwigamba??

You are just pathetic MP!! Na kama ukombozi tunaoutafuta ni kuja kuongozwa na watu opportunists kama wewe, ni aheri tusiupate kabisa!!

So sad, so sad, so sad, kusoma huu utumbo wako Mheshimiwa, tafadhali anua nguo zako chafu ulizoanika kwenye kamba!!!
 
Jina la kiongozi wa wasaliti ni nani ?

Au ndio habari za magezetini ,Jina limehifadhiwa ?

Ukifadhi jina msaliti na wewe ni msaliti
 
Kama ni mshangao mkubwa nilio nao, ni jinsi mnavyolea mnafiki mkubwa ambaye anjidhihirisha wazi na kukichezea chama kama mwanasesere jinsi anavyotaka Shibuda.

Hakuna sababu zozote za msingi za kuendelea kuwa na Shibuda kwenye chama... Kama ni kweli alishiriki katika njama za kusingizi ugaidi ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA huyu anafaida gani kwenye chama, bora ata angekuwa akifanya hayo mambo kwa kificho lakini anafany awzi wazi na mnazidi kumchekea!

Huyu mnafiki kwa kuendeleza unafiki wake na kuwaharibia future vijana aliendelea kugawa ruzuku kama ifuatavyo:

Tarehe 26/3/2012 saa 11:12 asubuhi, MNAFIKI kupitia namba yake ya simu +2557568..53. aliwatumia shilingi 150,000/= wafuasi wa kundi lake, Juliana +255756.5..73, Habi+255.6217.6.., Mtela +2557.5..89.7, Burton +25571..167.., Eddo +25575..49..3, Grey +255755.2..0., Deo +2556.50..60., Adam +2557..137..1, Exaud Mamuya +2557671606.., Ben Saanane +255768078...(CISS),

Baada ya hapo saa 11:43 asubuhi hiyohiyo MNAFIKI kupitia namba yake ya simu +25575.8.9.3. alimtumia shilingi 200,000/= John Shibuda +2557544655..
 
Is this real Godbless Lema?.

Mimi nilidhani Godbless Lema ni kamanda shujaa kumbe ni wale wale tunanaowasikia kila siku ambao wanafanya mawindo ya kisiasa kwa kuvizia.

CHADEMA muwe Jasiri kama sungusumgu na wakali kama simba. Kuja kulalama hapa bila hata ya kupata ujasili wa kumtaja huyo kiongozi wa wasaliti ndani ya chama huku ukiwataka CHADEMA wachukue maamuzi wakati wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu ni udhaifu wa kiwango cha juu kabisa. Ni bora hata yule anayekaa kimya.

Nani atachukua maamuzi magumu iwapo hata wajumbe wa kikao cha juu kabisa cha chama wanaogopa hata kulitaja tu jina la mkuu wa usaliti ndani ya chama.

Bandiko lako limekaa kimajungu badala ya ukweli kwa sababu unazunguka kwa hasira lakini unashindwa hata kumgusa anakukasilisha kisiasa.

Take stand, mention the culprit name and let the world know kwa sababu hii siyo puzzle game. It's real. He/she is here!.

Majungu na fitina zitaimaliza CHADEMA.
 
Mkuu ukimsoma vizuri kamanda Lema utamuelewa,

Anatoa onyo kwa huyo mnafiki msaliti a.k.a Mzee wa Tunguli, kaaga Kigoma
Anatoa elimu kwa vijana tusiwe wasaliti... katoa na mifano ya vijana waliokatishwa ndoto zao za kisiasa...
Anatutia moyo ni mtu moja tu anaetuvuruga ni mnafiki hata wanaomtumia wanamuona mnafiki.

vile vile anatoa hamasa kwa vijana

Hapana lazima tukubali Godbless J Lema amepotoka kabisa anachofanya yeye kutuhumu wenzie kwenye mitandao ni sawa na mwigamba alivyo fanya. je kuna tofauti kati ya lema na mwigamba?

lema haya anayo yasema yanasaidia kumpata msaliti au kutuvuruga? Lema kwanini haya asiyapeleke kwenye vikao vya chama?

ujinga aliyo ufanya mwigamba ndio ujinga anao ufanya lema leo.

Ninapenda wote tumwambie hapana kwenye hili maana halijengi chama kabisa.
 
Last edited by a moderator:
...

Mtu huyu wote tunamjua ni matumaini yangu Usaliti wake sasa utafika kikomo kama Chama kitaamua kuwa na busara za kutosha katika kujenga siku njema zinazokuja . Mtu huyu amefanya mambo mengi mabaya katika Chama yanayohusu usaliti na amewaponza Vijana wengi na kuangamiza ndoto zao kwa sababu ya mambo yake binafsi .

...


Heshima kwako Mh. Mbunge. Sijakuelewa vizuri hapo kwenye red! How?

Nilidhani kwa kuwa wote (wanachama?) mnamjua huyo msaliti na kwa kuwa usaliti wake haukubaliki na kwa kuwa wanachama ndio wenye maamuzi ya mwisho na kwa kuwa ni kama "nyota ya jaha" kwamba Uchaguzi Mkuu wa chama ni 2014 huoni ingekuwa ndio wakati muafaka kabisa wa kumuengua huyo msaliti peacefully kupitia uchaguzi halali. Lakini to my surprise, imetangazwa uchaguzi utaahirishwa hadi baada ya Uchaguzi Mkuu wa nchi, 2015!

Kwa uamuzi huu wa kuahirisha uchaguzi wa chama huoni kama viongozi mumeamua kuendelea kuishi na huyo msaliti ambaye inaonekana naye ana title ya juu ndani ya chama? Kwanini msingetumia fursa hii njema (uchaguzi wa 2014) kumuengua kihalali bila kuacha doa au lawama kutoka kwa jamii?
 
NCCR mageuzi ilianzaga hivi hivi....kuwapa matumaini makubwa watanzania, just to find out kuwa ilikuwa a bunch of traitors na wote tunawajua. More than a decade ya serious politics za CDM, naona tunataka kurudishwa kule kule kwa 1995!
Na ili tusirudi huko ni lazima tuchukue different approach ku-deal na elements zinazofanana na zile zilizoiua NCCR-Mageuzi.Ndiyo falsafa ya kumtoa nyoka mdogo ndani
 
busara itumike kufanya maamuzi,waswahili wanamsemo wao mmoja kuwa ukiambiwa jambo jema na punguani chukua jambo jema muache na upunguani wake,sasa CHADEMA kamatunaelekea 2015 katika uchaguzi,ni vizuri kuwa na timu 1 ya ushindi,maana hata kama wapo hao mnao waita wasaliti lakini kwa sasa wana nafasi katika gurudumu la kuelekea katika uchaguzi wa 2015,CHADEMA ni taasisi kubwa,nilazima tuheshimu michango ya hata wale tunao waona ni maadui au wasaliti wa chama,kila la kheri kwenda 2015 mapambano yanaendelea
 
Mh. Lema fanyeni maamuzi ki-inteligensia zaidi na kisayansi zaidi sio kwa hisia kama ambavyo mnataka kufanya. CCM wanaogopa CDM kwa sababu ya inteligensia yake na mipango yao inashindwa kila siku kwa sababu inteligensia yao ni hafifu kulinganisha na inteligensia ya CDM, vyama vingine vyote vya siasa vipo hafifu kwa sababu ya inteligensia zao; ila leo mnavyokuja hadharini kuongea poyoyo nyingiiiiiiiiiiiiiii kwa ishu ndogo kiasi hiki tunapatwa na shaka sana juu ya uwezo wa chama chetu cha ukombozi, CDM. Makamanda hatuangalii sura ya mtu; kama kiongozi amezingua tunamfungashia virago fasta tena fasta mchana kweupeeeeeeeeee!

CDM ni tumaini la tanzania mkome kutuletea poyoyo mtandaoni; hakuna muda wa kupoteza, sasa ni kazi tu hatutaki blahblah, shetani mwovu CCM anarusharusha miguu tu pumzi inamwishia! Msaliti tupa kule hatuna muda nae, jeshi la ukombozi ni kubwa sana na wanazidi kujiandikisha kila kukicha!

Karibu sana JF ........................ huku kwenye jukwaa la siasa kambi rasmi ya upinzani ni CCM!
 
Tatizo sio kutofautiana kifkra tu,KUNA USHIRIKIANO NA CCM ANAUFANYA ILI KUIUA CDM.

Zaidi ya kuongelewa kwenye mtandao, dai hili hslijawahi kuthibitishwa...

Najua kinachomponza Zitto ni yeye kuutaka uraisi wa Tz ambapo anaamini njia rahisi ya kufanikisha hilo ni kuwa mwenyekiti wa CDM. Kwa hili naamini Zitto anakosea, but haya makosa yanamcost mwenyewe na sio CDM...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom