Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Status
Not open for further replies.
Umeongea kweli tupu,na ni matumaini yetu uongozi wa juu wa chama utayapa uzito maoni yetu.sisi wanachama wa chadema tumechoshwa na chokochoko za huyo kinara wa usaliti na tunataka kuona akipewa mlango wa kutokea sasa.nawahakikishia wana cdm kuwa alishakuwa mwepesi huku field toka alipoanza kujitenga na chama na kuongoza kundi la wasaliti.huu ni wakati wa kuwafukuza wote wenye harufu ya usaliti na roho chafu za kuhujumu chama.nipo igoma mwanza.
 
Safari yetu ya kubadilisha utawala inaonekana kufika ukingoni na nifuraha ya kila Mtu mwenye hisia ya ukweli katika maisha na ninapotazama mbali sana ninaona jinsi ambavyo Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa ni bahati mbaya sana uwezi kuwaepuka katika harakati hizi lakini tukiwa makini tunaweza kuwathibiti
mkuu najua we ni mpiganaji wa ukweli mpaka arusha imekukubali kweli maintain status aim your coverage kwa lukuvi na wasira; nchimbi;
 
Uoga wa kutaja wasaliti ni dhambi kubwa kuliko unafiki...Tena isiishie kutaja tu jina la huyo msaliti,ushahidi nao utolewe na hatua zichukuliwe......kuwe na tofauti kati ya waimbaji wa mipasho na mnaojiita viongozi vinginevyo raia watashindwa kutofautisha....

Tafakari
 
Ni Kweli Mh.Mbunge..!

Zitto Kabwe kaponza wanasiasa wengi sana tukianza na

1.David Kafulila


Na kuwaharibia future kisiasa vijana wetu

1.Mtela Mwampamba
2.Juliana Shonza
3.Habib Mchange

Ambao ndoto zao za kuwa hata diwani zimeyeyuka
 
Tatizo tamaa ya madaraka MTU HAJALALA MAHABUSU HATA SIKU MOJA anataka uenyekiti,urais huku umri hauruhusu na hajaenda vijijini sana kukijenga chama
 
Kwa mwendo huu wa kila kiongozi kulalama ndani ya mitandao na kwenye media,CHADEMA haina maisha marefu.

Sure, mitandao ni kwa ajili ya advocacy. Hata ukiwa na ugomvi na mkeo ukiwa unazungumza on public hatuongei mpk watu wakajua kuna tofauti kwa sababu matatizo ya wanandoa humalizwa na wanandoa wenyewe.

Matatizo ndani ya chadema yatamalizwa ndani ya chadema, na sio nje ya chadema
 
Godbless J Lema,
Mimi nakukubali katika harakati za ukombozi wa taifa hili. Lakini naomba kukushauri kitu kimoja: Katika siasa kubali kutofautiana na watu fikra. Na sio kila mara unaotofautiana nao fikra basi ni maadui zako. Ni wazi kabisa kwamba Mwenyekiti wetu Mbowe angesema nawachukulia kama maadui wale wote anaotofautiana nao kifikra, CHADEMA isingekuwa hapo ilipo.

Kila shilingi ina pande mbili. Sio sahihi kumjudge mtu kwa kuangalia weakness zake peke yake. Naamini CHADEMA imefika hapo ilipo kwa juhudi kubwa za viongozi wake WOTE na wanachama wake. Na ninaposema wote nina maana ya WOTE. Sio vyema mtu mmoja au kikundi cha watu kujiona kuwa wao ni bora zaidi ya wengine. Kila mtu anayo madhaifu yake kama alivyo na mazuri yake. Hakuna mtu aliyekamilika, sio CDM, sio CCM na sio popote.

Wanasema mbwa ukishamjua jina hakusumbui Lema.... Tafakari braza...

Tatizo sio kutofautiana kifkra tu,KUNA USHIRIKIANO NA CCM ANAUFANYA ILI KUIUA CDM.
 
Last edited by a moderator:
Mie napita tu.

603985_617812231595410_1812893646_n.jpg
 
Mtu huyu wote tunamjua ni matumaini yangu Usaliti wake sasa utafika kikomo kama Chama kitaamua kuwa na busara za kutosha katika kujenga siku njema zinazokuja . Mtu huyu amefanya mambo mengi mabaya katika Chama yanayohusu usaliti na amewaponza Vijana wengi na kuangamiza ndoto zao kwa sababu ya mambo yake binafsi

Tunamjuwa, ni Dr.W.Slaa au sio? aliwasaliti na kusema eti hamjawahi kuwa katiba yenye ukomo wa muda wa uongozi. Halafu akawaita wanachama wa chadema "indigo walk"ins.

Halafu tunasikia kamweka mchumba ndio anadhibiti programu za mapato na matumizi yote ya chadema.

Si ndio huyo? sasa kinakushinda nini kumtaja tu?
 
Na watakaoibomoa CDM si wengine bali hawa ambao wamekuwa wakipima upepo tangu mwanzo. Leo nccr, kesho tlp, keshokutwa cdm...
Kila siku unatuhubiria ujasiri, unashindwa nini kumtaja huyo msaliti? Mwigamba alichukuliwa hatua kwa uzushi kwa viongozi wake. Lema is doing the same, CDM chukueni hatua before it's too late.

Busara imetangulizwa kabla hajatajwa. harufu ya kutajwa inanukia. obviously atajitaja mwenyewe kama kweli ni mzalendo. juzi kwenye gazeti alijitaja bila kutajwa.
 
Kamanda Godbless J Lema kwanza nikupongeze sana kwa maneno murua uliyoandika katika thread hii. Pia nikufahamishe kuwa haya unayoyaandika leo wanachama wenzako wa Chadema wamekuwa wakilipigia kelele kwa muda mrefu kwamba huu usaliti unaoendelea kutokea ndani ya chama ni kwasababu Mkuu wa kikosi cha usaliti chama hakijambaini na kumchukulia hatua.

Mimi nataka nikuhakikishie kwamba siku huyo mkuu wa operation usaliti akibainika na chama kikamchukulia hatua kali bila kujali ukubwa wake ama udogo wake basi siku hiyo mtakuwa mmewatendea haki wanachama, haki ambayo wameisubiria kwa muda mrefu sana.

Kamanda Lema wewe ukiwa mjumbe wa kamati kuu, matarajjio yangu ni kwamba hoja hii utaiwasilisha katika kikao rasmi chakamati kuu na kwakuwa unaonekana unao ushahidi wa kumtambua mkuu wa kikosi cha usaliti basi hatua kali zitachukuliwa haraka sana ili kukinusuru chama na huu usaliti unaotaka kushika kasi.
 
Last edited by a moderator:
Tunamjuwa, ni Dr.W.Slaa au sio? aliwasaliti na kusema eti hamjawahi kuwa katiba yenye ukomo wa uogozi. Halafu akawaita wanachama wa chadema "indigo walk"ins.

Halafu tunasikia kamweka mchumba ndio anadhibiti programu za mapato na matumizi yote ya chadema.

Si ndio huyo? sasa kinakushinda nini kumtaja tu?

Faiza,

Wengine sie tunasema tik tok tik tok towards :rip: Chadema
 
Ni kheri kuwa na wanachama 100 ambao si wanafiki wala wasaliti kuliko kuwa na wanachama 1000 wasaliti na wanafiki.
 
Godbless J Lema sioni sababu ya wewe kuendelea kulalama humu. haya mamba kamwe hayawezi kukusaidia kabisa wala kukisaidia chama.

Muda mwingine ni bora kukaa kimya, kuna mambo mengi ungefanya zaidi ya haya kuja kwenye mitandao kulahumu kuhusu msaliti.

Tunataka chadema mmoja hatutaki chadema ya makundi ya kulalama na kulahumiana.

Hivi kama una ushahidi wa wasaliti kama ule wa mwigamba kwanini usiupeleke sehemu husika?kwanini tuishi tuki lalama mkuu?

Me naamimi kukaa kimya ni busara zaidi kuliko kuongea kila wakati.

Kwakweli hizi mambo hazijengi kabisa, ukiulizwa ni nani una mlahumu katika hili pengine hutomtaja kama ulivyofanya.

Kwanini tufanye mambo yakutoa lawama kila leo.

Wewe si Lema ambaye nimekuwa nikimadmire kila leo.

Huwa na kuadmire kwa kuwa muwazi na ufichi lakini ninacho jiuliza ni lini umeanza mafumbo?

Umekuwa ukisema hakuna dhambi kama uoga lakini wewe umeonesha uoga maana unaonekana una ushahidi wa kutosha jinsi huyo mtu anavyo fanya usaliti lakini umeshindwa kumtaja sasa kwa nini unaogopa kama una kitakia mema chama?



Huu upuuzi wa kulahumiana haujengi chama,hatuutaki.
 
Last edited by a moderator:
Huyo msaliti ni nani? Vp umeshndwa kuongea hayo kwenye vikao vya chama unakuja hapa hadharani.
Mkuu, kikao kiitwe kuongea usaliti? hapa kamand anatoa elimu ya uraia... wapo tunaojifuza... ulimu anayotoa lema ni muhimu kwa kipindi hiki amabapo, waliopo madarakani wanatumia dola... Lema anapandikiza ujasiri kwa vijana...
bravo Lema
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom