Usalama wa barabarani ukiwa Kwenye Usukani... The Do’s and Don’ts

AshaDii

Platinum Member
Apr 16, 2011
16,190
18,080


Habari wana JF...


Siku zinavozidi kwena ndio ajali za barabarni zinavozidi kushamiri katika maeneo mbali mbali ya nchi…. Kumekua na ajali nyingi na mbaya za watu kupoteza maisha ama kulemaa hadi maeneo ambayo bara bara ni nzuri kabisa hadi observers mwashangaa hasa ilikuaje.

Katika historia ya inchi yetu hii changa sasa hivi idadi ya wamiliki wa magari ni kubwa than ever before… Leseni zinavotolewa na mafunzo yanayotolewa kwa wananchi wengi ni ya kienyeji mno! Na ni ukweli na uwazi usiopingika kwamba Watanzania tulio wengi ni mabingwa wa kupenda shortcuts na twapenda saana kurahisisha mambo. Idadi kubwa za lesseni za magari hutolewa hata mhusika anaekatiwa hayupo hapo walau hata kwa interview kuhakikisha kua kweli kapitia Mafunzo stahili.

Serkali imekuja na system mpya na nzuri ya njia ya kupata lesseni (toka lesseni mpya ziwe introduced) as much as kuna some unneccessary berueacracy zinahusishwa pale; ukweli unabaki kua kama kila mmoja ambae ana lesseni angepitia zile stages zooote; hata hao wenye age 50+ ambao wamewekwa kama exceptions katika baadhi ya vipengele – ingeweza kabisa ku minimise idadi ya Lesseni zisizo stahili. Badala yake imekua ukiritimba wa hali ya juu na a way and sorce of income katika baadhi ya vipengele hasa pale ambapo Traffic inatakiwa asaini kua wastahili.

Hata hivo nia na madhumuni ya hii thread ni kama a dedication to all those who have lost their lives katika road accidents….. na kutaka na kuomba michango ya my fellow members ambao kweli wana uzoefu mkubwa wa udereva… Kwamba kwa wale members ambao hua twapita pita humu hasa via mobile na while wapo on the wheel OR not on the wheel or what ever mode you are using… tuweze pata tips za vitu gani ambavo mtu (dereva hata mpita njia) aweza epuka kufanya ili kuweza zuia ajali. Ajali nyingi ambazo zingetokea zingeweza kabisa kuepukika ama kuokoa maisha endapo tu huyo mhusika angeweza pata tip husika. JF is a social network with more than 60000 members… Naamini kwa dhati kabisa kua hatutakosa tips za kutosha kuweza zingatia tuwapo barabarani.

Na naamini pia kwmba ni weengi ambao wamepitia experience za road accidents nyiiingi na kwamba waweza share those terrible/horrible na terrible experiences na sababu zilizo cause na ni dhahiri kua zingeweza kwepeka kabisa. Poleni woote ambao mshawahi pata ajali, mshawahi poteza wapendwa/ndugu na jamaa katika ajali na hata kama ushawahi guswa in one way or another katika ajali hizi za kila siku za barabarani.
Kuna wengine ni madereva kabisa lakini hata alama za barabarani hawajui za maanisha nini na wala ziko ngapi… Watu wanakufa kwa ajali ni wengi jamani inabidi tubadilike… na naamini nakujua kua Change starts from us. Tujaribu kua responsible na tuweze kumbushana. Nitashukuru kwa wale woote ambao watatupa uzoefu wao na kutoa tips…. Hata kama ni moja ama a List of them.

Tip zangu


  • Please don’t drive and use a mobile… Ni wengi saana wadharau hii tip, but ni moja ya factor ambayo inachangia saana ajali. Hio ajali sio lazima ipoteze maisha but hata ile tu kuharibu resources (in this sense gari yako) na kuanza gharama ambazo ungeweza epusha.

  • Please do not overtake kwenye corner na hata mahala popote hatari bila kupewa ruhusa na aliekutangulia. Ni hatari.

  • Please do not forget to use your seat belt.

Mategemeo yangu ni kua tips nyingi na za kitaalam zaidi zitatoka among members.... nategemea sana toka kwenu. Natanguliza SHUKRANI.


Pamoja Saana.

AshaDii.


P.S

Will really appreciate Lack of Uchakachuzi.
 
Leseni mpya sio solution, its our social responsibility to abide by the rule!! and we usually dont...
 
Dah! haya mambo ya ajali hata usinikumbushe anti...tarehe 27 mwezi wa 11 mwaka 2011nilishuhudia ajali , siwezi kusahau:
Nilkua kasehemu fulani ambapo bado wanatumia daladala za hiace, si unazijua zile za mlango wa kuslide?
Konda kaacha mlango wazi, anasimama huku anapiga debe, na hela za nauli mkononi... kichwa katoa kwa nje hivi.
Sisi tuko ndani ya kabajaji ketu (or VX) nyuma ya hiace mara mbili, mbele yetu kuna Jeep Sherokee jeupeee kama barafu, alafu ndio hiace.
barabara ya two ways la finyu kiasi.
Sasa jamaa mwenye sherokee sijui ana haraka gani, anataka ku-overtake hiace. anaongeza mwendo na kuvuka lile line
ila bahati mbaya kulikua na lorry nilakuja on the other side, liko speedy na lenyewe.
Badala ya kupunguza mwendo arudi nyuma ya hiace, alicho kifanya ni kuongeza speed
huku akibana sana upande wa hiace ili asikwarusane na lorry.
Matokeo yake, aliugonga ule mlango wa ku-slide jambo ambalo lilisababisha mlango kujifunga kwa haraka,
ukamkata Konda kichwa instantly!!!
Unadhani alisimama tena? hata hajasimama, akaendelea mbele kwa mbele...
sisi huku kwenye bajaji tulipiga kelele na kujaribu kuki avoid kile kichwa, kikawa kinaroll utasema mpira hivi.
Hiace ikasimama, walivo fungua tu mlango mwili wa konda ukaanguka mfano wa gunia, madamu yanamiminika kama bomba tu!
Sita sahau hii ajali... hata sasa hivi nakumbuka nahisi kichefu chefu...

What went wrong: Konda hakutakiwa kukaa mlango wazi na kichwa nje, sherokee lilitakiwa ku-overtake kwa wakati muafaka.
What is to be done: kuongeza awareness kuhusu posture kwenye gari, na utaratibu wa ku-overtake.
 
Pole sana ndugu. Kweli inasikitisha.
BUT napenda kufahamu overtake hiyo ilikuwaje maana naamini mlango wa Hiace ulikuwa kushoto na overtake naamini ilifanyika kwa kulipita upande wa kulia. U
Au ulimaanisha Dereva? Hata hivyo dereva mlango wake sio wa ku slide.
Please tufafanulie
 
Thanks AshaDii for this important reminder...
Apo juu, pole Mwali...it is really disgusting!
shkamoo uncle... (sorry Anti, sio kuchakachua) :A S embarassed:
Tea Cup.jpg
 
tatizo la madereva wa dsm, sijui ni haraka au sifa, anaweza kukuovatake then asimame mbele kushushz mtu.

Hili tatizo la kuovatake hata milimani au kwenye kona mahala ambapo anayekuja mbele yzko humuoni sijuilikoje. Juzi tu nilikua narudi ubungo toka maeneo ya jitegemee nikaamua nipite chang'ombe, napandisha kimwinuko cha jitegemee hamadi kuna platz olikua inaovatake lorry!!!!!!
Mbaya zaidi kushoto kwangu kuna lundo la wanafunzi. Ikabidi nisimame!!!!! Kile ni kimwinuko kidogo sana lakini kinaweza sababisha damage kwa madereva wazembe, unaovataki lorry huku mbele huoni ????

Madereva wabadilike. Haraka za kijinga barabarani ziachwe.
 
Pole sana ndugu. Kweli inasikitisha.
BUT napenda kufahamu overtake hiyo ilikuwaje maana naamini mlango wa Hiace ulikuwa kushoto na overtake naamini ilifanyika kwa kulipita upande wa kulia. U
Au ulimaanisha Dereva? Hata hivyo dereva mlango wake sio wa ku slide.
Please tufafanulie

Ila hiace milango yake hufunguka kotekote... Na ashasema ni maeneo ya ndanindani... Dah scenrio inatisha sana hiyo!
 
Pole sana ndugu. Kweli inasikitisha.
BUT napenda kufahamu overtake hiyo ilikuwaje maana naamini mlango wa Hiace ulikuwa kushoto na overtake naamini ilifanyika kwa kulipita upande wa kulia. U
Au ulimaanisha Dereva? Hata hivyo dereva mlango wake sio wa ku slide.
Please tufafanulie
Aisee uko sharp!
gari lilikua sio adapted. kwa hiyo hata likisimama abiria wanalizunguuka na kuingilia upande wa barabara.
Katika recomendation tuongeze: dive the adequate car (most adapted tot he driving rules of the country)
 
Mwali..pole sana..hiyo scenario inatisha sana...

Ulikuwa na nani kwenye gari? Au mlikuwa wangapi? Na nani alikuwa kwenye usukani?
Asante Matis...
Tulikua watatu. Mimi, rafiki yangu na kaka yake.
Alikua anaendesha rafiki yangu, mi nimekaa mbele, kaka amekaa nyuma.
 
Asante Matis...
Tulikua watatu. Mimi, rafiki yangu na kaka yake.
Alikua anaendesha rafiki yangu, mi nimekaa mbele, kaka amekaa nyuma.

You can call me Trachoo..

Pole tena.. Kila nikijaribu kuimagine mimi ndiyo kwenye hiyo gari yenu... Ningepaki/nigeshauri tupaki pembeni for about angalau robo saa... Mi huwa natetemeka kidogo,nikishuhudia ajali awful namna hiyo live!
 
Thanks AshaDii for this useful post...

Mi nauliza,hivi madereeva wa kiume si ni wengi kuliko wa kiume? Ratio,ni vigumu kupata..
Swali: kwanini % kubwa ya akina mama hawawi involved kwenye accidents? Ila akina(sisi),vice versa is true...?
 
You can call me Trachoo..

Pole tena.. Kila nikijaribu kuimagine mimi ndiyo kwenye hiyo gari yenu... Ningepaki/nigeshauri tupaki pembeni for about angalau robo saa... Mi huwa natetemeka kidogo,nikishuhudia ajali awful namna hiyo live!
Ndio tulifanya hivo. Kaka yake rafiki yangu alichukua uskani, mimi nikakaa na rafiki yangu nyuma. she was shaking and crying. tukaenda mbali na eneo lile, tukasimamisha gari kwa muda mfupi alafu tukaendelea tuliko kua tunaenda.
 
Asante sana AshaDii,
Umenikumbusha siku ileeee...Nitajitahidi kutofungua page ya JF nikiwa kwenye foleni...
 
Back
Top Bottom