Hivi wakuu hili suala la kwenda haja kubwa, halafu wakati wa kuchamba mtu anashika shika mavi ili kujiosha mnalionaje?
Ukweli ni kwamba wengi wamelishwa mavi. Huwezi kusema wote hujisafisha mikono vizuri na maji ya kutosha na sabuni au ikiwa wote hunawa na sabuni.
Na wengine hujisafisha na maji ya ndoo ya chooni au kopo la chooni linalotumiwa na wengi. Tena utakuta ni maji kidogo sekunde 2 tu mtu kashamaliza kunawa anarudi jikoni au kwenye mgahawa anaendelea kuaanda chakula au kupakulia chakula wateja wake. Hivi kweli kuna usafi unazingatiwa hapo?
Unakuta mmama au dada wa nyumbani ambaye ndiye mpishi wa familia akienda chooni anajisafisha kwa njia hiyo hivi kweli mna uhakika huwa hawawalishi kinyesi walaji?
Ifikie wakati huu utamaduni wa kuchamba kwa kushika shika kinyesi Watanzania waachane nao. Unatia kinyaa sana.