jmushi1,
..ni vigumu sana kuwa-label wamarekani ktk kundi fulani. nimeona umeongelea ulokole na kuunganisha na Jimmy Carter,na George Bush.
..ningependa pia uwazungumzie John Kennedy,Ronald Reagan,George Bush, na Bill Clinton.
..mimi nafikiri mara nyingi Wamarekani huchagua Raisi ambaye wanaamini atarekebisha matatizo ya predessor wake.
..Jimmy Carter alichaguliwa kurudisha dhima ya serikali baada ya uhuni wa Richard Nixon.
..Ronald Reagan alichaguliwa ili kurudisha hadhi ya Wamarekani ktk duru za kimataifa baada ya kudhalilishwa kule Iran.
..Bill Clinton pamoja na udhaifu wake ktk masuala ya ngono, alichaguliwa ili kurekebisha matatizo ya uchumi yaliyoanzia kwa Reagan mpaka kwa George Bush.
..kuna jamaa yangu aliniambia Bill Cosby is not the most talented Black comedian. lakini kilichomfanya afanikiwe ni kuweza kujiuza kwa white audience.
..Obama naye kama anataka kufanikiwa kuwa Raisi itabidi ajenge imani ya watu weupe kwake. alianza vizuri, lakini haya madudu ya Pastor wake ni kama speed bumps.
..Mgombea mweusi anapaswa kuwahakikishia kwamba anakuja ku-serve Wamarekani wote, na siyo weusi wenzake.
NB:
..katika Marekani ya leo kuna wananchi weupe ambao wana maisha ya shida na hayana tofauti kabisa na ya weusi.
..Weupe masikini hawawezi kumuelewa mgombea mweusi anayejiuza kama civil rights leader.
Nakubaliana na wewe ila kumbuka kwamba Obama anataka kurun kama mmarekani na sio kama kibaraka wa mmarekani mweupe!Kumbuka hotuba yake maarufu ya 2002 ambayo alisema "there's no white america,there's no black america,there's no latino's or asians america..There is the UNITED STATES OF AMERICA!"mabadiliko anayotaka kuyaleta ni watu kupewa nafasi za uongozi based on their characters and qualifications and nothing else!Anataka ashirikiane na wale wote(wazungu,weusi,latino na asians) kuelekea kwenye mabadilko ya kweli..mabadiliko ambayo wamekuwa wakiyalilia kwa muda mrefu.Kumbuka kuwa Martin Luther King aliuawa sio kwasababu alitaka black power..NO!..bali alitaka wote wazungu na weupe waishi kama familia moja na kwa upendo!Maneno kama hayo ya upendo yalisababisha akauawa.Obama anasema kuwa weupe wana resentment na weusi wana anger..na hii ni kutokana na hali halisi ya kihistoria ambayo ndiyo ime ishape jamii ya wamarekani...weupe masikini wakiwa na resntment ya kuona wengi wao bado ni masikini huku kuna weusi(licha ya kwamba ni wachache)wakionekana kupata tumafanikio.na anger ya blacks wanaobaguliwa na masikini ambao pia ni wengi!Bill Cosby yeye ni mchekeshaji tu!Amepata mafanikio kwa kuwachekesha..lakini then huwa anzungumza mambo mabaya kuhusu weusi na hivyo kupendwa na weupe!Agombee urais ndio utagundua sura halisi ya mzungu!Kwani huwaoni wakina 50 cent wakitapanya pesa mbele ya wananwake wenye vichupi kwenye video zao.. wengi wao wakiwa weusi huku jamii zao zikisota na huku wazungu wakiwatajirisha kwa kuwaweka kwenye tv,kunua cd zao! na kuwafanya wawe ndio wawakilishaji wa jamii ya weusi?Ukitaja mtu mweusi marekani tah ha..unapata sura za kina 50 na lil wayne!na nyingine za walioko jela either kwa ubakaji ma ujambazi na drugs!Obama analeta picha ya tofauti kuwa hata mtu mweusi ana uwezo wa kufanya mabo mengine muhimu kwenye jamii ikwemo pia urais!
Umegusia issue ya Reagan.Reagan kama Obama aliraise kwenye occasion..kumbuka alifanikiwa kumuondoa Jimmy Carter kabla hajamalizia kipindi chake cha pili cha urais kwasababu ya issue ya mateka wa iran..na blunder iliyopelekea mapinduzi ya kiislam huko iran!waliamua kuvunja mwiko kama walivyofanya wakati wa Kennedy!Kumchagua mkatoliki kwani walokole wote waliopita(Nixon,na Carter)Waliitumbukiza marekani kwenye majanga ambayo hata wananchi hawakuweza kutabiri!Kipindi hicho ndio wakati ambapo kwa mara ya kwanza kulikuwa na Democrats waliojiunga na Reupublicans na kujiita Reagan Democrats..wakavunja miiko ya chama kwa kuepuka udini,wanachama ambao wako mpaka sasa!Watu walichoshwa..bahati nzuri Reagan sasa alikuwa mweupe huku akitoa speech mithili ya zile za Obama!.Speech zenye kuwaamsha wamarekani na kuwapa matumaini mapya!Jamaa alivunja historia kwa kuzomba kuta nyingi dhdi ya mpinzani wake kwenye historia nzima ya marekani!Ni kam Obama sema yeye ilikuwa laini zaidi kutokana na rangi again!George H.W Bush..yeye alikuwa makamu wa rais kipindi cha Reagan so akashinda kwa urahisi kwasababu ya sifa ya Administration ya Reagan ambaye anapewa sifa ya kuvimaliza vile vita baridi dhidi ya Russia kwa amani,kuliimarisha jeshi la wamarekani na kuwaletea maendeleo makubwa ya kibiashara especially wale matajiri!Bush mkubwa naye alifanya mambo ambayo ni dhahiri yanaonyesha ni kwa kiasi gani marekani imegawanyika huku jamii hii ikiwa haifahamu sio tu historia..bali hata kile kinachoendelea kwenye maisha yao na ya wanajamii wenzao!Almaarufu kama "out of touch"Mithili ya yale mapinduzi ya ufaransa ambapo wananchi wenye njaa wanamuomba malkia walau mkate kwao na watoto wao..malkia aliwajibu kuwa ni kwanini wasile keki?Hii inaonyesha wazi kuwa mbali na njaa iliyokuwa imeigubika ufaransa kipindi hicho..bado watawala wake hawalifahamu hilo..huku wakidhani kuwa kila mtu anakula keki kama wao!Na hii ilitokea live hivi majuzi tu ambapo Bush hana habari kabisa jinsi ambavyo raia wa marekani anavyoteseka na bei ya mafuta pale alipoulizwa kuhusu bei kupanda hadi dola nne!Rais anaweza akaja akasema atashusha kodi kwa wamarekani..lakini wamarekani anaowazungumzia ni wale anaowafahamu yeye..class aliyotokea!Hili tatizo lilimkumba Bush senior aliyekuja na usemi wake maarufu wa "No more tax,read my lips"Akimaanisha kuwa sasa ni wakati wa kuwapunguzia wananchi kodi!Sasa wananchi wanashangazwa mbona hawaoni hayo mapunguzo?Baadae wanakuja kugundua mapunguzo hayo ni kwa matajiri peke yake.Wakamtupilia mbali kabla ya muhula wake wa pili..wakamleta Clinton ambaye naye alikuwa na sifa kama za Obama sema yeye ni mweupe..so ikawa rahisi kurelatem huku akizungumza lugha ya wananchi wa kawaida,na kuahidi kuwa kodi sasa ndio itapinguzwa kwa wamarekani middle class ambao ndio wengi na wenye kuihitaji!kauli ambayo ni maarufu kwa Obama this time around!Baada ya vipindi vyake viwili na matukio kadhaa ya kashfa za Monica pamoja na matatizo ya mashambulio ya kiugaidi..walokole wakaja tena na mpya kwamba ufuska na uliberal ambao umepelekwa mpaka white house ndio unaosababisha matukio haya yote mabaya marekani inayoyapata..Kwamba sasa Mungu amechukia for they just forsaken him!wakafanikiwa kuingiza kahofu kidogo huku wakisaidiwa na sysytem mbovu ya electoral coleges iliyompa Bush ushindi ambao wengi waliamini haukuwa halali!Nguvu kubwa za makampuni makubwa kuwarudisha watawala wao zilifanikishwa na jopo la majaji..na mara baada ya hapo bado marekani ikawa haitawalaki..rais hathubutu kwenda washigton kwani alikuwa akipigwa mayai viza na hali ya hatari na maandamano vikaigubika marekani..bush akaenda zake huko texas huku akifikiri aanzie wapi kwani hakuna mwananchi anayetaka kumuona!Then BOOOM!!more hofu!magaidi wameivamia marekani na sasa wananchi wanansubiri rais wao(ambaye ghafla amekuwa mpendwa)atoe tamko na ni kwanamna gani atawashughulikia magaidi hao!Yaliyotokea ni familia ya Bin Laden kukimbiziwa saudi na kunza kwa vita vya iraqi huku magaidi karibia wote(19)wakiwa wametokea saudi!sasa imagine kama wangekuwa wametokea iraqi!na huko iraqi wanaonufaika ni wenye makampuni ya uuzaji wa silaha kama kina Chenney na makampuni ya mafuta ya kina Bush...pesa zote zinazotolewa na Congress zinarudi mifukoni mwa kina Bush na washirika wake kwa namna moja ama nyingine!Kampuni zote za ulinzi,ujenzi na za mafuta na usafirishaji ni za marekani!viongozi wamewekwa na marekanihadi kazi ya udereva ni ya wamarekani..na pesa wanazolipwa zinatoka kwa wamarekani..so ni kama wanagawana bila kujali kwenye proces maisha ya raia wengi yanpotezwa bila sababu!wamarekani wamechoshwa na uhuni huo na ndio maana wako excited na Obama!Ila tatizo bado linarudi palpale..mweusi!Hivo ni wazi kwamba kusema vita viishe ni kujaribu kukata ulaji wa watu wenye nguvu kubwa duniani ambao wanaweza kukuondoa saa nusu tu kama ilivyokuwa wazi kwa saddam na wengine wengi waliopita kama kina lumumba na Nkrumah!wakina mandela na wengineo!Sitaki kumfananisha saddam na hao viongozi wengine!ila nachozungumzia hapa ni sera!sera ambayzo wamarekani wamechoshwa nazo..ambazo Obama anapromise kuzimaliza!Taitizo?once again unaweza kumalizia mwenyewe!Ndio maana Obama kwenye hotuba zake huwa anapenda sasa kusema.."WE WILL END THE TYRANNY OF OIL ONCE AND FOR ALL".."WE WILL CHANGE THE COUNTRY AND WE WILL CHANGE THE WORLD!Hizo ni baadhi tu ya kauli zake!Anajua kuwa akizibadilisha siasa za marekani..then dunia pia itabadilka!Wananchi ni kweli wamechoshwa..ila wana ubavu wa kupuuzia suala la kuwa Obama ni mweusi?Hilo tunasubiri kuona itakuwaje!
However..kuna wamarekani ambao wako aware kuwa heshima yao mbele ya dunia imeyumba huku supporters wake wengi wakipoteza uongozi wao kwa kumsupport Bush na siasa zake!Wanajua kuwa dunia imeshaanza kuwaangalia kwa jicho la kiaina..at the same time hawataki kuonekana kuwa ni bias..kwamba wanapiga kelele kuhusu demokrasia huku ya kwao ikitakiwa kufanyiwa kazi..watu wengi hawaelewi kuwa mambo kama haya yalianza zamani..kuanzia wakati ule Muhamad Ali alipogoma kwenda Vietnam kwa madai kuwa kuna vita hapo marekani kabla hajaamua kwenda kupigana vile vya nje ya marekani!Vita dhidi ya ubaguzi!Ni wazi kuwa utaona mgawanyiko mkubwa wa kijamii!Kihistoria..majeshi ya weusi(wakati huo walikuwa hawaruhusiwi kuchanganyika na yale ya weupe)ndio walifanikisha kwa kiasi kikubwa kwenye vita ya ukombozi wa ufaransa iliyoongozwa na wamarekani..lakini kwa mshangao mkubwa wa wengi..wanajeshi hao weusi walikatazwa wasishangile wakati wa shamrashamra za kuingia huko Paris kwasababu tu ni weusi na hawastahili heshma ya kibinadamu wala ya kushujaa!
Obama kumtenga mchungaji wake ni kuitenga hali halisi pamoja na historia yenye misukosuko ya marekani kwa ujumla!Mabadiliko anayotaka kuyaleta kusema ukweli yanatisha!Sio tu kwa matajiri wakubwa bali hata watu wa kawaida kama mimi tu!Kwanza kabisa ulinzi anaopatiwa huyu jamaa ni kama ule wa Bush mwenyewe ambaye ni rais!Ulinzi huu hakuuomba yeye!kwanza alikuwa akipuuzia!Lakini mwenyekiti wa kamati ya homeland security ya marekani ndiye aliyemuandikia barua mkuu wa secret services kumuomba kuwa Obama apewe ulinzi unaoendana na hali halisi ya kihistoria ya hapa marekani!Taifa ambalo kuna wakati walikuwa wakivalia rasmi kama vile wanakwenda kwenye party ama kanisani..kumbe wanakwenda kwenye "black lynching"ambapo ilikuwa ni kama sherehe wakati wa usulubishaji msalabani wa watu weusi!Weusi walikuwa wakikamatwa na kusulubishwa hadarani huku watoto,kinamama na waungwana wengine wakihudhuria kama vile ni concert flani hivi ama sherehe!Ilikuwa ni utamaduni wao!hawakuona kwamba ni unyama!Na bado kuna tamaduni nyingine wanazozikumbatia za kibaguzi na kinyama ambazo wao hawaoni kama kuna ubaya wowote!
Obama sasa anakuja na kusema kuwa yeye ndie anaye qualify kuwaleta pamoja weupe na weusi,weusi na latinos!Weusi na latinos nao hawapatani kwani mzungu keshawachonganisha kwa manufaa yake..esp ya kura na kuwaneutralize weusi na kuwasubdue kama sio second minority no more!(madai ya kuwa wazungu wanawaingiza mexicans wengi ili wawazidi weusi na kupoteza nguvu zao kisiasa na kijamii na kuwafanya wawe kundi la mwisho kwa wingi baada ya wazungu!Wazungu matajiri nao wanawaingiza wamexico isivyo halali ili kuwapa mishahara midogo..halafu wanawageukia weusi na kuwaambia kuwa hawa mexicans wamekuja kuchukua kazi zenu!chuki hapo tartiibu hadi ikakomaa!Wengi wao wamebakia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe wakigombea maeneo ya kuuza madawa(territories)na ndio maana Obama alistruggle ilipokuja kwenye kura zao!Uwezo wa kusema lolote kuhusu weupe anao kwasababu ni familia yake!Bibi yake na babu ni wazungu so as mom..na anasema amesikia vilio kutoka pande zote!Mambo mengi wameshindwa kuyatatua kwasababu ya divisions hizo!
Ubaguzi ukiwekwa pembeni..then Obama ndiye anayezungumza the right message at the right time..that also makes him the right person with the right message at the right time!Tatizo ni zile righteousness nyingine..kama vile to be with a right color,right religion and so forth..can he beat the odds?ofcourse it remains to be seen..so far he has proven so with his big coalition!however wamarekani wengi(wazungu)wanaompigia kura ni wale wa mainstream..waliosoma na wanaosoma..ambao wanajua wazi taifa lao linachukua mkondo mbaya na wanataka mabadilio yanayoendana na marekani ya sasa!marekani ya kila mtu(wahamiaji)Hta hivyo wamarekani wenye kukaa maeneo ya shamba..ambao bado pia ni wengi sana..bado ni wabaguzi wa kutisha!Ambao wameshuhudia marais weupe wenye sera za kibaguzi dhidi ya weusi..hivyo kuwapa wao wasiwasi kuwa sasa huyu mweusi naye atawawakilisha weusi hence black power..wengi wao pia wameathirika na sera za kiuchumi za republikan lakini kumpigia kura mweusi haiko kwenye damu kabisa!Kuna ambao piga ua hawawezi kumchagua mweusi!Kutokana na hilo..Simlaumu sana Clinton kwasababu anaijua historia ya nchi yake na ndio maana hataki kudrop out!Anajua jinsi wamarekani walivyokuwa vulnerable!Hataki Democrats waikose white house..wanajua kuwa wananchi wamechoshwa na republikans lakini haina maana kwamba watamchagua mweusi wa democrats!Kwamba hawa wazungu wanajua namna ya kuwatisha wananchi wao na kuwafanya wachague watu wanaowataka!Clinton na vibaraka wake kama kina sullivan wanajua kuwa maslahi yatapotea!Obama amesema atafunga milango yote ya special interest!matajiri na corruption no more in Washington!Anayo support na ulinzi wa kutosha!vitu vitakavyomsadia kuendelea kutoa ujumbe wake bila woga!Ila Clintons wanahisi Democrats wanaweza kuikosa white house kwasababu anajua issue ya kwamba ni mweusi inaweza kumlet down mwishoni!Fukuto kubwa limo ndani ya uongozi wa juu ambao wanasema sasa ni wakati wa siasa mpya kabisa!wanadai ni once in a history event..wakimaanisha kuwa kama Obama akipata urais inawezekana rais mwingine mweusi akajakupatikana baada hata ya karne moja or so!Kwamba akikosa nafasi hii kwasababu ya rangi yake then itakuwa imewarudisha nyuma sana wamarekani na once again kutia doa siasa za taifa lao na maybe Obama kuanza tena siasa za mika ya 60 za kugombea haki za binadamu!!Na hii ni kama vile wanavyotaka waonekane mbele za macho ya wanaulimwengu!Huku wakijua wazi kuwa atakayeweza kuirudisha heshima ya wamarekani mbele za mamcho ya raia wa kawaida wa ulimwengu huu ni Obama!The problem is ...race and more race!at least to the white house!