Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Nakushauri Tuko usiondoke kwani wengine tunajifunza mengi kwenye mjadala wenu wewe na Molemo. Lakini mpaka sasa sijaona kama mjadala wenu umejikita kwenye kueleza nini hasa. Najua mnabishania kama ni haki au si haki kwa Zitto kutangaza nia yake ya kugomebea Urais. lakini pia mnabishana kama tendo hilo la Zitto linahatarisha uhai wa chama au la.

Sisi wengine hili la Zitto kutangaza kuomba kugembea Urais kupitia CHADEMA ni jambo LISILOJADILIKA. Kwani tendo hilo ni la kidemokrasia. Ingekuwa taabu sana kama Zitto angesema "iwe isiwe mimi lazima niwe mgombea Urais kupitia CHADEMA mwaka 2015" hapo tungemjia juu kwa kumuuliza yeye ni nani kwamba ni lazima yeye tu awe mgombea Urais kupitia CHADEMA.

Hoja ya pili kwamba kama kauli ya Zitto inayumbisha chama au la ni ya kijinga sana. Hivi CHADEMA ni dhaifu kiasi kwamba mwanachama wake akisema "nitagombea Urais mwaka 2015" inavurugika"? Wale wanaosema kauli hii ya Zitto inavuruga chama watuambie basi inavurugaje chama!? Sipuuzii ushawishi wa Zitto ndani CHADEMA bali nichotaka kuelezwa ni kwa nini ushawishi huo uonekane kama vile ni silaha inayotumiwa na Zitto kusambaratisha chama!!?
 
Kwa mara ya kwanza najitokeza kutoa maoni yangu. Nimeanzia na kutoa ushauri wa bure kwa ndugu mtumishi wa wana Kigoma Kaskazini Zito Kabwe. Hakukuwa na sababu ya kuanza kujipigia debe ikiwa unajiamini kuwa wewe ni kiongozi bora. Kwa nini usingefanya kazi ya kukifanya chama chako kizidi kuaminika na kuaminika zaidi? Kumbuka hata kigoma utokako kama sikosei mbunge wa CHADEMA ni wewe peke yako. mimi ningedhani ungehakikisha ukanda huo wote unakua himaya ya CHADEMA. Kumbuka kuna mikoa ya kusini pwani na katikati ya nchi pia. Mtazame katibu wako mkuu kwa umri wake na jinsi anavyohangaika mpaka vijiji vya ndani kabisa. nashindwa kujua kama huwa anapata muda wa kupumzika. Inasemekana 2010 hakukuwa na mgombea aliyeonekana na sifa ya kugombea uraisi zaidi ya Dr. Uzuri ni kuwa chama ndicho kilichomuomba kugombea na siyo yeye aliyejipendekeza. Ningependa CHADEMA iwe na utaratibu huo huo. Wapo watakaosema una uchu wa Madaraka, Wapo watakaosema unamuonea gere JK anavyopasua anga kila kukicha. Ndio maana Hayati Nyerere aliuliza kuna nini IKULU? Uwezo wako utapimwa na sisi wananchi. Naomba usituache na maswali juu yako bado tunakuamini. Fanya kazi za kujenga chama. CHADEMA KWANZA, KWA MASLAHI YA WOTE, KWA UKOMBOZI WA KWELI.
 
Nakushauri Tuko usiondoke kwani wengine tunajifunza mengi kwenye mjadala wenu wewe na Molemo. Lakini mpaka sasa sijaona kama mjadala wenu umejikita kwenye kueleza nini hasa. Najua mnabishania kama ni haki au si haki kwa Zitto kutangaza nia yake ya kugomebea Urais. lakini pia mnabishana kama tendo hilo la Zitto linahatarisha uhai wa chama au la.

Sisi wengine hili la Zitto kutangaza kuomba kugembea Urais kupitia CHADEMA ni jambo LISILOJADILIKA. Kwani tendo hilo ni la kidemokrasia. Ingekuwa taabu sana kama Zitto angesema "iwe isiwe mimi lazima niwe mgombea Urais kupitia CHADEMA mwaka 2015" hapo tungemjia juu kwa kumuuliza yeye ni nani kwamba ni lazima yeye tu awe mgombea Urais kupitia CHADEMA.

Hoja ya pili kwamba kama kauli ya Zitto inayumbisha chama au la ni ya kijinga sana. Hivi CHADEMA ni dhaifu kiasi kwamba mwanachama wake akisema "nitagombea Urais mwaka 2015" inavurugika"? Wale wanaosema kauli hii ya Zitto inavuruga chama watuambie basi inavurugaje chama!? Sipuuzii ushawishi wa Zitto ndani CHADEMA bali nichotaka kuelezwa ni kwa nini ushawishi huo uonekane kama vile ni silaha inayotumiwa na Zitto kusambaratisha chama!!?

Unajua mkuu Kigarama, binafsi natambua kwamba baadhi ya kauli na misimamo za Zitto inam-cost hasa zile ambazo ziko highly politically vulnerable. Namaanisha kwamba katika baadhi ya mambo ambayo ni sensitive sana, ambayo wanasiasa legelege hawathubutu kuonyesha misimamo yao (hadi waone upepo unavyoenda), Zitto amekuwa akionyesha misimamo yake 'mapema', na katika baadhi ya hayo, ana fall kwenye disadvantagous side. Mojawapo ya issues ambazo Zitto amerisk haiba yake ni Tanesco, Kafulila kutimuliwa CDM, na yeye kuamua kugombea uenyekiti wa chama. Hata hivyo tusisahau kwamba zipo nyingine ambazo amefanya vizuri na wengi wakamsifia, mfano posho, madini n.k.
Wasiwasi wangu ni kwamba, je, wote wanaomsakama Zitto kwa misimamo yake, ni misimamo yake tu au wana ajenda zilizojificha nyuma yao? Je hawa wanaotaka kutuaminisha kwamba Zitto ni adui ya Slaa, adui ya Mbowe n.k, kweli ni hivyo au wanaona kama anawazibia nafasi baada ya zama za Mbowe/Slaa kuisha?
Binafsi ingawa namuona Zitto kama kiongozi mahiri na anayefaa, hakuna nafasi yeyote ya kisiasa atakayogombea yeye na Slaa au Mbowe, nimpe zitto kura yangu, never for now. Hata hivyo, sidhani kama Mbowe/Slaa watakuwepo milele. Naamini kuna siku nitampima Zitto dhidi ya akina Mnyika, Mrema, Wenje, Lema, Heche na wengine wengi ambao kwangu wote ni majembe. Sasa ni nani atakayepewa nafasi ipi kati ya hao 'vijana' hapo, haitategemea ni nani ambaye anaongea sana sasa, bali ni yupi anaonekana kuwa anafiti wapi kwa wakati huo. Hii ndiyo sababu mi sitishiki, wala sioni kwa nini tuparune makucha eti kwa sababu ya kitu kidogo kama 'nia' ya Zitto kugombea uraisi. Thats very light. Tena siamini kama zitto yuko bize anatangaza nia, bali tunamuona kila siku yupo bega kwa bega anajenga chama, sawa na wanavyofanya viongozi wengine wote...
 
Ushauri wa mtei ni mzuri,uamuzi wa zito nauunga mkono kwa sababu anahaki ya kufanya hivyo.
Uchaguzi wa 2010 nasikia chadema walifanya utafiti (KWA mujibu wa Munyika John radio Magic fm wiki iliyopita)kutambua ni mgombea yupi alifaa kupeperusha bendera ya chama kwenye uchaguzi mkuu na utafiti ulionyesha Dr Slaa alikuwa anakubalika na wasomi na wanachama wa chadema pia wananchi kwa ujumla.Upepo katika uchaguzi ulivuma vema kwa chadema.

Nashauri chini ya Pro Baregu tumieni utaratibu uleule kumpata mgombea urais wakati ukiwadia bt Dr slaa is the best presidential Candidate Kupitia chadema kwa sasa lkn kwa kuwa upepo unabadilika 2015 tumieni busara kumpta mgombea
Nawasilisha.
 
Unajua mkuu Kigarama, binafsi natambua kwamba baadhi ya kauli na misimamo za Zitto inam-cost hasa zile ambazo ziko highly politically vulnerable. Namaanisha kwamba katika baadhi ya mambo ambayo ni sensitive sana, ambayo wanasiasa legelege hawathubutu kuonyesha misimamo yao (hadi waone upepo unavyoenda), Zitto amekuwa akionyesha misimamo yake 'mapema', na katika baadhi ya hayo, ana fall kwenye disadvantagous side. Mojawapo ya issues ambazo Zitto amerisk haiba yake ni Tanesco, Kafulila kutimuliwa CDM, na yeye kuamua kugombea uenyekiti wa chama. Hata hivyo tusisahau kwamba zipo nyingine ambazo amefanya vizuri na wengi wakamsifia, mfano posho, madini n.k.
Wasiwasi wangu ni kwamba, je, wote wanaomsakama Zitto kwa misimamo yake, ni misimamo yake tu au wana ajenda zilizojificha nyuma yao? Je hawa wanaotaka kutuaminisha kwamba Zitto ni adui ya Slaa, adui ya Mbowe n.k, kweli ni hivyo au wanaona kama anawazibia nafasi baada ya zama za Mbowe/Slaa kuisha?
Binafsi ingawa namuona Zitto kama kiongozi mahiri na anayefaa, hakuna nafasi yeyote ya kisiasa atakayogombea yeye na Slaa au Mbowe, nimpe zitto kura yangu, never for now. Hata hivyo, sidhani kama Mbowe/Slaa watakuwepo milele. Naamini kuna siku nitampima Zitto dhidi ya akina Mnyika, Mrema, Wenje, Lema, Heche na wengine wengi ambao kwangu wote ni majembe. Sasa ni nani atakayepewa nafasi ipi kati ya hao 'vijana' hapo, haitategemea ni nani ambaye anaongea sana sasa, bali ni yupi anaonekana kuwa anafiti wapi kwa wakati huo. Hii ndiyo sababu mi sitishiki, wala sioni kwa nini tuparune makucha eti kwa sababu ya kitu kidogo kama 'nia' ya Zitto kugombea uraisi. Thats very light. Tena siamini kama zitto yuko bize anatangaza nia, bali tunamuona kila siku yupo bega kwa bega anajenga chama, sawa na wanavyofanya viongozi wengine wote...
Tuko maelezo yako yananielekeza kwamba wewe unaamini katika chama Imara kwa sasa lakini chama endelevu kwa huko tunakokwenda!! Na unaamini katika demokrasia inayojengwa kwenye misingi ya kuvumiliana ingawa tunapingana!!
 
Last edited by a moderator:
Tuko maelezo yako yananielekeza kwamba wewe unaamini katika chama Imara kwa sasa lakini chama endelevu kwa huko tunakokwenda!! Na unaamini katika demokrasia inayojengwa kwenye misingi ya kuvumiliana ingawa tunapingana!!
Kweli mkuu...
Na hadi sasa naamini hiyo ndio CDM niliko mimi. Isingekuwa CDM ya namna hiyo, kugombea nafasi ya uenyekiti, na baadae nafasi ya kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni kati ya Zitto na Mbowe, kungesababisha leo wasiwepo kwenye chama kimoja.
 
Zito hana uzoefu wowote ni tamaa tu inamsumbua au anakimbia kivuli chake baada ya kuona mambo magumu,hivi kutoka shule hadi ubunge kwa miaka 10 ndiyo uzoefu tunaotaka? hajui hata serikali inaendeshwaje hajawahi kuajiriwa zaidi ya hizo siasa,au kuzungumza kwa jazba bungeni ndiyo uzoefu?ajiangalie ajichunguze kama kweli anaweza kuwa kiongozi wetu mkuu.
 
Kweli mkuu...
Na hadi sasa naamini hiyo ndio CDM niliko mimi. Isingekuwa CDM ya namna hiyo, kugombea nafasi ya uenyekiti, na baadae nafasi ya kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni kati ya Zitto na Mbowe, kungesababisha leo wasiwepo kwenye chama kimoja.
Well said... Kama hali iko hivyo kuna kuvumiliana kwa hali ya juu namna hiyo, sasa hili ZOGO ni la nini au limesababishwa na nini hasa??
 
Au mimi ndio sielewi nini?! Hivi kuna tatizo gani mtu kutangaza nia ya kugombea nafasi fulani ya kisiasa, ikiwa mchakato wa kumpata mgombea uko wazi na utafanyika kidemokrasia? Unless mniambie kuwa wanaofanya uteuzi wa wagombea sio watu makini na hawawezi kuteua mgombea kutokana na sifa zake. Tena mimi nadhani mtu akijitangaza namna hiyo ni vizuri maana inatupa mwanya wa kumpima aliyofanya, anayofanya na atakayofanya kabla ya kuteuliwa, yanayompa stahili ya kuwa mgombea.
 
Alwayz on top title yako inaendana na hoja zako well done>>>>>>>kwa m2 yeyote ambae hajastaafu kufikiri hawez kumpinga mh.ZZK kwa nia yake ya kutaka urais wa nchi na kumsifia mzee mtei kwa makemeo yake,suala la msingi ni kuangalia yupi ni mtu makini anayeweza kuongoza nchi bila kujali anatoka familia ya nan au chama gani,hilo ndo suala la msing vinginevyo tutaishia kutukana na kulaumu kila anayeingia ikulu bila ya kujiuliza sisi tumefanya nin i kama mchango wa maendeleo ya nchi ye2
 
Last edited by a moderator:
Kama kweli una nia njema katika kauli zako, rudisha ile summary ya topic uliyopost mwanzo kabisa kabla ya kuiondoa na kuacha habari ya gazeti peke yake.
Mtei kaongea vizuri sana, kidiplomasia, na kwa hekima kubwa aliposema "Kama yeye akichukua hatua ya kupambana ili Katiba ibadilishwe kwa kuwa anataka kuwania urais, basi itaonekana ni mtu wa ajabu sana; ni mtu mbinafsi na siyo vizuri."
Kwa sababu unazojua wewe, mwanzoni ulikuwa umesema eti Mtei kasema kama Zitto atapambana kufanya marekebisho ya katiba yaondoe kipengele cha umri "atakuwa mbinafsi na mwenye uroho wa madaraka". Usidhani kwamba mzee Mtei hakujua kutumia maneno ya hivyo, bali alitumia akili kuhakikisha maoni yake hayamu'attack' Zitto. Kuna tofauti kubwa sana kati ya maneno "itaonekana kuwa" na "atakuwa' kwenye context ya diplomaisia. Mzee Mtei hakuongelea kuwa Zitto atakuwa mroho wa madaraka...

Pili, gazeti limeandika ..."Mtei alisema amekuwa akimshauri Zitto mara kwa mara kuhusu hatua yake hiyo akimtaka kuwaunganisha wana Chadema na siyo kuwagawa au kuwavuruga"... Kwa sababu unazojua wewe ukaandika eti; ...Mtei alisema amekuwa akimshauri Zitto mara kwa mara lakini kijana huyo amekuwa "mkaidi na asiyesikia"...

Narudia tena, mimi siungi mkono kauli za Zitto kutangaza nia kugombea uraisi. Hata hivyo bado namwona Zitto kuwa ni capable and potential leader wa CDM na nchi, sasa na baadae, kama ilivyo kwa Slaa na Mbowe. Kauli zake hizi ambazo hajazitoa kwa nia mbaya, zisitumiwe na maadui wake kisiasa wachache, kutuvuruga CDM kwa kutufarakanisha na viongozi wetu na kusema eti CDM kuna makundi.
Kwa heri Molemo, na sitakujibu tena.
Mkuu wangu manneo yako murwa na yanazumgumzia ukweli ambao wengine wanashindwa kuufahamu na pengine hata kuyazingatia.. Lakini pamoja na hayo yote lugha na majibu ya Zitto yameonyesha dharau. hakuhitaji kujibu wala kusema aloyasema na hivyo inatushangaza sana mtu anayetaka kugombea Urais anaweza kuropoka hivyo...

Chama cha CDM sio Mbowe, Zitto, Dr.Slaa, Lissu na sijui Mnyika hawa wote ni wanachama kwanza ambao wanatakiwa kuziheshimu sheria na katiba, kanuni za chama na kisha kama wabunge KUILINDA katiba ya nchi yetu..Haya ndio majukumu walopewa na wananchi hivyo usitake sana kutuaminisha kwamba ikiwa Mbowe, Dr.Slaa na Lissu hawakusema kitu basi watu wengine hawana haki ya kudadisi. Mbona pia hakuna kati yao alotangaza kugombea? kwa nini na yeye ZZK pia alisubiri maana naona unataka kuziweka character kuwa sawa.

Halafu swala la kukivuruga chama sio swala la viongozi bali kuwavuruga wanachama wote, makundi kati ya viongozi yapo na yataendelea kuwepo lakini pamoja na tofauti za makundi bado UMOJA wa wanachama wote hasa pale wanapoungana pamoja kuwa imara, ndivyo chama kinavyoweza kusomeka. Hizi nyufa nyufa za kutoaminiana ndizo zinaweza kuwa sababu ya kukivuruga chama maana kuwepo Mbowe au Dr.Slaa Chadema haina maana wao ndio CHAMA na wala yoyote kati yao ikiwa wananchi watakosa imani nao, chama kitabakia kuwa kama NCCR. Chama hiki kipo toka mwaka 1995 na hakikupata Umaarufu wowote kwa kuwepo viongozi hao hao isipokuwa sera zake na jitihada za pamoja ktk kumkomboa mwananchi ndizo zimewasukuma wengi kujiunga na hata kulipa kura zao. Chama pasipo kura za wananchi hakuna kitu hata kama kingeongozwa na Mandela.

Labda pengine niseme ya kwamba sisi wengine tumejiunga na CDM kwa sababu tumekiona chama hiki ndicho PEKEE chenye mwelekeo wa kuwaondoa MAFISADI ktk utawala na kurudisha mfumo bora, kuwajali wananchi wenyewe kama warithi halali wa maliasili na rasilimali zilizopo. Kama CCM ingeweza toka mwaka 2000 kupambana na wahujumu Uchumi, uwekezaji wa mikataba feki, ikaboresha maisha ya wananchi hasa WAKULIMA na WAFANYAKAZI kwa kuwajengea daraja la maisha wakatoka ktk umaskini na Ujinga kufikia nafasi ya kati middleclass yenye WAFASIRIAMALI wengi kuliko maskini basi bila shaka ingekuwa kazi kubwa sana kwa huyo Mbowe, Dr.Slaa au Zitto kutuvuta Chadema..This is the fact, naomba uipate kutoka upande wa pili..

Sipendi Unafiki na nitaendelea kusema ukweli pale napoona ZZK akijaribu sana kutuvuruga watu akili zetu sisi watu wazima na tuna mapenzi na chama sio Mtu. Na ukimsoma Mzee Mtei kazungumza kwa hekima kubwa sana. Zitto kufikia 2015 miaka atakuwa miaka 39 na katiba ya NCHI inasema wazi mgombea lazima awe na miaka 40. Sasa hapa anaitangaza nia hiyo akiwa na maana gani kuwa ana protect kiapo chake cha katiba vipi au anapingana nayo!. Na unaweza vipi kusema ni haki yake ya msingi ikiwa ni kinyume cha Katiba iliyopo? Mengine jamani hatuhitaji kuyasema ZZK mwenyewe anatakiwa kuyapima.


Ya kwamba yeye ana hakika Katiba ijayo itapunguza miaka? Na yeye kama Mbunge hivi hakuapishwa Bungeni kuilinda Katiba iliyopo hata kama kuna mapendekezo ya kuibadilisha katiba? kwa nini anapingana na katiba iliyopo sasa hivi tena kwa sababu yake mwenyewe kutaka kugombea Urais. Angeweza sana kuyafanya haya nyuma ya pazia la chama chochote kwa kushinikiza mabadiliko huku chama kikimuandaa kama itatokea hivyo. Ni Ubinfasi mkubwa sana maana hata katiba ikibadilika itaonekana imebadilishwa ili kumwezesha Zitto agombee wakati haikutakiwa kabisa watu wafikirie hivyo..

Besides, Zitto anatumia vibaya nafasi hii kwa kusema ya mwaka 2015 wakati uhai wake wa kesho hajui itakuwaje..Kulingana na imani yake haya ni makosa pia. Muumini huwezi kutangaza matakwa yako mbele ya majaaliwa, badala ya kuomba Uzima kila siku kufikia hiyo 2015 maana hajui atakuwa wapi na atakuwa nani. Zaidi ya hayo anajijengea maadui zaidi. Kesho likimpata Jambo Itaonekana CDM wamemkolimba. Na pengine sisi wanachama tulikuwa na imani naye sana lakini kujitokeza kwake tayari CCM wataanza kumtazama kama kikwazo. wataanza mapema kumshughulikia na pengine hata kumkolimba wakijua lawama zote zitakwenda Chadema. Je hajakiweka Chama ktk nafasi mbaya?.. Jamani wengine hayahitaji tuseme hovyo humu aaaaah!

Muda wote sisi wengine tumekuwa tukimshauri ZZK kwa kutazama mbali sana na ndio maana nasema siku zote ZZK bado hajakomaa kisiasa. najua fika kwamba wadanganyika ni watu wenye fitna, wanafiki na wapenda kurudishana nyuma lakini maajabu ameendelea kuonyesha udhaifu wake ktk kuwajaua watu anaotaka kuwaongoza kwa kutoweza kuliona hata hili dogo.. Mzee Mtei kazungumza vitu ambavyo ZZK alitakiwa kuvisoma na kuvielewa badala ya kutoa majibu ya kihuni. Huyo Mbowe aambaye siku zote wanagombana sidhani kama anaweza kukubalika kugombea Urais.. He is a good Political leader, ni mwanasiasa mzuri sana lakni he is not a Presidential Material. Hivyo hata yeye analijua hili isipokuwa anategemea pengine anaweza kupendekezwa.
- IKULU SII MAHALA PA KUKIMBILIA.
 
Katiba ya Tanzania kwa sasa, inamnyima Zitto sifa za kuwania urais mwaka 2015 kwa kuwa hadi kufikia mwaka huo atakuwa amefikisha miaka 38, huku Katiba ikielekeza kuwa mgombea urais anatakiwa awe na miaka isiyopungua 40.
Labda Zitto, ameshatonywa kuwa katiba mpya itamruhusu kugombea. A man has his resources:eyebrows:
 
zitto??? huyo mlafi? anayehongwa na kufunga mdomo, akiwa rais itakuwaje? yaani kama CHADEMA wanataka kusimamisha jiwe basi wemweke huyo zito. ni bora tumpe Lowassa kura kuliko huyo zito.
 
Katiba ya Tanzania kwa sasa, inamnyima Zitto sifa za kuwania urais mwaka 2015 kwa kuwa hadi kufikia mwaka huo atakuwa amefikisha miaka 38, huku Katiba ikielekeza kuwa mgombea urais anatakiwa awe na miaka isiyopungua 40.
Labda Zitto, ameshatonywa kuwa katiba mpya itamruhusu kugombea. A man has his resources:eyebrows:
Katonywa na nani? ina maana Katiba imeshatungwa tunasubiri kutangazwa tu?..haya ndio yanayoleta Utata maana anawafanya watu kuanza kuhoji hata hiyo katiba mpya yenyewe...
 
Ingekuwa Vizuri Sana Kama Zito Angesema Kuwa Endapo Slaa Akishinda Uraisi 2015 Amkumbuke Uwaziri Sio Kutangaza Kugombea Urais Hana Ubavu Huo Au Katumwa Kuivuruga Chadema
 
Baada ya kutangaza rasmi nia yake ya kugombea urais,, nashawishika kusema kwamba ana sifa zote na anatosha sana. Vijana bila kujali u-CCM au u-CHADEMA tumuunge kijana wmenzetu mkono ili atuongoze. Go Zitto.
 
Baada ya kutangaza rasmi nia yake ya kugombea urais,, nashawishika kusema kwamba ana sifa zote na anatosha sana. Vijana bila kujali u-CCM au u-CHADEMA tumuunge kijana wmenzetu mkono ili atuongoze. Go Zitto.
Hueleweki mkuu
 
Kama anatosha anakutosha wewe. Yalekea wewe Koffie ni Zitto Kabbwie mwenyewe au kuwadi wake. Siku zote tumemshauri Zitto angalau ajipatie jiko kwanza ili ajifunze kulea watoto na kutunza familia ndiposa afikiri kuongoza nchi. Nani yuko tayari kuchagua mtu ambaye hata hajijui? Tumalizie kwa kusisitiza kuwa Zitto anakutosha wewe kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom