wilbard athanass
Member
- Feb 28, 2014
- 69
- 83
soma mwanzo vizuri naonaMalaika hawana jinsia kwahiyo hawakuumbiwa program ya uzazi ktk bongo zao. Ni viumbe wa dunia hii pekee ndio waliumbiwa program ya kuzaana, na program hii ni ya mda tu baadae huondolewa. Imeandikwa kule mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, mtaishi km malaika... Maanake malaika hawazai na hawana uwezo huo, sanasana wanafanya mazingaumbwe mbele ya binadamu kwasababu tuko chini ya utawala wao hapa duniani... Sasa nini kilitokea baada seluthi (1/3 )moja ya malaika kuasi mbinguni? Mungu alimtahadharisha Adam na mkewe kipi cha kujihami nacho... Shetani na malaika zake wakamtumia Eva kwa udhaifu wake wa kibinadamu... Km Eva angekataa shetani angekuwa mbali na sayari dunia leo. Eva alikubali ndo ukawa mlango wa shetani kuwa mtawala badala ya adam, ikabidi afukuzwe bustanini waende waishi kwa shida.... Kuwakomboa mikononi mwa shetani ilihitajika afe yule yule aliekwepo kwenye uumbaji. Ndo maana shetani alipomjaribu yesu alimwambia nitakupa fahari hizi zoote unisujudu kidogo tu. Maanake alimshawishi aachane na mpango wa kuwakomboa uzao wa adam. Hilo alishindwa, ukombozi ukafanyika likabaki swala moja tu kuwa ni binadam ndo mwenye jukumu la kuamua kumkubali, kumwamini na kumfuata huyo mkombozi.