Updates za yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA

Updates za yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA

Mbowe anafanya siasa za kitoto sana, kwa akili yake ndogo hapo anafurahi kuwa umaarufu unaongezeka.

comrade msalani. ni vyema mambo kama haya mngenyamaza.maana chanzo cha yote ni chama chako. mkizidi kuongea mnazidi kikichimbia chama kaburi kwa kuzidisha asira kwa wananchi. kiukweli ccm ndio itabeba mzigo uhu 2015 sijui kama itapona.
 
Waliokuwa wanasema jana kuwa kesho tutakuwa mstari wa mbele ndo wanaomba updates wapo na vi-keyboards,ukamanda ni shida

Ukiwafuata hao jamaa utakufa masikini au kupata ulemavu wa kudumu.
 
Maranyingi tumeona polisi wakienda na mbwa kuzuia maandamano Au mikusanyiko ya vyama vya siasa. Hivi kuna umuhimu kweli wa kwenda na mbwa katika matukio ya namna hii?

Mbwa wa polisi wapo kwa ajili ya nini?
 
Mbowe anafanya siasa za kitoto sana, kwa akili yake ndogo hapo anafurahi kuwa umaarufu unaongezeka.

mkuu msalani mbowe tayari ni maarufu sana ktk nchi hii,labda useme jingine siyo issue ya umaarufu
 
Watu hawajaamua hata kutoka majumbani kuandamana - tayari mcheche kibao - CDM ni balaa!!
 
Huu udharimu na uhuni wa kutumia polisi punde utakuwa historia
 
Serikali muangalie jinsi ya kuwawezesha vijana ama sivyo hili bomu litakuja kulipuka.Fikiria hao vijana wangekuwa na shughuli za kufanya nani angewarubuni .
Serikali msikimbie tatizo haswa mama Kabaka,mama Franella. Njooni na strategy ya kutatua hili suala.
 
Hao polisi hawajui 2015 chadema itakuwa ikulu wao watakimbilia wap au wanadhani ccm itawapa amri kila siku
 
P olisi wafanya maandamano inchi nzima kufikisha ujumbe wa CHADEMA kwa wanainchi.


Kumbe polisi wananguo nzuri za sare zao huwa wameziweka tu majumbani, nimefanya mawasiliano nchi nzima nimeambiwa jeshi la polisi liko stand bay , liko barabarani likifanya doria kudhibiti maandamano ya wafuasi wa CHADEMA ambao wangeandamana leo.


Ofisi zote za CHADEMA zimezingirwa na magari ya ngarandinga ya FFU wakiwa wamavalia sare zao safi teyari kukabiliana na lolote litakalotokea. Ofisi za CHADEMA Mtwara maeneo ya chikongora karibu na soko kuu zimezingirwa, Masasi maeneo ya uwanja wa fisi kuna polisi kibao, Kasulu ofisi za CHADEMA ziko Kigoma Kibondo road karibu na nyumba ya Gorofa ya Ndituye zimezingirwa ,Tanga ofisi za CHADEMA ziko mabanda ya papa zimezingirwa. Mpwapwa ofisi za CHADEMA ziko maeneo ya stand ya zamani zimezingirwa. Dodoma maeneo yote ya barabara inayochepuka toka barabara kuu itokayo Dar kwanda maeneo ya ukumbi wa bunge kuanzia CBE wapo polisi na magari yao, mbwa na farasi ,hapapitiki wamefunga njia, kwenye ofisi za CHADEMA mkoa karibu na FOTS kuna gari za ngarandinga zipatazo 10. Kigoma maeneo yote ya Mwanga, mnarani hadi Ujiji ni polisi tupu.


Wanainchi wanajiuliza kuna nini leo? Wanajibiwa na wenzao kwamba Polisi wanazuia maandamano ya wanachama na wapenzi wa CHADEMA wanaotarajia kuandamana kupinga bunge la katiba kuendelea kufuja hela za walipa kodi bure.


Kwa mwenendo huu wa polisi wamekisaidia chama cha CHADEMA kufikisha ujumbe wa CHADEMA kwa wanainchi bila wao kujua, kwa maneno mengine Polisi ndiyo imefanya maandamano ambayo yangefanywa na CHADEMA kupinga matumizi ya ovyo ya raslimali za wanainchi yanayofanywa na bunge la katiba.
Ama kweli Polisi watu uwezo wao wa kufikiri ni mdogo, wanafanya kazi kubwa namna hii ya CHADEMA bila wao kujua.


mkuu kwa point ulizotoa ningekuw nakufahamu ningekupa japo zawadi; ila nadhani ujumbe umefika kwa walafi wa pesa za walipa kodi pale Lumumba,respect to you
 
  • Thanks
Reactions: jme
Sasa hao polisi wanawakamata kwa kosa gani?? Kumsindikiza mtu ni kosa?? Yan Tanzania?? Tumelaaniwa.
 
Jeshi la polis mkoani dar es salaam limerazimika kutumia mbwa na virungu kuzuia wafuasi wa cha cha democrasia na maendeleo CHADEMA waliokuwa wakimsindikiza kamanda MBOWE kwenda makao makuu ya polis dar.

BACK TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom