Upanuzi wa barabara Mbeya ungeanza na maeneo yanayoua wananchi

Chintu

JF-Expert Member
Feb 4, 2011
5,437
3,457
Naipongeza juhudi inayofanywa na serikali kupanua barabara kuu Mkoani Mbeya. Lakini najiuliza ni kwa nini wajenzi wameanza na maeneo yasiyo na matukio ya kupoteza maisha ya wananchi?
Binafsi labda kama kuna sababu za kiufundi nadhani ujenzi ungeanza na maeneo hatarishi ambayo kila mwaka tunapoteza uhai wa wanaMbeya
Mfano
Mlima simike ambapo juzi tu kuna lori limesababisha ajali na kuua wananchi kadhaa
mtelemko wa iwambi kuelekea Mbalizi kila mwaka kuna matukio ya wananchi kupoteza maisha hadi ilibidi RC Makala kuamua kuweka kituo cha trafic kuzuia magari yawe yanapita kwa zamu.
Kinachonishangaza jana nimeona mkandarasi kaanza na maeneo salama kabisa (kama kule Ifisi) yasiyo na matukio yeyote ya kutisha.
Naomba serikali imuelekeze mkandarasi kuanza na maeneo hatarishi na yenye matukio mabaya kwanza ndipo aendelee na maeneo yasiyokuwa na changamoto kubwa kiusalama.
Tukifanya hivyo tutawahi hata kuondoa kero za kusimamishwa kwa dakika kadhaa ili kupishana malori na magari madogo pale Mwisho wa waya.
 
Naipongeza juhudi inayofanywa na serikali kupanua barabara kuu Mkoani Mbeya. Lakini najiuliza ni kwa nini wajenzi wameanza na maeneo yasiyo na matukio ya kupoteza maisha ya wananchi?
Binafsi labda kama kuna sababu za kiufundi nadhani ujenzi ungeanza na maeneo hatarishi ambayo kila mwaka tunapoteza uhai wa wanaMbeya
Mfano
Mlima simike ambapo juzi tu kuna lori limesababisha ajali na kuua wananchi kadhaa
mtelemko wa iwambi kuelekea Mbalizi kila mwaka kuna matukio ya wananchi kupoteza maisha hadi ilibidi RC Makala kuamua kuweka kituo cha trafic kuzuia magari yawe yanapita kwa zamu.
Kinachonishangaza jana nimeona mkandarasi kaanza na maeneo salama kabisa (kama kule Ifisi) yasiyo na matukio yeyote ya kutisha.
Naomba serikali imuelekeze mkandarasi kuanza na maeneo hatarishi na yenye matukio mabaya kwanza ndipo aendelee na maeneo yasiyokuwa na changamoto kubwa kiusalama.
Tukifanya hivyo tutawahi hata kuondoa kero za kusimamishwa kwa dakika kadhaa ili kupishana malori na magari madogo pale Mwisho wa waya.
Uko sahihi boss , TanRoads na Mkandarasi ndio Walitakiwa kukaa kuyaweka sawa.
 
Mambo ya project management yana utaalamu wake, unaweza kubadili kitu kidogo tu ukajikuta bajeti ime double.
Nadhani hakuna cha kubadili kwa sababu barabara yote inatarajiwa kujengwa.
kinachoshauriwa hapa ni kuanza na maeneo hatarishi. juzi tu kuna lory limeua watu mlima simike. Hayo nadhani ndiyo maeneo waliyopaswa kuanza nayo. Huko kwingine ambako hakuna changamoto kubwa za kiusalama wafanye baadaye
 
Huko unapopataja raia wanapita tu il pale ifisi watu wanapita na makazi mengi hivyo kura nje nje
 
Naipongeza juhudi inayofanywa na serikali kupanua barabara kuu Mkoani Mbeya. Lakini najiuliza ni kwa nini wajenzi wameanza na maeneo yasiyo na matukio ya kupoteza maisha ya wananchi?
Binafsi labda kama kuna sababu za kiufundi nadhani ujenzi ungeanza na maeneo hatarishi ambayo kila mwaka tunapoteza uhai wa wanaMbeya
Mfano
Mlima simike ambapo juzi tu kuna lori limesababisha ajali na kuua wananchi kadhaa
mtelemko wa iwambi kuelekea Mbalizi kila mwaka kuna matukio ya wananchi kupoteza maisha hadi ilibidi RC Makala kuamua kuweka kituo cha trafic kuzuia magari yawe yanapita kwa zamu.
Kinachonishangaza jana nimeona mkandarasi kaanza na maeneo salama kabisa (kama kule Ifisi) yasiyo na matukio yeyote ya kutisha.
Naomba serikali imuelekeze mkandarasi kuanza na maeneo hatarishi na yenye matukio mabaya kwanza ndipo aendelee na maeneo yasiyokuwa na changamoto kubwa kiusalama.
Tukifanya hivyo tutawahi hata kuondoa kero za kusimamishwa kwa dakika kadhaa ili kupishana malori na magari madogo pale Mwisho wa waya.
Yawezekana Mlima mbalizi,Simike kushuka Mbembela ni pa kuombea kura.


Kuna hapa Meta kushukia Mabatini,pamekaa kihatari,ni vile tu hapana rekodi ya majanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom