Jasusi Mbobezi
Senior Member
- May 17, 2020
- 195
- 851
Nimesikia bwana Ndugai ameomba radhi kwa kusema Yesu ana mke, lakini hajaomba msamaha kwa kudanganya kuwa alikwenda Yerusalemu kuhesabiwa.
Hata kama alimaanisha Yusufu, bado alidanganya kuwa eti alikwenda Yerusalemu. Biblia haisemi Yusufu alikwenda Yerusalemu, Biblia inasema Yusufu alikwenda Bethlehemu, ngoja ninukuu maandiko hapa chini;
Luka 2:1-4
1 Siku zile amri ilitoka kwa Kaisari Augusto ya kwamba iandikwe orodha ya majina ya watu wote wa ulimwengu.
2Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyoandikwa hapo Kirenio alipokuwa liwali wa Shamu.
3 Watu wote wakaenda kuandikwa, kila mtu mjini kwao.
4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;
Kwahiyo alichokisema Ndugai ni uzushi wa kupuuzwa na ahojiwe na kamati ya maadili ili kukomesha vitendo vya ukurupukaji kwa viongozi wenye dhamana, pia ameliaibisha sana kanisa la Anglican.
Hata kama alimaanisha Yusufu, bado alidanganya kuwa eti alikwenda Yerusalemu. Biblia haisemi Yusufu alikwenda Yerusalemu, Biblia inasema Yusufu alikwenda Bethlehemu, ngoja ninukuu maandiko hapa chini;
Luka 2:1-4
1 Siku zile amri ilitoka kwa Kaisari Augusto ya kwamba iandikwe orodha ya majina ya watu wote wa ulimwengu.
2Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyoandikwa hapo Kirenio alipokuwa liwali wa Shamu.
3 Watu wote wakaenda kuandikwa, kila mtu mjini kwao.
4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;
Kwahiyo alichokisema Ndugai ni uzushi wa kupuuzwa na ahojiwe na kamati ya maadili ili kukomesha vitendo vya ukurupukaji kwa viongozi wenye dhamana, pia ameliaibisha sana kanisa la Anglican.