Uongo mwingine wa Spika Ndugai kuhusu Yesu kwenda Yerusalemu

Mkuu,
Betlehemu ni sehemu ya Yerusalemu.

Ni sawa na Sinza kuwa sehemu ya Dar es Salaam.
Hata kidogo! Bethlehemu leo hii iko kwenye eneo la mamlaka ya Palestina, Yerusalemu iko Israeli. Katikati kuna ukuta. Unahitaji kuonyesha pasipoti ukitaka kuvuka mpaka.
Zaidi ya hapo, zamani ilikuwa wazi ni miji miwili tofauti kabisa!
Hata kama mheshimiwa ameshawahi kufika, hajajifunza kitu. Anasema tu.
Angefungua masikio na kuwasha bongo, bila shaka walikuwa na mtu aliyewaongoza na kuwapa elimu.
 
Mheshimiwa pamoja na ile barua ya kuomba radhi Watanzania bado kafanya kosa juu ya kosa. Yusufu (na mkewe) alikwenda mji wa Daudi unaoitwa Bethlehemu na si Yerusalemu. Hili ndilo jambo ambalo watu wengi hawajaligundua. Tusome:

Luka 2 : 4-5
4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;

5 ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba.
Lilishawekwa hapa kitambo sana mkuu Uongo mwingine wa Spika Ndugai kuhusu Yesu kwenda Yerusalemu
 
Mtu ameshakiri kwa barua, kwamba ulimi uliteleza kuendelea kujadili ni upungufu wa hoja period
Hiyo barua ya kukiri mapungufu nayo pia inamapungufu hiyo ndio hoja ya mleta uzi.
Inabidi warekebishe na hayo mapungufu kwenye barua yao ya kuomba samahani.
 
Kamati ya maadili naiagiza imwite imuhoji maana keshasababisha taharuki kwenye jamii na amewachonganisha wakristo na serikali yao
 
Huyo ndiye mshauri wa askofu mkuu wa anglikana duniani

20211105_123934.jpg
 
Back
Top Bottom