Undani wa Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa

WanaJF,

Nawashukuru sana nyote kwa jinsi mlivyoipokea na kuijadili hii mada. Idadi ya watu walioipitia hoja hii na waliochangia mpaka sasa ukilinganisha na threads nyingine za leo imeonyesha wazi kwamba viongozi hawa wawili Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa ni majabali wa siasa za upinzani na Tanzania kwa ujumla.

Kwa kupitia maoni yenu nyote mpaka sasa imeonekana dhahiri wale Pro-CDM walioko hapa jamvini na waliojitambulisha rasmi wanawaunga mkono majabali hawa kuendelea kuongoza chama hiki na upinzani kwa ujumla. Nimegundua kitu kimoja cha ziada wafuasi wa Chadema wana imani kubwa na viongozi hawa wawili na wasingependa viongozi hawa kutenganishwa kwa njia yoyote walau kwa sasa.

Nimefurahishwa na comment moja hapa kwamba baada ya viongozi hawa wawili kuiingiza Chadema Ikulu 2015 basi Freeman Mbowe ataweza kuruhusiwa kukaa pembeni.Lakini sharti akiingize kwanza chama Ikulu.Nimeipenda hii!!


Wapo rafiki zangu kina Rejao,Faiza Foxy,Ritz,Kim Kardash,Barubaru na wengineo wachache ambao wanajulikana hapa jamvini kama wapinzani wakuu wa Chadema.Pamoja na kwamba hoja mlizoleta ni za mzaha zaidi dhidi ya majabali hawa wa kisiasa,lakini nimezipenda kwa sababu mbali na kujadili kwa mizaha mmeshindwa kupinga kwa hoja chochote kile nilichoeleza katika mada yangu juu.Lakini niwashukuru kwani michango na mizaha yenu inazidisha utamu wa mjadala

Wito kwa Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa

Ningependa viongozi hawa wote wawili wasome yote yaliyoandikwa kwenye hii mada.Najua Dr Wilbroad Slaa yuko huku jamvini,sina uhakika sana kama Freeman Mbowe naye yupo. Lakini naomba walau wasaidizi wao wawatonye viongozi wao kuhusu hii mada ya leo.Pia naomba viongozi hawa wawili wasome kwa makini madai yote yaliyojadiliwa na wanaJF mpaka sasa na michango itakayoendelea kutolewa kwa sababu mjadala haujafungwa.

Kama kuna mapungufu yoyote watakayoelezwa kulingana na mada hii wajirekebishe ili azma yao ya kukamata dola 2015 itimie.Wanapaswa kufahamu kitu kimoja tu-wanachama wana imani kubwa nao!!


WanaJF nafurahi kuwa member wa hili jukwaa. Thank you all.

Tuendelee na mada yetu.
 
Tatizo la watanzania wengi ni wavivu wa kufikiri badala yake wanaruhusu hisia zao kutawala na kuishia kutuhumu vitu ambavyo hawana uhakika navyo.Unakumbuka kabla ya ubinafsishaji hali ya viwanda ilikuwaje? Unakumbuka hali ya uchumi ilikuwaje?
Hao akina Slaa na mbowe wamefanya nini significant kwenye uchumi wetu? kazi tu kupiga porojo na kutoa lawama. Wawauige menzao Zitto Kabwe na Mnyika, atleast hawa wawili wana ABC za uchumi na siyo PHD za sheria za kanisa na UDJ!

Itabidi tumtafute mwalimu wa Uchumi aliyemfundisha JK (B.A in Economics) kwamba kuongezeka kwa magari ni alama ya uchumi kukua.
 
Naswali kila siku, AlhamduliLlah, kila kipindi si Ijumaa tu. Katika hukumu za sala ya Ijumaa, mwnamke anaruhusiwa kusali nyumbani na si lazima aende msikitini, akipenda anaenda si vibaya.

Interesting, kutakuwa na hukumu over so many things then.
 
kwanza sikubaliani na wewe kuwa mbowe aliacha kugombea urais ili ampishe slaa bali aliona hatapata ndo maana akakaa pembeni. na kama unakumbuka, mbowe alishajisemea mapema kuwa anaenda kugombea ubunge huko kwao hai.

Slaa mwenyewe alishasemaga siku nyingi hautaki urais ila aligombea to pale walipomhakikishia maslahi yake yote kama ya mbunge ndipo akagombea. sijapata muda wakuisoma yote ila kwa hiyo mistari michache uliyoandika nimeona ni porojo tu. kwa hiyo nimeipotezea.
 
kwanza sikubaliani na wewe kuwa mbowe aliacha kugombea urais ili ampishe slaa bali aliona hatapata ndo maana akakaa pembeni. na kama unakumbuka, mbowe alishajisemea mapema kuwa anaenda kugombea ubunge huko kwao hai. slaa mwenyewe alishasemaga siku nyingi hautaki urais ila aligombea to pale walipomhakikishia maslahi yake yote kama ya mbunge ndipo akagombea. sijapata muda wakuisoma yote ila kwa hiyo mistari michache uliyoandika nimeona ni porojo tu. kwa hiyo nimeipotezea.

kama alivyosema mtoa mada hata watu kama nyie mnafaa kwa michamgo yenu ya mzaha kwa sababu mnanogesha mjadala.
 
Wewe unasumbuliwa na na usemi wa Bendera hufuata upepo na wala huna data zozote. Ni wasomi wangapi wanaunga mkono CHADEMA? Unajua undani wa CHADEMA mpaka useme viongozi wake hawana migogoro? Slaa ni BMOWE ni kama X na Y kwa watu wa hesabu wanajua , mlinganyi kama Y =2x, Y inatemegea sana X.

Wale jama wanajuana na wanajua wanavyoitafuna CHADEMA. SLAA anaishi kwa fedha za CHADEMA, Mbowe anaidai Chadema madeni kibao na ni kama Mzabuni wa CHADEMA, sasa atawezaje kumkoromea Slaa ambaye ni mtendaji wa Chama?

Hebu jikumbushe episodi ya ZITTO na Mbowe katika kugombea ukuu wa Chama hicho. Unajua chanzo cha kifo cha Chacha Wangwe?. Mimi usiniambie kabisa kuhusu hao Mabwanyeye.

Ni kweli kwamba wamefanikiwa kufanya harakati mbalimbali kama Migomo vyuoni, migomo ya wafanyakazi n.k. Hivi siku wakifanikiwa kushika hatamu watajidai kwamba walikuwa wapiganaji au wachochezi? Uliza fukuto la upendeleo wa uongozi kwa wanawake katika Chama hicho.

Unajua chizi anaweza kujifanya anajua sana mbele ya watu wenye akili zao akadhani yeye ndo basi kumbe wanamsanifu tu. Hakuna wasomi wanaokiunga mkono Chadema bali wanakiona kama kikundi fulani cha wasanii, si unajua wasanii wanavyoweza kushangiliwa kwenye majukwaa lakini siku ya siku JINA WASANII linatawafanya waendelee kuonekana wasanii tu.
 
Umesahau kuorodhesha fanikio moja ambalo hawa wawili wanalo nalo ni mafundi wa kuiba viburudisho vya watu
 
chama kinaenda kuchukua dola, kina mnyika bado wana nafasi kubwa tu ya kukiongoza hiki chama, kwa sasa tuachieni viongozi hawa wawili -- pia kuna wengine umependekeza hapo bado hawaaminiki na sisi wananchi wanyonge.

Hawaaminiki sio wa kaskazini au? Na wamefikaje waliko ina maana waliowateua na kuwapitisha na kuwachagua nao hawaaminiki,mtu anakuwa kaimu katibu mkuu,mwenyekiti wa kamati, waziri kivuli bado haaminiki tu, hapo ndo mnaposhangaza watu
 
Ndugu siasa sio kama mchezo wa kiduku ukichuchumaa watu wanashangilia.

Kwa hiyo msipakane mafuta kwa mgongo wa chupa, sifa mnazowamwagia hawa jamaa ni sifa za kienyeji zaidi.

Mwisho wa siku mtasema Mbowe na DK Slaa, wanamzidi Obama, kwa siasa.
Kwani ikiwa hivyo ubaya uko wapi? Kwani Obama hawezi kuzidiwa sifa za uongozi?
 
SLAA na MBOWE hawawezi kugombana, wao ndo wanaitafuna CHADEMA wengine wapo ili kuhalalisha hao wawili kuendeleza ukora wao.

SLAA analipwa fedha nyingi sana asizozitolea jasho ukilinganisha na wanachama na viongozi wengine. Mbowe ni kama mzabuni wa CDM na anakidai chama hicho fedha nyingi sana, hawezi kumkoromea SLAA ambaye ndiye anayeidhinisha malipo hayo.

Hivi Mbowe alimwachia SLAA agombee? Mbona wakati wa kampeni SLAA alisema yalikuwa ni maamuzi magumu kukubali kugombea urais, maana yake ni kwamba alishinikizwa na siyo kuutaka kwa nguvu sasa iweje useme Mbowe anastahili credit kwa kumwachia?

Yaani wewe unaandika ama ambacho hujui au umefundishwa kuandika hivyo na kwa sababu huwezi kuchanganua mambo unaamua kudhalilika kwa vile sasa unaonekana wewe ni Kihiyo. Kuhusu migogoro: Unajua chanzo cha kifo cha Chacha Wangwe? Unakumbuka sakata la ZITTO na Mbowe kugombea uenyekiti wa Chama hicho kama siyo Mtei si pangechimbika? Unajua chanzo cha Charles Mwera kuhamia CUF?

Kwamba Chadema ni chama tulivu, hivi wao ni akina nani mpaka watoe tamko la vifo vilivyotokana na mgomo wa Madaktari? Hivi migomo wanayoisababisha vyuoni huioni? utulivu uko wapi?
 
Watanzania tuna matatizo sugu. Badala ya kufanya kazi za kujenga nchi tumekalia kujadili watu. Subirini kampeni zikianza mtafanya kazi hiyo tena kwa mapana na marefu. Jamani mpaka lini ujinga huu?
 
Kwanza napenda kukupongeza kwa uchambuzi huu ambao ni yakinifu halafu una mafundisho mengi sana.

1. Kwanza CDM ni chama chenye vision

2. CDM ina falsafa inayoeleweka, sio unafiki

3. CDM ina kanuni zinazotekelezeka, yaani kupitia katiba na miongozo yake

4. CDM katika mzingira haya yanadumisha nidhamu ya hali ya juu ndani ya chama kwa kuzingatia demokrasia

5. Inafanya kila kiongo kujua wajibu na nafasi yake ndani ya CDM

6. Inaondoa dhana ya chama mtu, na hivyo kila kiongozi anajua kuwa uongozi ni dhamana

7. CDM inahaha kudumisha nguvu ya umma kwa kila mbinu, chama cha wanachama kwa niaba ya umma.

Yapo mengi mengine yanayofanya CDM iwe na mshikamano wa hali ya juu.

Huu uzi umenikonga roho.
Hongera Dk Silah na Mk Mbowe.
 
Nyie ndio mlioviringishwa katika kiini (yoke) ya chama cha magamba. Mtasema, mtatukana, bado Mbowe na Slaa ni viongozi halisi watakaoikomboa nchi hii. Sote tuko nyuma yao. Kama ni suala la ufuska kuna anayewazidi wana-magamba ccm? Akili finyu huwaza na kuongea kifinyu. 2015 itawaumbua
 
Back
Top Bottom