Unaolewa na hustler? Dishi limeyumba nini?

Unaolewa na hustler? Dishi limeyumba nini?

Na uniandae kuharibikiwa mwili wako mana kila atakachoongea utakubal cz ana hela

Weee wangapi wamekukubalia unachosema ilihali huna hela .....
katika mahusiano kukubaliwa vitu unavyotaka haihusiani na hela unaweza usiwe na pesa na bado ukakubaliwa.
Choice is yours .... Being a surviver or to live a life everyone wish tooo
 
Kuna stages, anajikuna anapofika, hata hao matajiri walianzia chini wakapanda juu. Leo anampeleka bar kesho atampeleka vacation Dubai( Kaboom shenzi wewe!)
Na wa hivyo mnaetengenezana hata likiharibika mahali basi kuna ile respect mnakuwa nayo to each other maana mnajua mlipotokea. Ukiikuta ready made pakiharibika ndio fimbo ya kukuchapia.

Ukimpata huyo mwenye nazo ni heri lakini pia ukimpata asie nazo lakini ana potential usimuache, mpe a shoulder to lean on ili mfikie pale unapopataka.

Shooo tatzo wakaka wa siku hiz hamnazo unaweza kumvumilia wee hiyo shoulder to learn lakin still ukaishia kujuta tuuu ....
Bora awe nazo tuuu itapunipunguzia ya kumlaani
 
...magenge mengine mabaaaya/watu wanapokusanyika/ ...
..wengine huwadanganya;
.wenzaaaoo!!
 
Haya ni mawazo ya waseja, waliopo nje ya ndoa, mara nyingi wana tabia za kujenga taswira moja matata sana juu ya ndoa na familia kwa ujumla.

Ingia ngomani ucheze ndio utajua ndoa ni kitu gani. Imaginations zinawaponza wengi.
 
Nashukur kwa kuzaliwa mwanaume wa shoka,,,




Kuna mwenzako mwenye akil kam zako APA ananisumbua sumbua sema kosa alofany ni kunikubaria BT ..............

Ebu ngoja niweke kituo kwanza ntandelea nikipt hela ,,
 
Yaan watu km nyie ndio kuoa kwa mikataba , mahakama inapitisha kbsa huyu hajawai chuma pesa jamvi moja na ww .... so ukisepa upati ata ndala.
 
Sexless, maisha hayawezi kuwa sawa maana hatuko kwenye ujamaa, uchumi ni wa ubepari huu, kuna wenye nacho na wasio nacho. Hivyo basi kila binadamu kwa ubinadamu wake ana haki ya kupenda na kupendwa regardless hali yake ya kiuchumi au vinginevyo.

Ingekuwa ni just simple like that dunia ingekuwa na akina Bil gates tu!! Cha msingi ni kuwa na mtu atakayeongeza kitu ktk maisha yako. Material things zinatafutwa. Kuna aina fulani ya wanaume ambao yaani wako sharp by nature na hawahitaji msaada wamwanamke kufika mahali fulani, ila kuna wale wanaohitaji a little push ili waweze kurealize the potentials they have na kuzifanyia kazi.

Ila sasa kama ndio mmekutana wote mnaohitaji kusukumwa ndio mtabakia hapo hapo maana hakuna wa kumsaidia mwenzie. Tuliumbwa jinsia mbili kwa sababu maalumu(sio kuunganisha vikojoleo tu) tunategemeana in one way or another. Hivyo basi cha msingi hapa ni kufundishana kutokuwa comfortable ktk umasikini as hakuna anayefurahia umasikini hata kidogo, we have to push hard,very hard ili tujikwamue na angalau tukienda outing akili ziko relaxed.
(hiki cha leo kwakweli ni cha arusha sio mimi. )
Kweli hichi leo ni cha CHUGGA sijaamini kabisa kama ndio wewe umeandika hapa hahah
 
Mwanamke kama huyu alinipiga chini enzi hizo natafuta ajira, akaolewa na mwenye ela, mwenye ela akamuona wa level yake kampiga chini, sasa hv anaganga njaa hadi namba yangu mpya aliipata
 
Mtu mwenyewe wewe ni "sexless" kama ID yako inavyoonesha!sidhani kama umekamilika!
 
Kila mtu na jinsi anavyoamua kuishi.



Ila inabidi uwe tayari kwa manyanyaso maana mtu aliyezitafuta mwnyw halaf ww uingie hapo kati uanze kuzitumia tu
 
Ewe dada amka shoga yangu. Unaanzaje kuolewa na mlalahoi mwenzako? Tafuta mtu mwenye kukupa raha ya maisha; -mitoko ya nguvu, nyumba safi, usafiri poa, n.k. Siyo unaolewa na mjinga mjinga tu ana vyeti vya elimu ya juu lkn maisha ya chini. Unaambulia kuandikiwa meseji zenye maneno magumu ya kingereza tuuu. Au unaolewa na mtu mwenye kifua cha mazoezi lkn hana kitu mfukoni. Huyu ataendeleza mazoezi yake kwenye mwili wako tuuu.

Wenzako wakiolewa wanaenjoy eti wewe unajifariji kwamba hayo ndiyo mapenzi ya kweli. Mmh!! Kweli?? Unajisikiaje unapo olewa na hustler, unachakaa na kuzeeka kabla ya wakati kwasabb ya ugumu wa maisha? Mara unakutana na classmate, choir-mate, au hata mpangaji mwenzio unakuta anazidi kuwa kijana wewe umepinda mgongo na miguu na unanuka uvundo kisa unataabika na mlalahoi anayekutesa na maisha magumu.

Eti unadanganywa tuanze maisha wote mpenzi wangu. Hii!!!! Mkiyaanza maisha wakati mna nanihino mtayakamilisha lini wakati mnaongeza shida kwa kuzaa watoto? Nenda kwa mtu mwenye maisha mazuri shosti. Acha uzwazwa.
-Umeolewa unapandishwa bodaboda ya kukodi?
-Umeolewa unaishi kwa baba mwenye nyumba?
-Umeolewa halafu mumeo ndo kwanza anatafuta kazi? Hana A wala B. Pole yako

Hivi unapokuwa unamkubalia mlalahoi wa dizaini hii unakuwa unawaza nn? Au umevurugwa?

Wanaume maskini pishana nao round about.

HUHITAJI KUPENDWA, unapendwa na Wazazi wako.
Ni wazo pia.
 
Ewe dada amka shoga yangu. Unaanzaje kuolewa na mlalahoi mwenzako? Tafuta mtu mwenye kukupa raha ya maisha; -mitoko ya nguvu, nyumba safi, usafiri poa, n.k. Siyo unaolewa na mjinga mjinga tu ana vyeti vya elimu ya juu lkn maisha ya chini. Unaambulia kuandikiwa meseji zenye maneno magumu ya kingereza tuuu. Au unaolewa na mtu mwenye kifua cha mazoezi lkn hana kitu mfukoni. Huyu ataendeleza mazoezi yake kwenye mwili wako tuuu.

Wenzako wakiolewa wanaenjoy eti wewe unajifariji kwamba hayo ndiyo mapenzi ya kweli. Mmh!! Kweli?? Unajisikiaje unapo olewa na hustler, unachakaa na kuzeeka kabla ya wakati kwasabb ya ugumu wa maisha? Mara unakutana na classmate, choir-mate, au hata mpangaji mwenzio unakuta anazidi kuwa kijana wewe umepinda mgongo na miguu na unanuka uvundo kisa unataabika na mlalahoi anayekutesa na maisha magumu.

Eti unadanganywa tuanze maisha wote mpenzi wangu. Hii!!!! Mkiyaanza maisha wakati mna nanihino mtayakamilisha lini wakati mnaongeza shida kwa kuzaa watoto? Nenda kwa mtu mwenye maisha mazuri shosti. Acha uzwazwa.
-Umeolewa unapandishwa bodaboda ya kukodi?
-Umeolewa unaishi kwa baba mwenye nyumba?
-Umeolewa halafu mumeo ndo kwanza anatafuta kazi? Hana A wala B. Pole yako

Hivi unapokuwa unamkubalia mlalahoi wa dizaini hii unakuwa unawaza nn? Au umevurugwa?

Wanaume maskini pishana nao round about.

HUHITAJI KUPENDWA, unapendwa na Wazazi wako.
Afu si juzi tu mlikuwa mnasema Msheni Town habari ya mjini....
nawengine wakanukuliwa " NIACHENI NA MISHENI TOWN WANGU"........
 
Shooo tatzo wakaka wa siku hiz hamnazo unaweza kumvumilia wee hiyo shoulder to learn lakin still ukaishia kujuta tuuu ....
Bora awe nazo tuuu itapunipunguzia ya kumlaani
Hahahaaa! Eti itakupunguzia ya kumlaani!!
Ukisema hivyo na wao wanasema wanawake wa siku hizi hamnazo....

Umewahi kula chakula kikakudhuru? Let say ukapatwa na alergy au ukahar..sha? Je uliacha kula? Jibu lazima ni NO!
Kwahiyo basi ukimthamini mtu then asikuthamini we muache aende haikuwa riziki hiyo, ila asiondoke na self worth yako. Endelea kuwa wewe na utampata anayestahili hiyo thamani yako.

Pesa mwanaharamu ukiipata ukaruhusu ikutawale lazima ikupeleke pabaya tu, hiyo ndio huwapata wengi na kuishia kujuta na kutamani hata wangebakia ktk umasikini na waume zao ili angalau wawe na amani. Chagua kwa umakini tu, mwenye utu hata akikengeuka kujirudi ni rahisi.
 
Back
Top Bottom