Unamiliki nini katika Umri huu?

Unamiliki nini katika Umri huu?

Nina nyumba 70,mashamba heka 50000,Ng'ombe 60000,watoto 32 wajukuu 148,vitukuu 88,mbwa 50,paka 126,malori 600,kuku 200000,swimming pool juu ya mlima kilimanjaro na mto rwaha penye mamba.Tv ninatumia projector.Kumbuka nina miaka 24.
 
Nina Miaka 45.
Nina mke mmoja na watoto watatu. Nina kighorofa floo mbili hapa hapa Mapinga.
Nina Biashara zifuatazo
1. Nina duka la vipodozi hili analiendesha mke wang
2. Nina saloon ya kiume hii ni kwa matumiz madogo ya home
3. Nina kigari kidogo cha kuzugia Passo
4. Nina mashamba 50hekari
5. Mwakani naongeza mke wa pili
I wish namba 5 mkeo angeiona halafu nikasikilizia majibu yake
 
Mimi Nina umri Wa miaka 40.... Nina chumba kimoja cha kwngu mwenyewe,,RADIO YA PHILLIPS... na Maua ya plastics,,NGOMA NA STULI ZAKE,,pamoja na kabati LA mbao ,,,na NDOO ZA PLASTICS kwa ajili ya kuwekea maji
Maua ya aiseee nimekumbuka mbalii
 
Nina 30, namiliki nyumba mbili moja ipo kibaha kwa mathias, nyingne ipo morogoro nane nane, nina gari nne (ranger nyeusi, harrier, noah , na spacio), sina mke, sina mtoto, sasa hvi najenga ghorofa moja kimara, nina mashamba ekari 22, nina biashara yangu kubwa tu ambayo inasogeza siku, ni machine za kusaga za kukoboa, nina viwanja viwili. Katika elimu nina degree moja, na sasa hv ninatarajia kusoma masters kwaajili ya sifa tu, si unajua sisi wahaya. Ni hayo tu.
Hahahahaha hahahahahahaah
 
Huu uzi ni katika nyuzi bora sana za funga mwaka japo wengi humu mnajibu mpendavyo hasa kejeli na utani utani tu..........
Mleta mada anakukumbusha ujitathimi iwapo kwa umri wako wa miaka 40 tuseme tangu umeanza kutafuta maisha ni kama umetafuta kwa miaka 20 au 10 na unamiliki pikipiki tu. Je mali uliyonayo inalingana na umri wako? Inamaana kama mpaka sasa unamiliki gari yenye thamani ya milioni tano 5ml. Na sasa una miaka 15 tangu uanze kutafuta ukigawanya hiyo hela kwa miaka 15 utapata jibu kuwa ni kiasi gani unaingiza kwa siku na je ndio hivyo unastahili? Nadhani uzi huu unalengo jema sana wa kukushtua ujijue bado hujachelewa
 
Nina 30, namiliki nyumba mbili moja ipo kibaha kwa mathias, nyingne ipo morogoro nane nane, nina gari nne (ranger nyeusi, harrier, noah , na spacio), sina mke, sina mtoto, sasa hvi najenga ghorofa moja kimara, nina mashamba ekari 22, nina biashara yangu kubwa tu ambayo inasogeza siku, ni machine za kusaga za kukoboa, nina viwanja viwili. Katika elimu nina degree moja, na sasa hv ninatarajia kusoma masters kwaajili ya sifa tu, si unajua sisi wahaya. Ni hayo tu.

Subiri wanaotafuta mume wajee
 
26 yrs old Nina 1.2 M kwa akauniti naskilizia upepo niiongezee nifanye bussnes fulani... Nina apple iphone 6s , tecno cammon CX .. 1 laptop.. Hizo ndyo ofisi zangu
 
What's the difference between me and you? 5 bank accounts, 3 ounces and 2 vehicles.
 
JF huwa patamu sana,kila mtu huwa ana pesa,viwanja, nyumba ,mke mzuri na elimu yake nzuri tu na kajiajiri ....Anyways mimi namiliki simu Tecno tu
Hii tunaita infiriority complex , yaan unajisikia myonge bila sababu.

JF , ni daraja ! Yaan mapaka tunakutana tunachangia hapa jua kuna sehemu tumevuka , kama humiliki computer, basi una smartphone , au una access na computer ,
Asilimia kubwa ya wadau wa jamii forum , wana ukwasi wa kiasi fulani, , swala la kuzidiwa ukwasi watu wanapojiachia lisikuumize kichwa sana , japo kuna wengine watakua wanaongopa ,

Elimu pia lazima iwepo kwa wadau wengi humu, nayo isikuumize kichwa , ndo maana hata wewe umeweza kuchangia

Una sema unamiliki" Tecno tu" amini nakwambia kauli hiyo ukiisema kwa watu fukani nao wataona unawatambia
Mantiki ni kuwa watu hatufanani na hilo lisikuumize kichwa .
 
Nina support asilimia zote mchango na hili tukijakulitambua watanzania tutakuwa tumechelewa sana ila huo ndo ukweli japo watu hawataki kuamini wamekalia hakuna ajira.
Wanasema kupata ni majaliwa ya Mola; kwamba MUNGU anakupa uwezo wa kuona fursa kuliko wenzako hata kama mpo level moja ya elimu mwenzio anafanikiwa wewe hakuna kabisa. Hili nakubaliana nalo; unakuta mtu ananusa 50 lakini kikubwa alichonacho ni mke na watoto 3 wanaosoma kayumba ; vikolokolo vya ndani vilivyomo kwenye nyumba ya kupanga ya vyumba 2 na sebure pia kiwanja kule kongowe hakina hata msingi.

Tusichekane; ila ni kweli unapokwenda uzeeni hata dalili za kulala kwako kajumba ka walau 120m hivi ka kisasa inakuwa ndoto - hapo ni tatizo - utawaacha watoto kwenye shida; pamoja na elimu bora unayowapa ni lazima uwaachie pa kuanzia ulipoishia wewe; miaka ijayo itakuwa 10 times ya ugumu wa maisha wa sasa. Kumwacha mtoto wako aanzie moja hutakuwa umemtendea haki.

Maisha ni kupeana vijiti; yaani mtoto anaanzia ulipoishia wewe; huu mfumo ni mzuri sana ndiyo maana wenzetu waarabu na wahindi wanafaidika sana na mfumo huu; unakuta mtu ana 45 ni billionea; unajiuliza kamaliza shule lini? Lini kaanza kupanga; lini kaanza kujenga; lini kaoa; lini kaamza kuwekeza miradi hadi at that age awe billionea. Vijiti.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom