Unamiliki nini katika Umri huu?

Unamiliki nini katika Umri huu?

Nina miaka 88,nina miliki nyumba moja ya matope na nyasi,kuku kumi wa kienyeji,shamba la heka sita na na sikumbuki nina watoto na wajukuu wangapi.
 
Miaka 25-40 unakaa kwenu huta hata godoro halaf unajichetua kuwa unataka mahusiano na mtu chefuuuuuuuuu kwa bbc haina dili, mambo yote abroad mambo ya usd shilling peleka gengeni huko
Mbona ka halihusiani na hili au nimesoma vibaya, hii inatakiwa iwe uzi unaojitegemea
 
Nina Miaka 45.
Nina mke mmoja na watoto watatu. Nina kighorofa floo mbili hapa hapa Mapinga.
Nina Biashara zifuatazo
1. Nina duka la vipodozi hili analiendesha mke wang
2. Nina saloon ya kiume hii ni kwa matumiz madogo ya home
3. Nina kigari kidogo cha kuzugia Passo
4. Nina mashamba 50hekari
5. Mwakani naongeza mke wa pili
Haaaa mke tena uongeze shsurina na bi mkubwa kwanza
 
Binafsi umri miaka 29 sina nyumba yakwangu ila nimemjengea mama kijijini nyumba ya milion25 nina wadogo zangu wawili mmoja miaka 23 nimemnunulia machine tatu za kuchomelea machine ya kupulizia rangi na vifaa vyote vinavyoitajika kwenye kazi yake,mdogo wangu wa pili ana miaka 26 Yeye janja njanja nyingi nimemnunulia kamchomoko kamoja anapiga shantingi mjini mama nimemfungulia kiduka ja rejareja kijijini cha milioni nne nimefanya hvyo ili nikianza familia yangu dipendants wangu wawe wachache sasa hv najenga nyumba mjini na mwakani mungu akipenda nafungua kiduka changu cha kunisaidia, sijaajiliwa napiga mishe town japo nina kashaada kangu kafedha mipango na uwekezaji.
Ubarikiwe
 
JF huwa patamu sana,kila mtu huwa ana pesa,viwanja, nyumba ,mke mzuri na elimu yake nzuri tu na kajiajiri ....Anyways mimi namiliki simu Tecno tu
 
Kumbe Jeiefu wengi ni bongo lala...yaani mtu anamiliki liabilities kibao eti naye anakuja kujitapa humu?
Wanao miliki assets ni wachache sana wallahi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom