The Bold,
Hizi ni hisia zako kama ulivyokiri kule juu!
Sijaelewa kwanini uandike hisia zako hapa? Kwa lengo gani?
Unawapaje watu "somo" lililojikita katika "hisia zako" kwa maslahi ya nani? Maana taasisi hiyo nyeti yenye weledi ingeona kuna hitaji la kutoa "somo" kama hilo bila shaka wangelifanya wao siku nyingi kabla hata hujazaliwa kwa namna bora ya kuwafaa kama taasisi. Lakini bila shaka hawajaona umuhimu huo wala faida ya kutoa somo hilo,Kwanini jukumu hilo unajipa wewe?
Je,hujui kuwa kutangaza kwa umma hisia zako juu ya chombo cha dola ambacho hata sheria yenyewe ya kuwepo kwake inatambua usiri ni kosa?
Unataka kuwaambia umma hisia zako juu ya namna ya ku-recruit ili uifunze nini? kwa minajiri gani? kwa maslahi ya nani? ya taasisi au ya umma?
Wapi umeambiwa kuwa zoezi hilo kuna haja la kuwapa watu "somo" kama ulilokuja nalo hapa juu?
Je,vipi kama somo la hisia zako katika hadhara hii,sio sahihi na zimepelekea "myths" kwa jamii na somo lako likawaletea shida taasisi kwa sababu ya kufundisha vitu visivyo vya kweli. upo tayari kuwajibika?
Je,upo tayari kubeba dhamana ya hisia zako?
Hahahah!! Ok, here we go...
Unauliza nimeandika kwa maslahi ya nani??
Jibu: kwa maslahi ya vijana wote wenye matamanio ya kuingia katika huu utumishi... Matamanio yao ya kuitumikia nchi yao ni matamanio memo na yanapaswa kuchochewa...
Umeuliza kwa nini nimeandika hisia zangu??
Jibu: Nafahamu kuhusu nilichokiandika hapa zaidi ya maneno haya unayoyaona nimeandika hapa... Ila kwa kuzingatia sheria za nchi na tamaduni za usiri wa idara hiyo siwezi kuandika kila kitu...
Hakuna ubaya wa kuandika utashi wako (unaweza kuita hisia ukipenda)
Unasema ni kosa hiki nilichoandika??
Jibu: sidhani kama unaijua hata sheria ya kuanzishwa kwa idara ya usalama wa Taifa... Nenda kaisoma ndipi utajua nini ni siri na nini si siri... Kipi kinapswa kuzungumzwa na kipi hakipaswi kuzungumzwa...
Unasema nina lengo gani??
Jibu: unarudia swali lile lile kila baada ya aya moja. Nimekujibu hapo juu...
Unauliza wapi nimeambiwa kuna haja ya kuwapa watu somo.
Jibu: sidhani kama unatambua haki na wajibu wa mwananchi wa Tanzania kwa mujibu wa katiba. Nenda kasome.
Niko tayari kuwajibika kama itajenga "myth" kwenye jamii?
Jibu: mimi ni muwajibikaji tangu siku ya kwanza natoka kwenye tumbo la mama yangu.
Na kama andiko hili lingekuwa na shida yeyote... Wahusika wenyewe wangenitaarifu mpaka muda huu... They know me... Na si Mara moja au mbili wameniambia nisiandike kuhusu kitu Fulani... So tutayamaliza wenyewe...
Mwisho..
Najua watu wa dizaini yako, najua unachojaribu ku-insinuate... Najua unataka watu wakuoneje, najua unataka watu wakuhisi wewe ni nani...
You are not.. Stop pretending.... Its pathetic!!
If TISS has a problem with me they have my number... Tutamaliza kiutu uzima... Wataniambia niondoe Uzi na nitaondoa... sio hizi ngonjera unazoleta hapa...
Siku njema..