Umwinyi na Usultani wa CCM ndio chanzo cha Balozi Ali Karume kubwatuka ukweli mchungu kawa Rais Mwinyi

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Jul 21, 2021
1,126
4,169
Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi ya Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, Khamis Mbeto amesema tayari chama hicho kupitia tawi la CCM Mwera kimemuita mwanachama wake, Balozi Ali Karume kwa mahojiano kuhusiana na kauli zake dhidi ya baadhi ya masuala ya chama hicho.

Chanzo: Azam TV

===

Kila mtu anajua kuwa kura za Zanzibar hupigwa kwa ubaguzi. Yaani Mpemba humchagua Mpemba mwenzaze na Muunguja humchagua Muunguja mwenzake. Wapemba ni wengi kuliko waunguja. Ni dhahiri tangu 1995 mpaka leo Wapemba huwa wana kura nyingi.

Lakini kuna watu walishaona kuwa wao walizaliwa kuwa watawala kisa tu baba zao walishawahi kuwa marais. Hii ni baada ya CCM kuweka mfumo wa kurithishana urais.

Tusijekushangaa Ridhiwani akaja kusema huko mbeleni naye anataka zamu yake kutawala.

Balozi Ali Karume anataka zamu yake awe Rais maana ni ka utamatuduni ka kupeana.

Anaona kama Rais Mwinyi alichukua zamu yake.

Mnamuhoji ili?

Pia soma: CCM Zanzibar kujadili kauli tata za Balozi Karume
 
Hiyo ndiyo CCM.
CCM ni tatizo kubwa Tanzania, Bara na Visiwani.

Tunataka Katiba Mpya, ili tujipange na kuanza upya!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom