CCM Zanzibar yamfuta uanachama Balozi Ali Karume

kambagasa

JF-Expert Member
Aug 18, 2014
2,241
1,749
IMG_7940.jpeg
Halmshauri Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kusini Unguja imemfuta uanachama kada wake Balozi Ali Karume.

Kikao cha kumfuta uanachama Balozi Karume kimefanyika saa saba usiku wa kuamkia leo Jumamosi Julai 8, 2023 chini ya Katibu wa Mkoa wa CCM, Amina Mnacho.

Taarifa ya kumuondosha kwenye chama hicho ilitolewa na Katibu Mwenezi wa Mkoa huo, Ali Timamu Haji.

Hatua hiyo inakuja baada ya chama hicho kumpa onyo kutoka na kauli zake zake akidaiwa kukidhalilisha chama na kuwatukana viongzi wakuu hadharani.

Kutokana na matamshi ambayo Balozi Ali Kalume amekuwa akiyasema likiwemo la CCM Zanzibar haijawahi kushinda uchaguzi na hujuma za kutwaa ardhi ya familia yao zinazofanywa katika Serikali ya Raisi Mwinyi, kikao cha CCM kilichokaa jana usiku huko Zanzibar kimemfuta uanachama Balozi Karume.

Ikumbukwe pia kumekuwa na kutokuelewana kwa muda sasa kati ya Raisi Mwinyi na Balozi Karume kwa kile ambacho Balozi Karume amekuwa akipinga hadharani sera za Mwinyi kuuza visiwa mbalimbali vilivyoko Zanzibar.

Pia soma:
 
Halimashauri kuu ya chama Cha mapinduzi nchini Zanzibari hasa ya Kijiji alichojiungia uana ccm,usiku wa kuamkia Tarehe 8/07/2023 saa Saba usiku imemfutilia mbali uanchama mtoto wa Rais wa kwanza wa Zanzibari

Pamoja na kufukuzwa kwake duru za siasa ndani ya ccm Taifa zinadai yakuwa Leo Tarehe 8/07/2023 wataketi kubariki maamuzi hayo uku Dr Slaa nae anajadiliwa either apewe kalipio Kali au afutiliwe mbali
 
Uamuzi huo umefanywa na Halmshauri Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kusini Unguja dhidi ya Kada huyo aliyekuwa kwenye mvutano na Chama hicho pamoja na Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Hussien Mwinyi.

Kikao cha kumfuta uanachama Balozi Karume kimefanyika saa saba usiku wa kuamkia leo Jumamosi Julai 8, 2023 chini ya Katibu wa Mkoa wa CCM, Amina Mnacho.

Katika moja ya kauli zake dhidi ya CCM, Balozi Karume alikituhumu chama hicho kuingia madarakani kwa wizi wa Kura, akidai CCM haijawahi kushinda uchaguzi wa urais Zanzibar kihalali bali kwa wizi wa Kura.
 
Halimashauri kuu ya chama Cha mapinduzi nchini Zanzibari hasa ya Kijiji alichojiungia uana ccm,usiku wa kuamkia Tarehe 8/07/2023 saa Saba usiku imemfutilia mbali uanchama mtoto wa Rais wa kwanza wa Zanzibari


Pamoja na kufukuzwa kwake duru za siasa ndani ya ccm Taifa zinadai yakuwa Leo Tarehe 8/07/2023 wataketi kubariki maamuzi hayo uku Dr Slaa nae anajadiliwa either apewe kalipio Kali au afutiliwe mbali
Wanaofuta wenzao uanachama ndo wanaotakiwa kufutwa. Ila Kwa vile wameshika mpini wanakata wenzao wanavyopenda.
 
Halmshauri Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kusini Unguja imemfuta uanachama kada wake Balozi Ali Karume.Kikao cha kumfuta uanachama Balozi Karume kimefanyika saa saba usiku wa kuamkia leo Jumamosi Julai 8, 2023 chini ya Katibu wa Mkoa wa CCM, Amina Mnacho.
Ni upuuzi tupu, kwani mtu hapa Tz hawezi kuishi vizuri bila ya kuwa mwanachama wa chama chochote kile cha siasa???
 
Hawajazoea mawazo kinzani, wanashangaza sana, kwao mpaka karne hii wao wanamuona yule mwenye mawazo tofauti nao ni adui yao, hivi hawa viumbe wasioweza kuvumilia upinzani miongoni mwao, wataweza vipi kuvumilia upinzani toka nje?

Ndio maana sasa tunaona wakina Prof. Nshala, na Adv. Mwabukusi, wakitishiwa maisha, kwa sababu tu ya kuwakosoa hawa wajuaji wasioamini mawazo tofauti na yao. Ajabu hili linafanywa chini ya Rais Mwinyi, niliyeamini ana fikra chanya kiuongozi, kumbe nilijidanganya.
 
Back
Top Bottom