kadoda11
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 21,453
- 20,712
oya acha tufanye kazi kwanza.. Sio kwa kunichekesha huku...kweli huyu nyoka mpaka umkanyage, niliwahi kuchunga ng'ombe utotoni nikabanwa na haja kubwa porini, nilipomaliza kukata gogo natafuta jani nichambe, kumbe pale karibu kabisa na niliposhusha gogo alikuwa katulia ananichora tu, ilibidi niondoke taratibu, nikaenda chambia sehemu nyingine, kumsimulia babu akasema huyo sio swila, huyo mpaka umkanyage, ndio akung'ate, na vile vile inasadikika katika kabila langu ukiwakuta kwenye shamba lako la mihogo basi mihogo itanenepa kama lenyewe na inakuwa hivyo, hizo ni imani tu za wahenga