umbea...............

gfsonwin

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
18,274
20,673
jamani leo ni j1-1 ila kiukweli kazi zimeisha mapemaaa kwa ofc sina cha kufanya nikaamua nijitupe jf nikanza MMU nimeona leo hakuna dili na sina topic ya kuitupamo huko nikaona niende siasani nikaona duh! hapa nanukia harufu ya kumtusi mtu sasa nifanyeje? nikaenda kwenye photos huko nikakutana na Boflo nikaona kaamua makusudi kunifupuishia wiki nikasema sasa ili niifupishe vyema basi nije chit chat hapa nipatemo umbea kidogo.

haya sasa shosti wangu na msiri wangu wa ukweli cacico njoo ukiwa na wake wenzio wote BADILI TABIA Yummy pamoja na dada yangu mkubwa AshaDii nipeni umbea jamani lol!

haya wadada wote wa jf nipenipo umbea mkiongozwa na King'asti, Kongosho, snowhite wakiwa na Kaunga nitupienipo umbea tafadhali ninahamu na umbea.

hivi nimesahau wanaume nao huwaga wanagossip sasa leo nataka Mr Rocky, Asprin KARIA Ndahani BAK @mpitwaga Bishanga na wanaume wote wa jf njooni leo mnipenipo umbea jamani.

chombezo: mwanamke umbea kusutwa sunna atii.
 
Last edited by a moderator:
Sasa usingewaita hao wababa manake watatuzidi umbea hapa. Mi naogopa kusema kitu changu, ila kiukwelileo nina mood ya uchonganishi na nna bastola ya kuazima hapa nilipewa na Bashe. Ntarudi kagiza kakiingia

khaaa! sasa raha ya umbea upewe mchana bana tena na mkiwa na mood ya umbea si ya ugomvi atii
 
heeee umejuaje shosti!!! mi pia nna ham ya umbea! c mchezo!!
yan King'asti cjaona ngumi sku nyingi bora tu ugombanishe !! zianzike hapa!!

mimi je ninavyo utamani lol! utaniweza sasa? yaaani mwaya wee acha tuuuu hapa nilipo key bodi inataka kufutika kwa jinsi nlivokuwa na hamu na umbea. halafu umbea ukinoga zuri lazima ngumi zilike si wajua? sasa miye ntakuwa kijumbe wa kudalisha.
 
Sasa usingewaita hao wababa manake watatuzidi umbea hapa. Mi naogopa kusema kitu changu, ila kiukwelileo nina mood ya uchonganishi na nna bastola ya kuazima hapa nilipewa na Bashe. Ntarudi kagiza kakiingia
Hello Chit Chat

ni mara chache sana kupost jukwaa hili...mara nyingi huwa ni mchangiaji au msomaji wa masuala mbalimbali ya kisiasa yanayoendelea kutokea kila siku nchi hii..........

Upepo wa kisiasa umeendelea kuibadili nchi yetu kila kukicha....si jambo la ajabu kukuta watu wamekaa tena vijijini wakijadili mambo mbalimbali ya kisiasa....

nakipongeza pia chama changu cha Chadema kwa kuendelea kuwaamsha watanzania walio wengi juu ya mambo muhimu yanayowahusu na wanachopaswa kukifanya...binafsi nimeamshwa zamani sana.........

sina shaka na uwezo wa wana CDM katika kuwamsha watanzania walio wengi ........katika kujazia kile kilichozungumzwa na bwana Sita leo.........naomba pia safu nzima ya wana CDM kila mmoja kw anafasi yake ajitazame upya status yake maritually..........viongozi (wa CDM) wengi wao wamekua na status zinazofanana na sio sifa nzuri kwa kiongozi hasa wa kiafrika.kama kweli tunatetea tamaduni zetu za Kitanzania tulizorithishwa na babu zetu basi tuliangalie na ilo,na kama kweli tunajiandaa kuchukua dola ya nchi hii..tujipange safu hiyo....................huu ni mtazamo wangu na wala siwakilishi mawazo ya mtu mwingine...viva CDM
 
mimi je ninavyo utamani lol! utaniweza sasa? yaaani mwaya wee acha tuuuu hapa nilipo key bodi inataka kufutika kwa jinsi nlivokuwa na hamu na umbea. halafu umbea ukinoga zuri lazima ngumi zilike si wajua? sasa miye ntakuwa kijumbe wa kudalisha.
haya ngoja tuwasubiri wana chitchat watupe maumbea tusuuze nyoyo!!
 
gfsonwin naona anataka kuanzisha gazeti kama la TANMO.
MBUNGE wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), hatimaye amevunja ukimya na kusema yupo tayari kujiunga na Chama Cha Alliance for Democratic Change (ADC), kama chama hicho kitapinga ubinafsi kwa ajili ya maslahi ya taifa.

Kauli hiyo, ilitafsiriwa kama kijembe kwa wanasiasa wanaofanya vyama kama mali zao binafsi.

Kwa kipindi kirefu sasa, Hamad amekuwa na msuguano na Chama chake cha CUF, hali iliyopelekea kufikishana mahakamani kupinga hatua ya kufukuzwa kwake uanachama pamoja na wenzake 10.

Akihutubia Mkutano Mkuu wa ADC, uliofanyika juzi mjini Dar es Salaam, ambapo Hamad, alikuwa kama mgeni mwalikwa, alisema kupatikana kwa usajili wa kudumu kwa ADC ni kuendelea kufungua njia ya demokrasia nchini.

Alisema vyama vingi vya siasa, vimekuwa na viongozi wengi walevi wa madaraka ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kutatua migogoro ya ndani, kuliko kuwasaidia Watanzania kuondoa matatizo yanayowakabili.

"Ninajua hadi kufikia hatua ya kupata usajili wa kudumu ADC, haikuwa kazi rahisi … kikubwa kinachotakiwa ni kuepuka viongozi walevi wa madaraka, kama ambavyo tumeona siku zilizopita.

"Ulevi wa madaraka ni tofauti na pombe, hakuna dalili ya kuumwa kichwa wakati wowote unapokuwa madarakani, hautoki mwilini mpaka ufe au ufukuzwe. Na humfanya mtu awe haoni wala hasikii na hafahamu isipokuwa yale anayoyataka yafanyike kwa kutumia nguvu za maamuzi.

"Nami nipo tayari kujunga na ADC, wakati wowote huko mbele, ikiwa mtaongoza kwa kuepuka migogoro na kauli za kibabe za sasa bwana mkubwa amesema.

"Wengi wale wanaolewa hubaki na maruirui ya madaraka hata baada ya kustaafu au kutolewa madarakani…kila mlevi wa aina hii, hutaka abaki na madaraka na hufanya kila njia ili alinde madaraka hayo yasimtoke."
 
Nasikia toka Lizzy apotee hapa jamvini Bishanga kawa mpole na ndio hasa nia ya kutulia na mmoja ambae ni The secretary. Nimepata fununu pia kuwa Cantalisia, Mwali, obsesd, Smile na Okya walifumwa wakijadili jinsi gani wanaweza kujisajili kikundi cha wadada wa mjini kwa madai kuwa wanataka wawe wana run lile city la Jamii. Hata hivo hilo lengo lao liliingia dosari kwa sababu hawakuwashirikisha dada zao wakubwa kama Zion Daughter, Roulette, FirstLady1, Chauro, WiseLady, Preta, blacki womani BelindaJacob na Keren_Happuch.

Nasikia chama kuu MMU cha Infidel kinakufa kiutendaji baada ya Kaizer kuonekana anaenda kinyume na sheria mama za chama. Hio imefanya Darling shem Asprin akiongozwa na RR, waite kikao cha dharura cha wanachama wachache tu; yaani Kimey, TIMING, Dreamliner, Baba_Enock, Fidel80, Teamo, The Finest, The Boss, klorokwini, Memo, Bigirita, kwa ajili ya hatma ya hicho chama.

Pia toka chama cha wabeba ma box kisajiliwe na Nyani Ngabu hapa jf nimepata tetesi kuwa kimepata wanachama wengi sana (atae hakiki hizi habari nitashukuru sana), wakiwemo jmushi1, BAK, Kiranga, Steve Dii, Mr Rocky na Ndahani majina mengine sijasikia... Ila Mzee Dark City hata hiyana atanipatia tu. lol

Nilitaka kusahau, soon kwa yeyote mwenye sherehe inayohitaji mapambo na maposhi ya cake afrodenzi kafungua kampuni.
 
Last edited by a moderator:
haya ngoja tuwasubiri wana chitchat watupe maumbea tusuuze nyoyo!!
Jana nimeangalia kwenye TV TBC, Lowasa alikuwa anapinga initiative ya rafiki yake kuhusu kilimo kwanza, anasema yeye anaamini elimu kwanza, kilimo baadae, inawezekana akawa na point, lakini mbona hakuyasema haya alipokuwa serikalinini? make wimbo wa kilimo kwanza JK kauanzisha siku nyingi.​


 
Nasikia toka Lizzy apotee hapa jamvini Bishanga kawa mpole na ndio hasa nia ya kutulia na mmoja ambae ni The secretary. Nimepata fununu pia kuwa Cantalisia, Mwali, @Obsesed, Smile na Okya walifumwa wakijadili jinsi gani wanaweza kujisajili kikundi cha wadada wa mjini kwa madai kuwa wanataka wawe wana run lile city la Jamii. Hata hivo hilo lengo lao liliingia dosari kwa sababu hawakuwashirikisha dada zao wakubwa kama Zion Daughter, Roulette, FirstLady1, Chauro, WiseLady, Preta, blacki womani BelindaJacob na Keren_Happuch.

Nasikia chama kuu MMU cha Infidel kinakufa kiutendaji baada ya Kaizer kuonekana anaenda kinyume na sheria mama za chama. Hio imefanya Darling shem Asprin akiongozwa na RR, waite kikao cha dharura cha wanachama wachache tu; yaani Kimey, TIMING, Dreamliner, Baba_Enock, Fidel80, Teamo, The Finest, The Boss, klorokwini, Memo, Bigirita, kwa ajili ya hatma ya hicho chama.

Pia toka chama cha wabeba ma box kisajiliwe na Nyani Ngabu hapa jf nimepata tetesi kuwa kimepata wanachama wengi sana (atae hakiki hizi habari nitashukuru sana), wakiwemo jmushi1, BAK, Kiranga, Steve Dii, Mr Rocky majina mengine sijasikia... Ila Mzee Dark City hata hiyana atanipatia tu. lol

Nilitaka kusahau, soon kwa yeyote mwenye sherehe inayohitaji mapambo na maposhi ya cake afrodenzi kafungua kampuni.

AshaDii, upo?
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom