Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 38,175
- 47,248
Utaratibu wa familia masikini kuuza watoto wa kike au kuwatoa kama malipo ya mkopo umekuwepo kwa muda mrefu Afghanistan ila kudorora kwa uchumi na kurudi kwa Taliban madarakani baada ya majeshi ya Marekani kuondoka kumezidisha janga hili la kibinadamu na kushuhudia familia nyingi zaidi zikiuza watoto wao wa kike kwa wanaume matajiri na wanaowadai.
Katika biashara hii katili wazee wa hadi miaka 70 wananua watoto wa kike wa hadi miaka sita kwa minajili ya kuwatumia kama wake zao.
Tofauti na nchi nyingi huko Afghanistan hii biashara ni halali kabisa chini ya Utawala wa Taliban!
Watoto wanaonunuliwa wanakuwa katika hali za kusikitisha sana wakilia kwa uchungu mkubwa kuchukuliwa na wanaume watu wazima wasiowafahamu au kujua wanaenda kuwafanyia nini.
Katika biashara hii katili wazee wa hadi miaka 70 wananua watoto wa kike wa hadi miaka sita kwa minajili ya kuwatumia kama wake zao.
Tofauti na nchi nyingi huko Afghanistan hii biashara ni halali kabisa chini ya Utawala wa Taliban!
Watoto wanaonunuliwa wanakuwa katika hali za kusikitisha sana wakilia kwa uchungu mkubwa kuchukuliwa na wanaume watu wazima wasiowafahamu au kujua wanaenda kuwafanyia nini.