Umaarufu wa Lissu umeondoka na JPM? Kwa sasa umeshuka mpaka kufikia asilimia 25, namuona Heche akichukua kijiti

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
12,009
20,684
Ni dhahiri Lissu ni mwanasiasa wa matukio, na huwa anapata nguvu panapokuwa na misuguano kati yake na viongozi wa juu. Na yeye amegundua hilo, kwamba ana thrive kisiasa katika mazingira ya ugomvi na kutukanana.

Ndio maana anaona kwamba wenzake wanapoenda katika maridhiano, ni kama "wanamchimbia kaburi" la kisiasa na anapotezwa. Kwa hiyo anayabeza na kuyakwepa.

Wanasiasa kama Mbowe, ni magwiji wa aina zote za Siasa, za mezani, na jukwaani, na mivutano. Na bado wameendelea kuwaka nyota kisiasa.

Lissu alikuwa maarufu enzi ya JPM kwa sababu kulikuwa na Siasa za ugomvi na kusutana, Sasa katika kusutana nani kama Lissu?

Alipotoka ubeleji na kuingia Tanzania mara ya kwanza, alipokewa na maelfu ya watu, barabara zikajaa watu, baada ya muda alirudi ubeleji bila kusindikizwa na yeyote, baadae akarudi Tanzania, alipokelewa na watu wawili.

Pale singida, alijaribu kuingia mitaani, watu wa Lissu wakitarajia umati mkubwa kumfuata, haikuwa hivyo, alikuwa na viongozi wanne tu wa chama chake.

Morogoro, alikuwa na umati wa kawaida kabisa, ambao unaweza kukusanywa na diwani au Abood katika ngazi ya Kata.

Je, wananchi wamechoshwa na aina ya Siasa zake? Au wamemchoka?

Katika mikutano mingi, hana hoja yoyote zaidi ya kuimba katiba, na neno likirudiwa sana, linachosha, na wananchi wanaona wakienda katika mikutano watakutana na maneno yaleyale, wanaacha kuhudhuria.

Humsikii akijadili kilimo, na sera ya chama chake kuhusu kilimo ili wananchi walinganishe, humsikii akijadili viwanda, humsikii akijadili chochote kipya.

Kwa Sasa umaarufu wa Lissu uko asilimia 25-30, asipoangalia, akina Heche wanachukua ufalme wake muda si mrefu.
 
Cha kushangaza nyie wafuasi wa Magufuli ndiyo mnaongoza kumuandika Lissu hapa jukwaani kuliko hata mnavyowaandika viongozi wenu wa CCM. Ona aibu kuidanganya hata nafsi yako mwenyewe
 
Nimecheka kidogo, tsk tsk....nikikumbuka alivyojaribu kuweka tukio lile la Dodoma hewani tena. Yani kabla hajaenda jukwaan alihakikisha anabakia kwenye vyombo vya habari kwa kulitembelea gari lake(Dr ordered therapy?) basi, kesho yake tukaona magazeti yameweka picha ya gari lile na vijirisasi vile ubavuni mwa V8, hakutoboa. akaanza kuzodoana na mwenzake.:oops:😆😆...kweli Bwana Mzeee Tundu anapenda Umaarufu,Ugomvi na Vijembe...ngoja akitoka Kigoma.
 
Alijipiga risasi ili amchafue JPM lakini ameambulia kuchafuka yeye mwenyewe. Shame up on nyumbus
Hivi una akili sawasawa kweli wewe? Kujipiga risasi manake nn? Unafikiri kujipiga risasi ni sawa na kupiga punyto ? Laana ya kutukana, kuzalilisha, chuki na kuongea uongo itakuandama wewe na vizazi vyako.
Shetani mmoja wewe
 
Mwishoni mwa zama za JK -(Richmond , escrow n.k) pia na zama za JPM na tukio la lisasi vilimpaisha zaidi.

Sahizi atachukua kundi Gani ? Zaidi atazungumzia katiba mpya ambayo Kwa kiasi flani haija kiki saaana kwenye vipaumbele vya watu.

Makundi yapo mawili tu yenye nguvu ni CCM iliopo madarakani na Kundi linalo amini ideology za JPM ambalo kimsingi lipo Lina hang halijapata pa kushikilia , LINA NGUVU KUBWA SANA ,

Vyama vya upinzani vimepotezwa ki ideology na JK, JPM mama anamalizia

JK- Agenda UFISADI
JPM- Agenda KUPINGA UDICTATOR (Acc. To them)
SSH-agenda KATIBA MPYA

Kila kitu tumeonja hapo utakuja na issue Gani Ika kiki kwa watu wengi. Kilichopo Kwa sasa ni makundi mawili tu yaliopo yakisukumana, huku vyama vya upinzani vikiwa kama daraja la Kundi Moja juu ya jingine.
 
Siasa mfuu hizi nilikuwa lunzewe juzi anapita alizoa nyomi km yote niliona kwa macho yangu huku komrade wa ccm katibu mkuu eneo siku ya pili watu waliletwa kwa malori na coaster huku buku5 zikitoka nami nililambishwa gari yangu ulikuwa imeharibika kwa siku nne pale

Sasa unayojisemesha wewe sijui????
Runzewe a.k.a Shamba la Nyege!! Ndo maana walijaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom