voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Kuendelea kumkashifu Magufuli ambaye hayupo Duniani kuja kujitetea!
Ambaye pia huna uhakika ana wafuasi wangapi katika halaiki inayokuwa mbele yako Lissu!bila kujua kwamba unawatonesha kidonda ambacho hakika bado kibichi mioyoni mwao!
Hapo tunasema ni "Techical Failure" Hiyo inakugharimu bila kujua.
Badala yake ungesimamia hoja za kuwaeleza ni mabadiliko gani unaweza kuwaletea watanzania na wafuasi wako,Wewe kupitia chama chako cha Chadema.
Pia utoe elimu kuhusu madhara ya ufisadi pamoja na kukithiri kwa ubadhirifu unaoendelea kwa sasa nchini.
Panga sera zako kwa weledi,Panga maneno yaendane na kilichoko vichwani mwa Watanzania kwa sasa!
Uache siasa za kudandia matukio.toa elimu ya uraia vizuri kupitia jukwaa hilo.Badala ya kuanza mwanzo mwisho kwa mashambulizi binafsi kwa wanasiasa wa milengo tofauti.
Haya matukio uyatumie kama kibwagizo baada ya kumwaga sera za chama chako na njia mbadala za kuwafanya wasikilizaji wako wakuone kama mbeba maono mapya.
Wafanye na uwawezeshe wafuasi wako pamoja na watanzania kuujua umuhimu wa katiba mpya, na pia ubovu wa katiba iliyopo kwa sasa uwaelimishe kwa kina madhara yake kwao kama wanyonge na wakulima wa nchi hii.
Badala ya kufafanua na kuishia kwenye vifungu vile vya kisiasa pekee.huku ukitoa kashfa kwa kada mbalimbali Kama unavyofanya kwa walimu.
Kuna kasoro kubwa au kosa kubwa linalojirudia kila wakati,Na kupelekea kukunyima uungwaji mkono kwa jamii ya wanyonge walio wengi nchini.
Sote ni mashahidi kwamba Lissu amekuwa akitoa lugha za kejeli kwa Hayati John Pombe Magufuli.
Ambaye alikuwa Rais wa awamu ya Tano.
Ambaye katika kipindi cha utawala wake aliizuia mikutano ya kisiasa kwa nchi nzima.
Ukiondoa kasoro kadhaa za kibinadamu alizokuwa nazo marehemu.kama ilivyo kwa binadamu wote.
Magufuli alijioambanua kuwa kiongozi shupavu aliyesimamia kile alichokiamini.Magufuli alishuka kutoka Ikulu na akaamua kuuishi Unyonge sambamba na wanyonge.
Akasmua kuwaambia watanzania ukweli bila chenga!.Hotuba zake zikawa sio za kisiasa bali za kiuanamapinduzi halisi.
Akazindua na kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati.Akaongea na wananchi na kuwapa majobu ya papo kwa papo kuhusiana na kero ambazo wangemtolea kwa wakati husika na eneo la tukio.
Akarudisha nidhamu mahali pa kazi kwenye sekta zote za Umma.Akakataa vyeti feki,Mishahara hewa,Uzembe nk.
Magufuli hakuwahi kuwa na Rafiki wa kufumu pale lilipkuja suala la uzembe,ufisadi au kutowajibika katika utendaji kwenye hufuma za Umma.
Akawanyoosha wezi wote wa mali za Umma katika kipindi kifupi na nchi ikakaa kwenye mstari.
Hata huko ndani ya CCM alihakiki mali zote za chama zinatambulika na kuwa chini ya uongozi wa chama.
Kwa hatua hiyo CCM ikageuka na kuwa chama tajiri, tofauti na hapo nyuma ilipokuwa chini ya Umangimeza wa makada wasio waadilifu.
Kituo cha televisheni cha Chanel Tem ni ushahidi tosha.
Sasa nirudi kwa Tundu Lissu!
Ni kweli kwamba Chadema inapita nchi nzima ikifanya mikutano ya majukwaani na kupokelewa na umati mkubwa wa wasikilizaji.
Lakini pia ni kweli kwamba sio wahudhuriaji wote ni wafuasi wa Chadema.Bali ni watanzania ambao wana kiu ya kuona mabadiliko katika siasa za nchi hii.
Kutokana na kuchoka na kile kinachofanyika sasa na serikali iliyoko madarakani ambayo ni ya CCM.
Hususan eneo zima la Wimbi la ugisadi mkubwa pamoja na ubadhirifu unaoendelea kufanywa katika sekta mbalimbali za umma nchini.
Baadhi ya hao wahudhuriaji pia kuna kundi kubwa la waliokuwa wafuasi wa Marehemu Magufuli. Ambao kwa hali halisi hawamuungi mkono Rais na mwenyekiti wa CCM wa sasa ambaye ni Samia Suluhu Hassan.
Lissu alipaswa kuwa makini kutowaudhi na kuwafanya warudi majumbani kwao wakiwa wamekasirishwa na matusi pamoja na kejeli wanazozisikia zikitoka kinywani mwa Tundu Antipasi Mughwai Lissu.
Wananchi hao wanaporudi makwao ni wazi kabisa wanakuwa wameanza kumchukia Tundu Lissu kwa kitendo cha kumdhalilisha mtu asiyekuwepo hapa Duniani ili kukitetea!
Ambaye pia huna uhakika ana wafuasi wangapi katika halaiki inayokuwa mbele yako Lissu!bila kujua kwamba unawatonesha kidonda ambacho hakika bado kibichi mioyoni mwao!
Hapo tunasema ni "Techical Failure" Hiyo inakugharimu bila kujua.
Badala yake ungesimamia hoja za kuwaeleza ni mabadiliko gani unaweza kuwaletea watanzania na wafuasi wako,Wewe kupitia chama chako cha Chadema.
Pia utoe elimu kuhusu madhara ya ufisadi pamoja na kukithiri kwa ubadhirifu unaoendelea kwa sasa nchini.
Panga sera zako kwa weledi,Panga maneno yaendane na kilichoko vichwani mwa Watanzania kwa sasa!
Uache siasa za kudandia matukio.toa elimu ya uraia vizuri kupitia jukwaa hilo.Badala ya kuanza mwanzo mwisho kwa mashambulizi binafsi kwa wanasiasa wa milengo tofauti.
Haya matukio uyatumie kama kibwagizo baada ya kumwaga sera za chama chako na njia mbadala za kuwafanya wasikilizaji wako wakuone kama mbeba maono mapya.
Wafanye na uwawezeshe wafuasi wako pamoja na watanzania kuujua umuhimu wa katiba mpya, na pia ubovu wa katiba iliyopo kwa sasa uwaelimishe kwa kina madhara yake kwao kama wanyonge na wakulima wa nchi hii.
Badala ya kufafanua na kuishia kwenye vifungu vile vya kisiasa pekee.huku ukitoa kashfa kwa kada mbalimbali Kama unavyofanya kwa walimu.
Kuna kasoro kubwa au kosa kubwa linalojirudia kila wakati,Na kupelekea kukunyima uungwaji mkono kwa jamii ya wanyonge walio wengi nchini.
Sote ni mashahidi kwamba Lissu amekuwa akitoa lugha za kejeli kwa Hayati John Pombe Magufuli.
Ambaye alikuwa Rais wa awamu ya Tano.
Ambaye katika kipindi cha utawala wake aliizuia mikutano ya kisiasa kwa nchi nzima.
Ukiondoa kasoro kadhaa za kibinadamu alizokuwa nazo marehemu.kama ilivyo kwa binadamu wote.
Magufuli alijioambanua kuwa kiongozi shupavu aliyesimamia kile alichokiamini.Magufuli alishuka kutoka Ikulu na akaamua kuuishi Unyonge sambamba na wanyonge.
Akasmua kuwaambia watanzania ukweli bila chenga!.Hotuba zake zikawa sio za kisiasa bali za kiuanamapinduzi halisi.
Akazindua na kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati.Akaongea na wananchi na kuwapa majobu ya papo kwa papo kuhusiana na kero ambazo wangemtolea kwa wakati husika na eneo la tukio.
Akarudisha nidhamu mahali pa kazi kwenye sekta zote za Umma.Akakataa vyeti feki,Mishahara hewa,Uzembe nk.
Magufuli hakuwahi kuwa na Rafiki wa kufumu pale lilipkuja suala la uzembe,ufisadi au kutowajibika katika utendaji kwenye hufuma za Umma.
Akawanyoosha wezi wote wa mali za Umma katika kipindi kifupi na nchi ikakaa kwenye mstari.
Hata huko ndani ya CCM alihakiki mali zote za chama zinatambulika na kuwa chini ya uongozi wa chama.
Kwa hatua hiyo CCM ikageuka na kuwa chama tajiri, tofauti na hapo nyuma ilipokuwa chini ya Umangimeza wa makada wasio waadilifu.
Kituo cha televisheni cha Chanel Tem ni ushahidi tosha.
Sasa nirudi kwa Tundu Lissu!
Ni kweli kwamba Chadema inapita nchi nzima ikifanya mikutano ya majukwaani na kupokelewa na umati mkubwa wa wasikilizaji.
Lakini pia ni kweli kwamba sio wahudhuriaji wote ni wafuasi wa Chadema.Bali ni watanzania ambao wana kiu ya kuona mabadiliko katika siasa za nchi hii.
Kutokana na kuchoka na kile kinachofanyika sasa na serikali iliyoko madarakani ambayo ni ya CCM.
Hususan eneo zima la Wimbi la ugisadi mkubwa pamoja na ubadhirifu unaoendelea kufanywa katika sekta mbalimbali za umma nchini.
Baadhi ya hao wahudhuriaji pia kuna kundi kubwa la waliokuwa wafuasi wa Marehemu Magufuli. Ambao kwa hali halisi hawamuungi mkono Rais na mwenyekiti wa CCM wa sasa ambaye ni Samia Suluhu Hassan.
Lissu alipaswa kuwa makini kutowaudhi na kuwafanya warudi majumbani kwao wakiwa wamekasirishwa na matusi pamoja na kejeli wanazozisikia zikitoka kinywani mwa Tundu Antipasi Mughwai Lissu.
Wananchi hao wanaporudi makwao ni wazi kabisa wanakuwa wameanza kumchukia Tundu Lissu kwa kitendo cha kumdhalilisha mtu asiyekuwepo hapa Duniani ili kukitetea!