Jambo la kwanza la kufanya ni kutoka nyumbani..omba support kwa wazazi nenda mkoa mwingine tofauti na walipo wazazi upange chumba chako uanze kujitegemea. Njaa na gharama za mahitaji mengine zitakupa akili na kukufanya usichague kazi. Hapo utaanza kufikiri na kufanya kazi ili uweze kujilipia kodi, chakula na mavazi baada ya support ya wazazi kuisha.
LABDA NIKUPE HISTORIA YANGU....
Baada ya kumaliza chuo sikurudi nyumbani (nilijua nitalemaa na kuzembea)....nikaenda Dar na kuanza kupambana na jiji..nakumbuka tulikuwa watu 8 tunakaa ghetto moja, kila jioni kila mtu alipaswa alete chochote mezani. Na ukichelewa kulikuwa na kuwahi kitanda, watu wanne walilala kitandani na mliochelewa mnalala sakafuni..mito ilikuwa viatu vya washkaji [emoji23][emoji23]. Na kila siku kulikuwa na zamu ya kupika...Hatujui utapika nini ila tunataka tule na tushibe.Hapo akili ikachaji haraka...nikaomba kujishikiza kwenye stationery moja pale Mabibo Hostel. Nikiwa na laptop yangu niliyotoka nayo chuo na smartphone yangu nikaanza kuwa nawaandikia wanachuo kazi zao wanazopewa (wengi huwa hawana muda kutokana na vipindi kubana), kuweka table of contents, wengine wanakuja na maswali waliyopewa (sana sana individual work) nawafanyia - Si nilikuwa fresh kichwa bado kinakumbuka. Kama sifahamu swali nagoogle. Kutype na kuedit Page nilikuwa natoza Tsh 1000. Table of content ilikuwa Tsh 5000. Bahati nzuri mwaka huo Halotel ndio wamekuja TZ, walikuwa wana promo ya unlimited internet Tsh 1000 kwa masaa 24. Nikawa naweka kifurushi kwa siku nawasha hotspot naunga kwenye computer nawauzia watu internet kwa dakika 15 (Tsh 500), nusu saa (Tsh 1000) na lisaa (Tsh 2000). Pia nikawa nadownload movies na nyimbo nawauzia wanachuo na raia wengine kama siku hiyo sikupata wateja wa internet. Nyimbo moja Tsh 200 na Movie Tsh 500. Hapo nikaweza kupanga chumba changu maeneo ya Riverside (karibu na Mabibo ili kuepuka gharama za usafiri) na kununua mahitaji muhimu (Godoro, feni, vyombo, jiko la gesi na vyakula - mchele, unga, sukari)
Kila siku nilikuwa naomba kazi zisizopungua 5 - sikujali experience,location wala level of employment. Mungu mwema nikapata kazi na sasa nipo kwenye nafasi nzuri.
Naamini nimekuhamasisha.