Mentor
JF-Expert Member
- Oct 14, 2008
- 20,328
- 23,879
Mimi hapa mungwana ninazo hizo tabia
ukweli ninaunena watu wanausikia
kipembeni wanongona maovu kunizulia
Hakika mi habari sina bukheri nimetulia
Uongo wanizulia, walahi sijaunena
tena wanishadidia, wala ukweli hauna
Wacha wako ufisadi, ukweli moyoni huna
Imani yako hupimwa, ovyo hapana ropoka
Tenda wema wende zako, usingoje shukurani,
Yalo mema ya wenzako, yazingatie moyoni,
Usitaje mema yako, kwa fakhari duniani,
Tenda wema usahau, usingoje shukurani.
Muungwana sina shaka nimeswafi yangu nia
Yazidi yangu baraka Mola aniongezea
Yangu yote yanyooka wewe watanga na njia
Wala sito hadhirika kama ulofikiria
Pasta hujanielewa, umekazana na kufoka
sijui umeshalewa, ama kufungwa na Kaka
ubeti (#)3 waongelewa, posti sabini na tatu
sa sema uongo upi, kama si kujifanya fisi!!!!!!!