Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,358
Ha ha nicheke mie,hivi umekaa unasubiri aniletee za kuleta then niku-PM,forget about that!
Hahahaha Acha woga mamii. Ni kwa wema tu.
Ha ha nicheke mie,hivi umekaa unasubiri aniletee za kuleta then niku-PM,forget about that!
Mj1 kweli maji yamefika kwa shingo,mwachie mbawa zote kwangu adondoke,nimpe ya motomoto yako asikumbuke,madoido alokuletea yote yamtoke,ila nakuomba chonde tena usimtake!!!
Shosti unaniangusha, kujiliza hadharani
Chati unampandisha, kakufanya hayawani
Bure unajikondesha, nakujishusha thamani
Amekufanya wa nini, mfanye wa kazi gani.
Mfanye wa kazi gani, amekufanya wa nini
Akipita mtaani, mvalie na miwani
Mmekutana ukubwani, majonzi sasa ya nini
Ulimwengu wa mapenzi, na wewe bado ni memba.
Na wewe bado ni memba, ulimwengu wa mapenzi
Hutakiwi kwenda Pemba, kuyatafuta mapenzi
Wanamuziki waimba, yalianza toka enzi
Aliye na niya hasa, penzi usimbanie.
Penzi usimbanie, aliye na niya hasa
Ila usikimbilie, Fidel Chrispin Masa
Hapana watamkie, usije wapa hamasa
Mbili zero moja mbili, ndoa zao watangaza.
Ndoa zao watangaza, mbili zero moja mbili
Hawajaenda angaza, wameahirisha mara mbili
Hapa nakupa mwangaza, silazimishi ukubali
Ukitala alosoma, jiulize pia why?
Jiulize pia why, ukitaka alosoma
Ningeshauri Bluray, ila kingereza chake noma
Anaongea in a way, tafsiri zinagoma
Pedejee sishauri, unless wahusudu.
Shosti unaniangusha, kujiliza hadharani
Chati unampandisha, kakufanya hayawani
Bure unajikondesha, nakujishusha thamani
Amekufanya wa nini, mfanye wa kazi gani.
..................
Jiulize pia why, ukitaka alosoma
Ningeshauri Bluray, ila kingereza chake noma
Anaongea in a way, tafsiri zinagoma
Pedejee sishauri, unless wahusudu.
take 5Marhabaa!,
Sinalo la kuongeza, na mimi nakusapoti
kama Pele umecheza, ninayarusha manoti!
Ni mengi umemjuza, nakutolea saluti
Tumebaki navidoti, vichwani tunavijaza!
Vichwani tunavijaza, tulivyoweka vidoti
kwa kina ukaeleza, asije kumpa chati
Apate pia mwangaza, amvalie na koti
Nakutolea Saluti, kama Pele umecheza!
Aendelee kuzoza, asidhanie hapati
Mapenzi anayaweza, na tena ana bahati
Mwanajamii waweza, umeambiwa kwa dhati!
Ni mengi amekujuza, na siyo ya kisaliti!
Huyu analipenda limtu lisilo mpenda na kumjali sasa mm nampenda yeye hanipendi umeona sasa ni vice versa mtu umpendae yeye hakupendi na unae mpenda nae hakupendi.
Wasalaamu salamuni, waungwana nawajia
Mababu wa mizimuni, walokwisha tangulia
Najongea kwa huzuni, najizuia kulia
ulimwengu wa mapenzi, buriani aagia
Ulimwengu wa mapenzi, buriani naagia
naondoka kwa majonzi, mlango najifungia
Si wangu nimemaizi, moyo nafungulia
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Umeyataka mabawa, meupe yaso na taka
Nimechoka kupagawa, na penzi lenye mashaka
Ulimwengu wa mapenzi, nawaachia wenye bahati.
Mwana jamii sikia, usia nakupatia
mapenzi yana udhia, kweli ninakuambia
Wengi walivumilia, Wakaishia kulia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Utampenda fulani, kwa yako yote nia
kamuweka fuwadini, Na moyoni kamtia
Atakudharau chini, kulia ukaishia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Njoo kwangu nakuasa, penzi nitakupatia
Uje ule sambuasa, na mikate ya sinia
Utasahau kabisa, moyoni nashuhudia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Beti nne kadi tama, mbele sitoendelea
Takuachia mtima, Moyo wangu upokea
Usibaki tena nyuma, hima na hima jongea
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Ah ah ah ah ah, baba paroko nawe kumbe huwa unatembelea ili jukwaa!Ustaadh , mafunzo ya dini yanaruhusu kutongoza ONLINE?..Bwe hee he he..
Mwana jamii sikia, usia nakupatia
mapenzi yana udhia, kweli ninakuambia
Wengi walivumilia, Wakaishia kulia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Utampenda fulani, kwa yako yote nia
kamuweka fuwadini, Na moyoni kamtia
Atakudharau chini, kulia ukaishia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Njoo kwangu nakuasa, penzi nitakupatia
Uje ule sambuasa, na mikate ya sinia
Utasahau kabisa, moyoni nashuhudia
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Beti nne kadi tama, mbele sitoendelea
Takuachia mtima, Moyo wangu upokea
Usibaki tena nyuma, hima na hima jongea
Mapenzi yataka moyo, kweli ninakuapia
Mkuu tupo tuna jaribu jaribu tu...!Mkuu....kumbe nawe huvumi lakini umo.......Safi sana aisee
Pasta acha uongo, Mola anakuonaMkuu tupo tuna jaribu jaribu tu...!
Pasta acha uongo, Mola anakuona
wewe umo ka kigongo, bahati sijaiona
umeiva kama gongo, mashairi yalotuna
ila acha uongo, kujipigia pasi!
acha kujipiga pasi, subiri akukubali
usilazimishe nafsi, kupenda sipokubali
moyowe huna nafasi, kupenda kusipojali
ashaumizwa jamani, subiri we ahueni.
Kizuri kinajiuza, wahenga walishasema
kibaya chajitembeza, hilo alisema mama
iweje leo kupaza, pendo wataka kufuma
kupenda ye hatoweza, moyowe unamuuma!
Mvumilivu hula mbivu, tena walituambia
kama wazitaka mbivu, mawe hutazitupia
tena uwe msikivu, wa nyakati na hisia
usimtolee uvivu, sababu ameumia!
<usisubiri kuwa fisi kufuata vilojeruhiwa>