Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,358
hahahahahaaaa.Haya Bwana .Pengine ushawahi kulizwa na mapadri,Aisifuye mvua..........
Sijalizwa ilikuwa kidogo nilizwe, mpaka nilipompiga marufuku mshori wangu kuimba kwaya.
hahahahahaaaa.Haya Bwana .Pengine ushawahi kulizwa na mapadri,Aisifuye mvua..........
Dah umeongea kweli,hizi kwaya hizi zinaharibu watu mara nyingi.hasa hawa makwaya masta.Na kwenye kwaya kukuta watu pair si ajabu.Hata Lucifer a.k.a shetani,a.k.a ibilisi naye alikuwa kwayamasta ndio maana ile dhambi inaendelea.Sijalizwa ilikuwa kidogo nilizwe, mpaka nilipompiga marufuku mshori wangu kuimba kwaya.
Dah umeongea kweli,hizi kwaya hizi zinaharibu watu mara nyingi.hasa hawa makwaya masta.Na kwenye kwaya kukuta watu pair si ajabu.Hata Lucifer a.k.a shetani,a.k.a ibilisi naye alikuwa kwayamasta ndio maana ile dhambi inaendelea.
Unaonaje tukianzisha kwaya yetu?
Makubwa,Chrispin nae anataka kuanzisha kwaya nicheke mie
Msindima utakuwa sauti ya kwanza na MJ1, zd na FL1 ya pili, mpwa fidel ya tatu, binamu Nguli ya 4,Mchungaji Masanilo meneja wa kwaya, katekista Geoff mshauri wa kwaya na shemasi mimi ntakuwa kwaya master. Lol! Rose Mhando haoni ndani kwa mauzo ya albam.
Ewaa,lakini mimi namudu sauti zote ya kwanza mpaka ya tatu,na hata ukitaka niwe mwalimu wa kwaya niko fit,haya taja jina la kwaya,nani atakuwa mwenyekiti wa kwaya na mtunza pesa je?
MJ1,vipi tena? umeamua kum-mwaga jamaa?
Wasalaamu salamuni, waungwana nawajia
Mababu wa mizimuni, walokwisha tangulia
Najongea kwa huzuni, najizuia kulia
ulimwengu wa mapenzi, buriani aagia
Ulimwengu wa mapenzi, buriani naagia
naondoka kwa majonzi, mlango najifungia
Si wangu nimemaizi, moyo nafungulia
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Umeyataka mabawa, meupe yaso na taka
Nimechoka kupagawa, na penzi lenye mashaka
Ulimwengu wa mapenzi, nawaachia wenye bahati.
mambo vp?
NiPM basi tutete zaidi, hapa lazima pana mpango wa Mungu.
Mambo kwa Yesu Joyceline,Mama Joe yuko wapi?nimem-miss,mfikishie salamu zangu nyingi sana za Upendo.
La nini hilo agano, njoo nikufungulie
Nieleze shida yako, mimi nikutatulie,
Nshafanya mchakato, kwangu mimi utulie,
Ulimwengu wa mapenzi, ni wetu mimi na wewe!
Ya nini yote majonzi, kwangu ndo umefika,
Nitakupa hevi dozi, utaipenda hakika,
Nimehitimu na kozi, ya mapenzi tikatika
Ulimwengu wa mapenzi, ni wetu mimi na wewe!
Magehema
Zangu nazitanguliza, shukurani zipokee
Unataka niliwaza, huzuni inipotee
Nimekula nimesaza, wali nyama na matonge
Nimeomba pumzika, naomba nikubalie
Nimeomba pumzika, naomba nikubalie
Nayachelea masika, mbani nende jililie
Nayaogopa majoka, moyo sijejipatie
Nakimbiza zangu mbawa, yatosha yalonifika.
Mchungaji Chrispin umefunuliwa na Bwana kuhusu hii kwaya?halafu wewe uwe kwaya masta? hata sikuamini kama unaweza kulitangaza neno wewe kwa uaminifu. Mpiga Kinanda atakuwa nani?
Pole dada pole, pole mwana jamii
mapenzi polepole, ndani ya yetu jamii
ulianza hisi polepole, ukadhani huumii
sasa yamegonga kole, watutangazia jamii
nimekusoma kwa kitambo, kwenye forum ya jamii
unalalama kimtindo, ewe mwanajamii
wengi tuliona kombo, kama wana jamii
tukasema mweke kando, akuumizaye mwanajamii
Vera na nyamayao, walikupa zao bidii
wote jinsia yao, walijituma kwa bidii
vidume ni kama zao, wakaanza kwa bidii
wakakaa kimkao, wakusherehe kibidii
lakini hadi sasa, ewe mwana jamii
sipati hata msasa, na kuelewa hii jamii
ni vipi twatakasa, tena kwa zetu bidii
kutoa ndoa takasa, ya Muumba kwa bidii?
Leom utatunga mashairi mpaka utakoma.
Chriss please mwache MJ1,maneno gani hayo ya kumwambia mwenzako?
Nimekoma mama. Ngoja nikajiliwaze na mchumba wangu Serengeti Lager. Hanitesi kama MJ1 anavyoteswa.