Ulianzaje kujenga?

Ulianzaje kujenga?

Kitu nimewahi kujenga ni mahusiano mazuri tu na bangi, kwa jinsi muda unavyoenda kasi nafikiri nitakufa bila kujenga hata banda la kuku
Muda wako ukitimia utajenga... Labda tu kama huna nia
 
Kwakweli kujenga naweza kusema ni mipango tu ya Mungu lakini ukiwa umeweka nia thabiti...
Muda unapotimia bila nguvu wala kashkash unajikuta kiwanja hicho... Unaweza kukaa muda mfupi au mrefu kidogo mara umepata pesa ya tofali, mara hiki mara kile.. Mpaka unamaliza ujenzi
Cha ajabu na cha kushangaza, ukimaliza tu ujenzi naweza kusema kwa asilimia 80 hivi pesa inakata na kupitia kipindi kigumu sana lakini uko kwako
NB: Hii haiwatokei watu wote lakini kwa asilimia kubwa huwa hivyo..
[/quoted] Hapo kwenye pesa kukata ni kweli huwatokea wengi na unaweza kujiuliza vipi ningekuwa nyumba ya kupanga? Mwenyezi Mungu wakati huo riziki anakuwa amempatia mwingine.
 
Habari za muda huu wanajamvi wenzangu

Kama uzi unavyojielezea, kuna watu wengi wanatamani kumiliki mjengo mjini lakini hawajui waanzie wapi, wapitie wapi, wafanye nini, watiririke vipi hatua kwa hatua za ujenzi na hivyo kukamilisha ndoto zao.

Kwa wewe mwenye uelewa au uliyefanikisha katika hili tunaomba tips zako, na vile ulivyofanikisha kusimamisha mjengo mjini.

NB: Mimi bado sijafanikisha hivyo naamini kuna vitu vingi nitajifunza hapa.

Karibuni
Iba mkuu
 
Baaada ya kununua kiwanja nilijenga kwa awamu Tatu na nimerumia almost miaka miwili na nusu

1)awamu ya kwanza nilitafuta milioni 10 nikanunua mifuko ya sementi, tofali,nondo, nikalipa fundi, jenga ukuta na kuchimba mashimo ya vyoo

2) awamu ya pili nilikaa miezi kama 12 nikapasahau pakaota mpaka majani nikajichanga milioni 12 nikapaua nyumba, bandaling kabisa, chonga madrisha ya gril, milango nilichongea kijjn coz mbao ni rahisi nilipelekea fundi sampo ya mlango, grill ya mbele na nyuma na vyoo nikanunua kabisa, nikaomba umeme,nikavuta na maji,

3) awamu ya tatu nikajipanga na 2mill nika pinga plazta vyumba viwili nikatengeneza chumba changu nikahamia

4) awamu ya nne natengeneza chumba kimoja kimoja mana siulizwi na mtu kwanza naishi kwangu na dilisha zangu za wavu nikipata ka laki nanunulia tiles mbona sina mwaka nyumba itaisha
Sarut mkuu

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom