DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati na kusuluhisha mvutano uliokuwepo kati ya klabu za Yanga na Simba kuhusu ratiba ya mchezo wao, imeleta utulivu mkubwa kwa Taifa na mashabiki wa soka nchini.
Akizungumza leo Jumamosi, Juni 14, 2025, wakati wa hafla ya kukagua miradi ya maendeleo katika uwanja wa ndege wa Msalato jijini Dodoma, Ulega amesema Rais Samia ameonesha mfano wa uongozi wenye hekima na usikivu kwa kutatua changamoto iliyokuwa ikiibua sintofahamu na hisia kali kwa mashabiki wa soka.
"Jana lilikuwa jambo kubwa ulilolifanya, pale ulipokutana na viongozi wa vilabu viwili vikubwa hapa nchini, Simba na Yanga. Kazi ile ya kihistoria uliyoifanya jana, umeituliza nchi, umewatuliza wapenda soka na Taifa kwa ujumla. Sasa kila mmoja anaelewa kuwa mchezo utafanyika kama ilivyopangwa," amesema Ulega.
Itakumbukwa kuwa, awali mchezo huo namna 184 wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga, ambao ni wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya NBC, ulipangwa kufanyika Machi 8, 2025, kabla ya kuahirishwa. Hata hivyo, baada ya mvutano uliohusu ratiba na maandalizi ya mchezo huo, Bodi ya Ligi (TPLB) ilitangaza rasmi kwamba mechi hiyo itachezwa Juni 25, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Akizungumza leo Jumamosi, Juni 14, 2025, wakati wa hafla ya kukagua miradi ya maendeleo katika uwanja wa ndege wa Msalato jijini Dodoma, Ulega amesema Rais Samia ameonesha mfano wa uongozi wenye hekima na usikivu kwa kutatua changamoto iliyokuwa ikiibua sintofahamu na hisia kali kwa mashabiki wa soka.
"Jana lilikuwa jambo kubwa ulilolifanya, pale ulipokutana na viongozi wa vilabu viwili vikubwa hapa nchini, Simba na Yanga. Kazi ile ya kihistoria uliyoifanya jana, umeituliza nchi, umewatuliza wapenda soka na Taifa kwa ujumla. Sasa kila mmoja anaelewa kuwa mchezo utafanyika kama ilivyopangwa," amesema Ulega.
Itakumbukwa kuwa, awali mchezo huo namna 184 wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga, ambao ni wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya NBC, ulipangwa kufanyika Machi 8, 2025, kabla ya kuahirishwa. Hata hivyo, baada ya mvutano uliohusu ratiba na maandalizi ya mchezo huo, Bodi ya Ligi (TPLB) ilitangaza rasmi kwamba mechi hiyo itachezwa Juni 25, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.