Ukweli mchungu: Vifurushi vipya vya NHIF vitaumiza wanachama zaidi ya kikokotoo kinavyoumiza wafanyakazi

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,838
18,250
Watu mnaopigia debe vifurushi vipya vya NHIF mnapaswa kutafakari kwa umakini sana. Hivi vifurushi vipya ni vya kipuuzi na ovyo kuliko kikotoo na sheria mpya ya mafao kwa wenza wa vigogo.
1710762911847.png

Kigezo kimoja tu kinachotumiwa kuwapinga AFTHA ni kukosa ubinadam....kwamba walipaswa kutoa notice ya siku 90. Hiki ndicho kichaka ambacho serikali inajificha. Lakini vipi kuhusu NHIF kubadilisha bei ya vifurushi bila kutoa notice kwa watoa huduma au wao hawahitaji kutoa notice? Nafahamu unapoingia mkataba unaingia pia mkataba wa bei za dawa na huduma. Ukibadilisha bei maana yake umevunja mkataba hivyo mnapaswa kukaa mezani na mtoa huduma kubadilisha vipengele vya mkataba au kuingia mkataba mpya.

Nawahakikishia hivi vifurushi vipya ni kandamizi kwa mteja ndio maana waziri Ummy alivisitisha. Kwanini NHIF wanataka kuvipitisha kibabe kwa maslahi yao binafsi badala ya kuzingatia maslahi mapana ya wanachama (wagonjwa)? Huoni kuwa NHIF wanatumia mwanya huu kuwahujumu na kuwakandamiza wanachama wao?

Huu ujinga wanaofanya NHIF ni zaidi ya ule wa kikokotoo kilichopambwa na kupigiwa debe sana na serikali. Mwanzoni kulikuwa na wajinga fulani walioingia mkenge na kukikubali kikokotoo lakini sasa kila mtu analia.

Serikali hii haijawahi kufanya mabadiliko yanayomnufaisha mlalahoi. Mfano halisi ni hii sheria ya kipuuzi ya mafao kwa wake za viongozi. Wanakomba fedha zote za taifa kukipa kikundi cha wachumiatumbo wachache huku wananchi wakiendelea kutopea kwenye umasikini wa kupindukia✍️

 
Watu mnaopigia debe vifurushi vipya vya NHIF mnapaswa kutafakari kwa umakini sana. Hivi vifurushi vipya ni vya kipuuzi na ovyo kuliko kikotoo na sheria mpya ya mafao kwa wenza wa vigogo.

Kigezo kimoja kinachotumiwa kuwapinga AFTHA ni kukosa ub8nadam....kwamba walipaswa kutoa notice ya siku 90. Hiki ndicho kichaka ambacho serikali inajificha. Lakini vipi kuhusu NHIF kubadilisha bei ya vifurushi bila kutoa notice kwa watoa huduma au wao hawahitaji kutoa notice? Nafahamu unapoingia mkataba unaingia pia mkataba wa bei za dawa na huduma. Ukibadilisha bei maana yake umevunja mkataba hivyo mnapaswa kukaa mezani na mtoa huduma kubadilisha vipengele vya mkataba au kuingia mkataba mpya.

Nawahakikishia hivi vifurushi vipya ni kandamizi kwa mteja ndio maana waziri Ummy alivisitisha. Kwanini NHIF wanataka kuvipitisha kibabe kwa mslahi yao binafsi badala ya kuzingatia maslahi ya wanachama (wagonjwa). Huoni kuwa NHIF wanatumia mwanya huu kuwahujumu na kuwakandamiza wanachama wao?

Huu ujinga wanaofanya NHIF ni zaidi ya ule wa kikokotoo kilichopambwa na kupigiwa debe sana na serikali. Mwanzoni kulikuwa na wajinga fulani walioingia mkenge wa kukikubali kikokotoo lakini sasa kila mtu analia.

Serikali hii haijawahi kufanya mabadiliko yanayomnufaisha mlalahoi. Mfano halisi ni hii sheria ya kipuuzi ya mafao kwa wake za viongozi. Wanakomba fedha zote za taifa kukipa kikundi cha wahuni wachache huku wsnanchi wakiendelea kutopea kwenye umasikini wa kupindukia✍️
Na bado hamjasema ninyi wezi wakubwa ,mnataka panad mlipwe 500 wakati mtaani ni 250?mnafanya biashara kwenye afya za watu ,kama hautaki si unaacha hakuna aliyekulazimisha ,tibu kwa cash
 
Watu mnaopigia debe vifurushi vipya vya NHIF mnapaswa kutafakari kwa umakini sana. Hivi vifurushi vipya ni vya kipuuzi na ovyo kuliko kikotoo na sheria mpya ya mafao kwa wenza wa vigogo.

Kigezo kimoja kinachotumiwa kuwapinga AFTHA ni kukosa ub8nadam....kwamba walipaswa kutoa notice ya siku 90. Hiki ndicho kichaka ambacho serikali inajificha. Lakini vipi kuhusu NHIF kubadilisha bei ya vifurushi bila kutoa notice kwa watoa huduma au wao hawahitaji kutoa notice? Nafahamu unapoingia mkataba unaingia pia mkataba wa bei za dawa na huduma. Ukibadilisha bei maana yake umevunja mkataba hivyo mnapaswa kukaa mezani na mtoa huduma kubadilisha vipengele vya mkataba au kuingia mkataba mpya.

Nawahakikishia hivi vifurushi vipya ni kandamizi kwa mteja ndio maana waziri Ummy alivisitisha. Kwanini NHIF wanataka kuvipitisha kibabe kwa mslahi yao binafsi badala ya kuzingatia maslahi ya wanachama (wagonjwa). Huoni kuwa NHIF wanatumia mwanya huu kuwahujumu na kuwakandamiza wanachama wao?

Huu ujinga wanaofanya NHIF ni zaidi ya ule wa kikokotoo kilichopambwa na kupigiwa debe sana na serikali. Mwanzoni kulikuwa na wajinga fulani walioingia mkenge wa kukikubali kikokotoo lakini sasa kila mtu analia.

Serikali hii haijawahi kufanya mabadiliko yanayomnufaisha mlalahoi. Mfano halisi ni hii sheria ya kipuuzi ya mafao kwa wake za viongozi. Wanakomba fedha zote za taifa kukipa kikundi cha wahuni wachache huku wsnanchi wakiendelea kutopea kwenye umasikini wa kupindukia
Hivi kabla ya kuandika huwa tunakuwa tumepata taarifa au. Hayo majadiliano na watoa huduma si yamefanyika kwa takribani miezi 8..NHIF ilipotaka kuanza kutumia huo utaratibu mpya si Waziri alisitisha ikabidi warudi kwenye meza ya mazungumzo sio peke yao bali awepo mediator ambayo TIRA ilihusika ku mediate.
Kwenye maridhiano yeyote kuna kupata na kuachia baadhi na hilo limefanyika.
Kutokubaliana kwenye baadhi ya masuala ni sehemu ya maridhiano.

Mgogoro wa gharama kubwa za tiba na dawa ambazo vituo binafsi vimekuwa vikipeleka bili zao zilipwe na NHIF ambazo hazilingani na bei ya soko au uhalisia huo ni ufisadi mkubwa wa fedha za wanachama.
Mf. Unakuta kipimo x ni sh 50,000 sehemu ya kwanza.. Kipimo hichohicho ni sh 80,000 sehemu ya pili.. Kipimo hicho hicho ni sh 250,000 sehemu ya tatu.. Halafu wote huko wanapeleka bill NHIF iwalipe kwa sababu wateja wa bima walipata kipimo hicho hicho sehemu tofauti tofauti hivi kweli wewe ndiye ungekuwa umepewa dhamana ya kusimamia hiyo michango ya wanachama ungefanya nini???
Ungeona ni sawa tuu.

Tukumbuke tumumbuke kuwa fedha zote zilizopo bima ya afya ni michango ya wanachama sio za serikali, nasisitiza ni za wanachama sio za serikali... Je wanachama wangepewa nafasi kuhudhuria hayo majadiliano juu ya suala la bei za huduma zisizolingana na uhalisia je unadhani wangekuwa upande gani?

Kosa nalo liona ni wachangiaji wa mfuko wa bima ya afya kutoshirikishwa kwa vile hakuna chama cha wachangiaji wa bima ya afya Tanzania.
Mijadala wanakaa wanaotaka kulipwa fedha yaani watoa huduma ambao kipaumbele kwao ni super profit kama ilivyo kwenye biashara yeyote..
Wanajadiliana na mtunza fedha za wanachama bila wanachama wenyewe kushirikishwa waamue juu ya gharama zipi wanaruhusu zikubaliwe au laa.

Kitakachoenda kutokea endapo bima ya afya wakikubaliana na suala la kila kituo kjiamulia chenyewe gharama za dawa na matibabu watakavyo na bima ikawalipa tuu... Mfuko huo lazima ufe....
Au viwango vya kuchangia lazima vipandishwe na mwanachama asilalamike na la tatu ambalo ndilo linaendelea sasa ni matibabu yamelimitiwa sana sana, masharti ni mengi na kuna huduma zitaendelea kuondolewa.
Mnaoenda hospital mnajionea jinsi huduma za bima siku hizi zilivyongumu utadhani unataka kuchukua mkopo benki.
 
Back
Top Bottom