Wakati mwingine kunahoja nyingine ukiziangalia na kuzisoma na zinaweza kukuhadaa kuwa za kweli vile na mtu akajitutumua kuuaminisha umma jambo kana kwamba anauhakika nalo kiutafiti kwa asilimia mia.
Haiwezekani mtu akaja na vihoja vyake hapa bila utafiti na kuuaminisha umma huo ndiyo ukweli.
1.Mtoa hoja anaweza kutueleza ni utafiti gani alifanya kujua watu wa mitaani ndiyo ni wanafundisha vizuri kuliko darasani?
2.Ni wanafunzi wangapi walifundishwa mtaani na wakafanya vizuri kuliko wale waliofundishwa na walimu darasani?
3.Ufaulu wao ulikuwaje?
4.Alipataje sampuli yake kufikia hitimisho hilo?
5.Ni walimu wangapi aliopitia vyeti vyao nakujirisha kuwa hakuna walimu wenye A za masomo tajwa?
6.Alitumia vigezo gani kujua kama walimu ni matokeo ya kushindwa maisha?
7.Anathibitishaje kuwa mwalimu kuto deliver vya kutosha darasani kunatokana na mwalimu kuwa anaufaulu hafifu?
8.Inawezekanaje kuwe na watu wengi mtaani wenye A+ za sayansi pasipo kupita kwa walimu?Hao wanazalishwa na nani?
9.Nafasi za visababishi vingine kama,utayari,ukosefu wa maabara,madawa, maslahi duni ,nk aliweka wapi?
10.Katika kila shule ni wanafunzi wangapi hupita mikononi mwa non-professional teachers na wangapi hupita kwa professional teachers na mpishano ni asilimia ngapi?na mwaka gani?
11.Ni mtaalamu gani au chombo gani kilithibitisha ubora wa hao wanaojiita walimu wa mitaani?
12.Kwaasilimia ngapi ya hao wanaojiita walimu wa mitaani ipo kwa kila somo?
Haya ni maswali machache tu naweza mwuliza mtoa hoja,yapo zaidi ya hayo,nikijibiwa vema naweza kukubali hoja za mtoa mada,zaidi ya hapo alikuwa afurahisha umma.
Mwalimu Nyerere naye! Jee vipi mwalimu maghufuri wote walikuwa viraza. Ngoja niwambie kitu ufaulu wa masomo sio kigezo tosha cha kumfanya mtu awe mwalimu bora! Mwalimu anaweza akapata hata hizo dvns za mwisho kama msemavyo lakini akaandaliwa vya kutosha na akawa mwalimu bora kuliko hata hao waliofanya vizuri katika masomo yao. Kitu kingine Tanzania ni nchi inayotumia mtaala mmoja kitu ambacho kwa shule za vijijini ni changamoto kwa sababu utamkuta mtoto kule kijijini anao uwezo mkubwa kuliko wa mjini anajituma kadiri ya uwezo wake mwisho wa siku anapata dvn III kutokana na changamoto za kijijini lakini yule wa mjini anapata dvns II ukiwachukua hawa wote wawili na ukawaweka ktk darasa moja na kuwandisha utabaini utofauti wao ambaye yule wa shule za kayumba tena za vijijini yuko vzr kuliko wa mjini. So I would like to conclude that, having division 1 or 2 doesn't mean of being a good teacher. Good teacher iz created no matter what divions she/he has......ni hayo tu. Think big....!!!