Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 1,137
- 2,702
Viongozi wetu wamekuwa mara kwa mara wanafanya majaribio ya kitaaluma na wakati wote majaribio hayo yameacha simanzi kwa baadhi ya wanafunzi ambao ndio wahanga wakati wote
Humu katikati kuliibuka waziri aliyeunganisha somo la Physics na Chemistry likawa somo moja (Chemistry with Physics),
Akaja mwingine akafuta somo la Book-keeping, commerce, agriculture na michezo mashuleni
Lakini cha ajabu chuo kikuu cha Kilimo - SUA, vyuo vya uhasibu na kozi za biashara vyuoni hakuzifuta sijui alitegemea wataalamu hao watoke wapi
Akaja mwingine na kampeni za BIG RESULTS NOW
Mwingine akaibuka na kutanga kuifuta division ZERO akaweka viwango anavyovijua yeye na matokeo yakawa yanasomeka kwa lugha nyingine nakumbuka neno moja tu "Distinction"
Sasa tunaye Proff. Mkenda amekuja na mtaala mpya (ulioboreshwa) ambao unawaruhusu wanafunzi kujichagulia masomo /combination mara tu wanapoingia kidato cha kwanza tofauti na miaka ya nyuma ambapo walisoma masomo yote hadi kidato cha tatu kabla ya kuchagua michepuo waipendayo
Mtaala huu unawagawa wanafunzi mara tu wanapoingia kidato cha kwanza, wale wanaosoma sayansi si lazima kwao kusoma masomo ya sanaa kama History, na wale wanaosoma masomo ya sanaa sio lazima kwao kusoma masomo ya sayansi kama Biology, Physics wala Chemistry toka kidato cha kwanza huku somo la Commerce likigeuzwa kuwa Bussiness studies na limekuwa la lazima kwa kila mwanafunzi likienda sambamba na Historia ya Tanzania na Maadili linalofundishwa kwa Kiswahili ambalo limekuja kufuta somo la Civics
Maelekezo ya wizara ni kwamba walimu wawashauri wanafunzi wakashauriane na wazazi wao michepuo waipendayo
Ni jambo jema sana lakini lenye angalizo kubwa sana.
Hapa nadhani wamefanya tafiti kwa kuzingatia watoto wanaoishi mazingira wezeshi ya tafakuri hiyo
Kuna watoto wanaishi na wazazi ambao hawajawahi kukanyaga darasani. Hawa wanapata shida sana na walimu wao. Hata hajui ndoto zake ni zipi anaenda kwa kufuata mkumbo. Hata hivyo naamini ikishazoeleka changamoto hii itaondoka yenyewe lakini wakuathirika watakuwa wamekwisha athirika na watanufaika watakaofuata
Katika hili la mtaala mpya limekuja na kitu kinaitwa "AMALI"
Hapa ndo pamenifanya nikumbuke namna elimu yetu inavyochezewa kwa majaribio yanayoacha simanzi kwa wanafunzi
Kwenye maandishi huu mtaala unaotaja amali unavutia sana. Yaani hadi unaona raha na unaweza kushawishika kumpongeza aliyebuni hiki kitu cha mtaala wa amali
Kwamba watoto watajifunza na kupata ujuzi utakaowafanya wamudu stadi za maisha na kujiwezesha baada ya kidato cha nne. Inavutia, inapendeza
Kwa tahadhari serikali imeanzisha mchepuo huu wa amali kwa baadhi ya shule za sekondari (sio zote). Wameteua shule chache kwa kila mkoa/halmashauri na kuzianzishia huu mchepuo wa amali
Hata hivyo tahadhari hiyo bado imekuwa ya kimagumashi kama kawaida yao
Shule nyingi zilizopewa huo mchepuo wa amali hazina miundombinu rafiki ya kuhudumia mchepuo husika
Shule inapelekewa mtaala wa amali kwa fani ambayo haina mwalimu wa fani husika. Kwa mfano, kuna shule zimepelekewa fani za ushonaji bila kuwa na miundombinu wala walimu wa ushonaji, kuna shule zimepelekewa fani ya kilimo bila kuwa na miundombinu ya kilimo na kadhalika
Wanafunzi wamekaa mwaka mzima (mtaala umeanza mwaka jana 2025) bila kufanya kitu cha maana.
Hapa unajiuliza, kati ya kuanzisha mtaala husika mashuleni na kuandaa miundombinu na walimu kipi kilitakiwa kuanza?
Kwamba hili nalo halikufahamika? Kwamba wasomi wetu hawakulijua? Unaweza kuhamia kwenye nyumba ambayo haujajenga?
Kusema kwamba wasomi wetu na viongozi wetu hawakulijua si sawa. Ila ni kwasababu wanazozijua wao wenyewe ndiomaana wameanzisha mtaala bila kuandaa wataalamu wala miundombinu
Na kingine cha msingi kabisa hapa wahanga si watoto wao. Naamini hivyo
Swala fikirishi katika mtaala huu wa amali ni hili la vyuo vyetu vya VETA
Ukiangalia kwa undani hili swala la kuanzisha mafunzo ya amali linafanana kwa asilimia 100% na mafunzo yanayotolewa na vyuo vya VETA. Kwa lugha rahisi hakuna kitu kipya kilichoanzishwa
Kwa mtazamo huo, unaweza kujiuliza kwanini serikali isingeboresha hivi vyuo vya VETA vikawa na uwezo wa kuwapokea na kuwahudumia wanafunzi wote wanaopenda na waliochagua kusoma mchepuo wa amali?
Huku sekondari walipowapeleka hakuna karakana, hakuna walimu wa amali wala mazingira yanayoonekana ya kutoa ujuzi
Hawa watoto wanaosoma mchepuo wa amali wanaruhusiwa kusoma masomo machache tu ya sekondari ambayo wangeweza kuyasoma huko huko VETA.
Kwanini serikali yetu inapenda kujipa mzigo isioweza kuubeba? Kwanini wataalamu wetu hawalioni hili?
Tuseme somo la amali litashamiri na kuvutia wanafunzi wengi na wakati huo huo kuna taasisi ya VETA inatoa mafunzo hayo hayo tena kwa ufanisi mkubwa. Kwanini wasiiongezee nguvu taasisi hiyo hawa vijana wakaenda kupata ujuzi huko na maboresho yakafanywa kwa kuwapa certificate zinazolingana na ujuzi wao na nyongeza ya NECTA kama hofu ni hicho cheti cha form four?
Swala lingine lililonifanya niseme viongozi wanachezea elimu yetu ni hili la kubadilika badilika kwa viwango vya ufaulu na alama za ufaulu
Miaka ya nyuma kidogo daraja "A" lilisoma mwanafunzi akipata alama 85+ lakini siku hizi ni alama 75+ kwa sekondari
Wastani wa serikali hasa kuvuka kidato cha Pili kwenda cha tatu ulikuwa wastani wa 30 kwa masomo saba ya msingi, lakini siku hizi ni ufaulu wa masomo mawili tu kwa alama 30 (yaani upate 30 masomo mawili au 45 kwa somo moja). Hii maana yake ni Division four na hata mwanafunzi wa kidato cha nne naye anapimwa hivyo hivyo
Hapa ni maandishi yanayosomeka kwenye makaratasi / miongozo yao lakini ukiongea na walimu wanaofundisha na yale wanayoyashuhudia kwenye usahihishaji wa kitaifa na matokeo yanapotangazwa vinakuwa vitu viwili tofauti
Wenyewe (Walimu) wanasema kunakuwa na maelekezo mengi ya kuhakikisha wanasahihisha kwa umakini lakini kwa kuangalia "mwelekeo" wa alichoandika mwanafunzi kama kinaelekeana na jibu sahihi basi apewe alama hata kama hakufikia kwenye jibu lenyewe.
Hata hivyo, pamoja na kufuata maelekezo hayo bado matokeo yanapotangazwa wanabaki kuduwaa kwa kuona ufaulu mkubwa tofauti na uhalisia waliouona wanaposahihisha.
Hili limebaki kuwa siri ya NECTA. Wanachokifanya wanakijua wao wenyewe kwasababu wanaoingiza alama za wanafunzi ni walimu lakini hata wao hubaki na butwaa matokeo yanapotangazwa
Hali hii imepelekea vyuo vya kati na vyuo vikuu kupokea wanafunzi wenye uwezo mdogo wa kumudu masomo kwa ngazi husika
Hali hii inazalisha watumishi wasio na uwezo katika fani zao na matokeo yake ni Taifa kushindwa kusonga mbele
Humu katikati kuliibuka waziri aliyeunganisha somo la Physics na Chemistry likawa somo moja (Chemistry with Physics),
Akaja mwingine akafuta somo la Book-keeping, commerce, agriculture na michezo mashuleni
Lakini cha ajabu chuo kikuu cha Kilimo - SUA, vyuo vya uhasibu na kozi za biashara vyuoni hakuzifuta sijui alitegemea wataalamu hao watoke wapi
Akaja mwingine na kampeni za BIG RESULTS NOW
Mwingine akaibuka na kutanga kuifuta division ZERO akaweka viwango anavyovijua yeye na matokeo yakawa yanasomeka kwa lugha nyingine nakumbuka neno moja tu "Distinction"
Sasa tunaye Proff. Mkenda amekuja na mtaala mpya (ulioboreshwa) ambao unawaruhusu wanafunzi kujichagulia masomo /combination mara tu wanapoingia kidato cha kwanza tofauti na miaka ya nyuma ambapo walisoma masomo yote hadi kidato cha tatu kabla ya kuchagua michepuo waipendayo
Mtaala huu unawagawa wanafunzi mara tu wanapoingia kidato cha kwanza, wale wanaosoma sayansi si lazima kwao kusoma masomo ya sanaa kama History, na wale wanaosoma masomo ya sanaa sio lazima kwao kusoma masomo ya sayansi kama Biology, Physics wala Chemistry toka kidato cha kwanza huku somo la Commerce likigeuzwa kuwa Bussiness studies na limekuwa la lazima kwa kila mwanafunzi likienda sambamba na Historia ya Tanzania na Maadili linalofundishwa kwa Kiswahili ambalo limekuja kufuta somo la Civics
Maelekezo ya wizara ni kwamba walimu wawashauri wanafunzi wakashauriane na wazazi wao michepuo waipendayo
Ni jambo jema sana lakini lenye angalizo kubwa sana.
Hapa nadhani wamefanya tafiti kwa kuzingatia watoto wanaoishi mazingira wezeshi ya tafakuri hiyo
Kuna watoto wanaishi na wazazi ambao hawajawahi kukanyaga darasani. Hawa wanapata shida sana na walimu wao. Hata hajui ndoto zake ni zipi anaenda kwa kufuata mkumbo. Hata hivyo naamini ikishazoeleka changamoto hii itaondoka yenyewe lakini wakuathirika watakuwa wamekwisha athirika na watanufaika watakaofuata
Katika hili la mtaala mpya limekuja na kitu kinaitwa "AMALI"
Hapa ndo pamenifanya nikumbuke namna elimu yetu inavyochezewa kwa majaribio yanayoacha simanzi kwa wanafunzi
Kwenye maandishi huu mtaala unaotaja amali unavutia sana. Yaani hadi unaona raha na unaweza kushawishika kumpongeza aliyebuni hiki kitu cha mtaala wa amali
Kwamba watoto watajifunza na kupata ujuzi utakaowafanya wamudu stadi za maisha na kujiwezesha baada ya kidato cha nne. Inavutia, inapendeza
Kwa tahadhari serikali imeanzisha mchepuo huu wa amali kwa baadhi ya shule za sekondari (sio zote). Wameteua shule chache kwa kila mkoa/halmashauri na kuzianzishia huu mchepuo wa amali
Hata hivyo tahadhari hiyo bado imekuwa ya kimagumashi kama kawaida yao
Shule nyingi zilizopewa huo mchepuo wa amali hazina miundombinu rafiki ya kuhudumia mchepuo husika
Shule inapelekewa mtaala wa amali kwa fani ambayo haina mwalimu wa fani husika. Kwa mfano, kuna shule zimepelekewa fani za ushonaji bila kuwa na miundombinu wala walimu wa ushonaji, kuna shule zimepelekewa fani ya kilimo bila kuwa na miundombinu ya kilimo na kadhalika
Wanafunzi wamekaa mwaka mzima (mtaala umeanza mwaka jana 2025) bila kufanya kitu cha maana.
Hapa unajiuliza, kati ya kuanzisha mtaala husika mashuleni na kuandaa miundombinu na walimu kipi kilitakiwa kuanza?
Kwamba hili nalo halikufahamika? Kwamba wasomi wetu hawakulijua? Unaweza kuhamia kwenye nyumba ambayo haujajenga?
Kusema kwamba wasomi wetu na viongozi wetu hawakulijua si sawa. Ila ni kwasababu wanazozijua wao wenyewe ndiomaana wameanzisha mtaala bila kuandaa wataalamu wala miundombinu
Na kingine cha msingi kabisa hapa wahanga si watoto wao. Naamini hivyo
Swala fikirishi katika mtaala huu wa amali ni hili la vyuo vyetu vya VETA
Ukiangalia kwa undani hili swala la kuanzisha mafunzo ya amali linafanana kwa asilimia 100% na mafunzo yanayotolewa na vyuo vya VETA. Kwa lugha rahisi hakuna kitu kipya kilichoanzishwa
Kwa mtazamo huo, unaweza kujiuliza kwanini serikali isingeboresha hivi vyuo vya VETA vikawa na uwezo wa kuwapokea na kuwahudumia wanafunzi wote wanaopenda na waliochagua kusoma mchepuo wa amali?
Huku sekondari walipowapeleka hakuna karakana, hakuna walimu wa amali wala mazingira yanayoonekana ya kutoa ujuzi
Hawa watoto wanaosoma mchepuo wa amali wanaruhusiwa kusoma masomo machache tu ya sekondari ambayo wangeweza kuyasoma huko huko VETA.
Kwanini serikali yetu inapenda kujipa mzigo isioweza kuubeba? Kwanini wataalamu wetu hawalioni hili?
Tuseme somo la amali litashamiri na kuvutia wanafunzi wengi na wakati huo huo kuna taasisi ya VETA inatoa mafunzo hayo hayo tena kwa ufanisi mkubwa. Kwanini wasiiongezee nguvu taasisi hiyo hawa vijana wakaenda kupata ujuzi huko na maboresho yakafanywa kwa kuwapa certificate zinazolingana na ujuzi wao na nyongeza ya NECTA kama hofu ni hicho cheti cha form four?
Swala lingine lililonifanya niseme viongozi wanachezea elimu yetu ni hili la kubadilika badilika kwa viwango vya ufaulu na alama za ufaulu
Miaka ya nyuma kidogo daraja "A" lilisoma mwanafunzi akipata alama 85+ lakini siku hizi ni alama 75+ kwa sekondari
Wastani wa serikali hasa kuvuka kidato cha Pili kwenda cha tatu ulikuwa wastani wa 30 kwa masomo saba ya msingi, lakini siku hizi ni ufaulu wa masomo mawili tu kwa alama 30 (yaani upate 30 masomo mawili au 45 kwa somo moja). Hii maana yake ni Division four na hata mwanafunzi wa kidato cha nne naye anapimwa hivyo hivyo
Hapa ni maandishi yanayosomeka kwenye makaratasi / miongozo yao lakini ukiongea na walimu wanaofundisha na yale wanayoyashuhudia kwenye usahihishaji wa kitaifa na matokeo yanapotangazwa vinakuwa vitu viwili tofauti
Wenyewe (Walimu) wanasema kunakuwa na maelekezo mengi ya kuhakikisha wanasahihisha kwa umakini lakini kwa kuangalia "mwelekeo" wa alichoandika mwanafunzi kama kinaelekeana na jibu sahihi basi apewe alama hata kama hakufikia kwenye jibu lenyewe.
Hata hivyo, pamoja na kufuata maelekezo hayo bado matokeo yanapotangazwa wanabaki kuduwaa kwa kuona ufaulu mkubwa tofauti na uhalisia waliouona wanaposahihisha.
Hili limebaki kuwa siri ya NECTA. Wanachokifanya wanakijua wao wenyewe kwasababu wanaoingiza alama za wanafunzi ni walimu lakini hata wao hubaki na butwaa matokeo yanapotangazwa
Hali hii imepelekea vyuo vya kati na vyuo vikuu kupokea wanafunzi wenye uwezo mdogo wa kumudu masomo kwa ngazi husika
Hali hii inazalisha watumishi wasio na uwezo katika fani zao na matokeo yake ni Taifa kushindwa kusonga mbele