Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 Oct 2011

Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 Oct 2011

'Wadudu' 150!? Linapokuja suala la kupima malaria,hospitali ya aga khan wanalo tatizo.....inawezekana ni mpimaji au vifaa wanavyotumia. Nimeshawahi kusikia malalamiko kutoka kwa watu kadhaa juu ya hosp hii kutokuweza kuona malaria.
 
mkuu zito pole sana na hiyo safari ndefu ya majaribu'upone haraka tuna kazi ngumu ya kumalizia tulioanza kuyafanya
 
HOH. ZITTO ZUBERI KABWE,
TANZANIA LOVES YOU (ref. prayers from around the world). SIMPLY SMILE AND REST ASSURED YOU WILL GET WELL VERY SOON.
GLK.
 
Kuna hospitali nyingine hata kama huna Malaria lazima watakuambia una vijidudu ili wakutibu wapate chao.
Ni kweli mkuu ndio maana hata mimi nilikuwa napuuza lakini kwa shuhuda hizi,siwezi kuzipuuza!
 
HOH. ZITTO ZUBERI KABWE,
TANZANIA LOVES YOU (ref. prayers from around the world). SIMPLY SMILE AND REST ASSURED YOU WILL GET WELL VERY SOON.
GLK.
Agakhan navyojua huwa ni hoteli ya dawa
 
Nilikuwa nimfunga ngoja leo nifungue kwa hii habari. Alievumisha kuwa umekufa alaaniwe.
 
Bado hujamaliza kazi aliyokupangia Mwenyezi Mungu kwa Watanzania. Hakika Mungu tunayemtumai atakuponya ili uje kuendelea na ratiba yako.
 
Pole sana kaka, huo ugonjwa ulioutaja yaan sinusitis ni kweli huambatana na homa kali sana including maumivu makali ya kichwa, mi hii kitu ilinitesa zaidi ya miaka 10, nilikuwa na malaria isiyoisha, maumivu makali ya kichwa na homa kali. nilienda Indraprastha Apollo hospital India wakafanya sugery sasa niko poa, sipati homa wala malaria yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Naamini utarudi ukiwa salama na wa afya njema kabisa wakiishafanya surgery kwa kutumia kifaa maalumu kiitwacho functional endoscopic sinus surgery-FESS, India wako makini na matibabu na zaidi ya yote wako cheep gharama zao.
Watanzania wenzangu
huu ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine, mpambanaji wenzetu atarudi salama salimini, ni ugonjwa unaotibika kwa kufanya upasuaji na mgojwa hupona na kurudi hali yake ya kawaida. Tumwombee upasuaji ufanyike salama.
 
Kwa kweli sikuwa na imani kabisa kwani uvumi ulichukua kasi kubwa...Nashukuru Mh Zitto umeamua kutuhakikishia usalama wako so far..Ukifanikiwa kupitia hii post, soma Hebrews 13:6...Bwana Mungu ndiye atakayekusaidia..mwanadamu atakutenda nini? Get well soon
 
Nadhani hii itakuwa imesaidia kuondoa doubt zote kuhusu ugonjwa wake.
 
pole sana ndugu yetu, mwenyezi Mungu akuafu! Inshallah
 
Pole sana Mheshimiwa!!!!
Kwa kweli Agha Khan kuna tatizo!! kuna haja ya watafiti kuichunguza hiyo hospitali!! kuna watu kadhaa ninaowafahamu wamewahi kukutana na mazingira yaliyokukuta wawili kati ya hao walipoteza maisha!!!!
Kwangu mimi aliyekuokoa ni yule aliyeshauri upelekwe muhimbili!!
AGAIN! POLE SANA MPIGANAJI WETU!!
 
Pole sana mkuu usijali,tunakuombea Mungu upone ili uje ktk uwanja Wa mapambano.Ila nimejifunza jambo juu ya hospital zinazofanya biashara na zile zinazotoa matibabu,kweli hakika tutakufa sana.
 
Get well soon,Brother! Umati wa vijana wa kitanzania tunakuombea sana,Mh.
 
Ndugu yangu Zuberi, nakuombea kwa Mola, Allah, SWT, upone haraka, na upasuaji utakaofanyiwa uende salama. Wewe ni shujaa wa Watanzania wote, bado tunakuhitaji kamanda!

./Mwana wa Haki
 
Pole sana Kaka Zito, Allah akuponye haraka!
Namimi nina tatizo kama hilo lako, ilinichukuwa muda sana kujuwa....!

Nimekuwa na tatizo la kupoteza fahamu tangu 1996 nikiwa form I pale Ilboru Secondary, lakini sikuwahi kulihusisha tatizo hilo na ungonjwa huu wa sinusitis, bali nilidhani ni PRESSURE ndivyo nilivyokuwa naambiwa na madaktari wetu hapo Bongo, mpaka hii leo ninapoisoma hii taarifa yako ndo napata mwanga kwamba huenda hata huku kuanguka na kupoteza fahamu kwangu kunatokana na ugonjwa huu sugu wa sinusitis!

Kilichonifanya nijue kama nna ugonjwa huu wa sinusitis, ni baada ya kupoteza uwezo wangu wa kunusa harufu na kuandamwa na flu zisizokwisha...mwaka 2007 nikiwa hapa Sweden, ndio niligundulika kwamba ni SINUSITIS, ambayo tayari ilishakuwa sugu, hizo dawa alizo suggests mdau hapo juu haziwezi kusadia tena ikishafikia stage hio ya usugu, kwa hiyo nilifanyia upasuaji mwaka huo 2007. Lakini hiyo pia si suluhisho la kudumu, sababu hizo polyps zinaota tena, hivyo basi baada ya muda (miaka 2) unatakiwa kurudi kwa checking, kama zitakuwa zimeota tena na ku block njia ya hewa, basi unapasuliwa tena!

Mimi bado sijarudi tena, sababu upasuaji wangu wa kwanza ulikuwa na complication (ulichukuwa masaa 3.30 badala ya 1.45 zilizokusudiwa), sababu nilikuwa nilitoka damu mno, kiasi walishindwa kukata hizo polyps zote, hivyo imenijengea woga wakurudi tena. Inshaallah nikipata ujasiri ntarudi tena. Alienifanyia upasuaji ni daktari bingwa wa ENT hapa Sweden, Dr Morgan!

Mh Zitto, nakutakia matibabu yenye mafanikio, Allah akujaalie uwe mwenye kupona haraka!
 
Kila la kheir ndugu yetu. Mungu akutangulie katika hiyo surgery ya kichwa, Amina
 
Back
Top Bottom