Ukweli kuhusu ATCL Boeing 787-8

Ethiopian Airlines and Air Austral are just two of the carriers that have bought the "terrible teens" airplanes.
That said, it's almost certain that the airlines received massive discounts on the 787-8's $224 million sticker price.
 
Ethiopian Airlines, anazo 787-8 pia ambazo sio "Terrible teens"
 
Ndugu ubishi wa nini
Ndege zimetengezwa 20 za mwanzo na zikatokea kuwa zinahitajika marekebisho na baada ya marekebisho ndio zikaongezeka uzito na masafa yakapungua na kampun zilizo order wakazikataa.
Ndege iliyonunuliwa ni moja kati ya hizo ishirini za mwanzo na karibia zoote zishauzwa kama inavyoonyesha kwenye post ya mwanzo kwa nusu bei. Na shida sio ndege, shida ni bei waliyoinunulia ni bei ya mwanzo au ni bei baada ya punguzo.
 


Mkuu ndege iliyotolewa order na tz bado IPO kwenye matengenezo wala haijakamilika au nimekosea?
 
1. Ndege zote 12 zipo kwenye order na zingine zisha chukuliwa.

2. Ndege za mwanzo zilitengenezwa kwa composite materials hasa titanium badala ya aluminum iliyo zoeleka ndio maana zikawa nzito. Matoleo mapya yote Boeing wametumia aluminum zaidi ili kuzifanya ndege zisiwe na uzito mkubwa.

3. Ukiweka order ya unaweza ukatoa pesa yote ama kulipia kidogo kidogo, ukikamilisha ndio unapewa mzigo wako. Tz hatujakamilisha deni. Sie ndege yetu ipo... Bado rangi tuu, tungekuwa hatudaiwi tungepewa mwaka huu.

4. Model ya 787-8 kabla haijatoka tayari ilikwisha wekewa order, ndege zilizo doda zilikataliwa sababu ya uzito makampuni yakachukua ndege zilizo tengenezwa baadae ambazo zilikuwa nyepesi.

NB. Jisomee zaidi,
www.businessinsider.com/boeing-787-dreamliner-terrible-teens-2016-7
 
Mkuu ndege iliyotolewa order na tz bado IPO kwenye matengenezo wala haijakamilika au nimekosea?
Ndege imeshafanyiwa matengezo au niseme ishakamilika.
Lakini ukitoa order ya ndege kuna mahitaji ya mnunuzi lazima yatengezwe kwenye kiwanda chenyewe mfano viti vya ndani unataka viwe vingapi na mpangilio gani. Je unahitaji wifi ndani au unahitaji ndege nzima iwe economic class na isiwe na classes zingine. Na hivyo vitu si kama umetoa order leo kesho wanakutengezea, hapana hivyo vitu vinachukua muda na kwa mpangilio. By the way mm si expart saana kwenye aviation.
Lakini nasisitiza ya kwamba shida sio ndege, shida ni kwenye bei. Je ni bei ya mwanzo au ni bei ya baada ya punguzo. Ni hio tu.
 


Heee!!
Mkuu mbona umekwenda nje ya maswali yangu.
Hebu rejea vizuri.
Mwenzo ulisema zilitengenezwa ndege 20( ndege zilizokamilika) bahati mbaya zikawa na uzito mkubwa zikakataliwa. Then zikapunguzwa bei ndipo zikauzwa zikabaki 12. Hayo ni maaelezo yako hapo juu.

Nikakuuliza swali.

Hizo ndege 12 za toleo la kwanza (zenye uzito mkubwa na kupunguzwa bei) Bado zipo hadi sasa???

Nikauliza tena
Katika Maelezo yako ulisema ndege iloyowekwa oda na tz ni moja ya hizo ndege za toleo la kwanza.( ambazo ni ndege kamili tayari)
Sasa kwanini hii ndege yetu bado IPO kwenye matengenezo??? Kama ni moja ya zile za toleo la kwanza ambazo ni ndege tayari zinasubiri mnunuzi???? Ni matengenezo yepi sasa yanayofanywa???

Nikakuuliza tena
Kama ndege yetu ni moja ya hizo za toleo la awali kwanini hatukupewa moja kwa moja (kwasababu ni ndege tayari) badala yake tunaambiwa bado ipo kiwandani ikitengenezwa???
Inamaana hapa hii ndege sio moja ya hizo za toleo la kwanza (nzito ) ambazo zimepunguzwa bei, kama zingekuwa ni hizo hakukuwa na haja ya kutengeneza mpya.
Inammana basi hii ndege yetu IPO katika hizo za toleo jipya ambazo zimeongezewa aluminium ili kupunguza uzito(ambayo ndio kasoro ya ndege za kwanza hadi kupunguzwa bei).
Na kama ni hivo Inamaana hizi za toleo jipya hazina punguzo la bei(ambayo na yetu ikiwemo), zenye punguzo la bei ni zile za kwanza(ambazo yetu haipo kwasababu yetu ndio kwanza inatengenezwa bado hajakamilika).

Sasa hii hoja kuwa tumepigwa inakujaje hapa??

Au ulifuatilia hizo ndege za toleo jipya bei yake???
 
Bombardier ni shiiidah.... Ful mpela mpelaaaaa! Zngekua ndege kubwa zile ungekua tumefunika hatar n air tanzania yetu bongo
 
Wewe unayekijua umenizidi nini mimi!?

Ha ha haaaaa

Ungetumia ka akili kidunchu husinge bwabwaja eeeeeeh, furahia kiingilishi chako hicho

Vipi juzi hukuguswa na yale maana, unaponda sana ya serikali hii na kumuonea wivu Mheshimiwa wetu mpendwa.
Kwan... Kwan ingilisi ndo nn
 
Ahaa sasa nimeelewa.
Kwahiyo mkuu unatuambia kuwa matengenezo tunayoambiwa ni ya vitu vidogo vidogo tu.
Na sio kwamba tunatengenezewa ndege mpya kabisa????

Nauliza hivyo kwasababu kama ingekuwa ndege mpya kabisa basi isingekuwa kwenye list ya zile za bei ya punguzo.
Ila mkuu uwe na uhakika kwamba si ndege mpya (ila ni marekebisho kutokana na matakwa ya mnunuzi). La sivyo tutapotosha watu hapa ujue.
 

Ila wewe ni muongo sana na sidhani kama huwa unaenda kanisani, Serikali ilishatenga fedha zote za ununuzi wa ndege hizo na zipo cash Rais alishatamka hadharani, eti hakuna hela ndiyo maana bado haijachukuliwa- UTAKUJA KUUMBUKA NI JAMBO LA MUDA TU UKAGUZI WA NDEGE INAYOJENGWA UTAKAPOANZA. ILA KUNA WATU WAONGO SANA MPAKA UNAOGOPESHA!
 
Umebeba website ya ajabu unasema ni boeing? Chukua hyo domain uone niya nan
 
Maelezo mareeeeeeeeeeeeeeeeefuuuuuuuuuuuuuuuuuuu LAKINI KIFUPI TUMEPIGWA KWELI.....

Maelezo marefu kama haya yalishawahi tokea
1. kwenye RADA hadi ikazaa NENO chenji..., VIJISENTI..., joka lenye makengeza
2. Kwenye ndege ya RAISI... hata ikibidi kula nyasi tule... LAKINI LAZIMA INUNULIWE
3. Kwenye EPA........ Eti mwizi baada ya kurudisha tukamsamehe.... LAKINI ANAYEJUWA KAMA KARUDISHA KWELI NI MMOJA AU WACHACHE... why????? ......... JUST BECAUSE.....

KIFUPI TAFUTENI NAMNA YA KUMUINGIZA LOWASA KWENYE HILI LA BOMBADIA ILI MPATE KUPUMUA
 
AHahahahahahaahaha hapo kwenye BOLD umenichekesha sana.... mnawezaje kurekebisha makosa BILA KUYAKUBALI KWANZA?
 
Ww tmoro pipo

Boeing 787 Register - Welcome

Hii domain ya www.b787register.com c website ya boeing.

Tuletee kutoka kwenye hii website
www.boeing.com hii ndo website ya boeing

Ili uhakikshe nachosema ingia hapa

www.whois.com afu weka hxo website watakuambia nan mmiliki.

Kwa ufupi
Ww na zzk mmereport habar kama ya tbc ya trump kumsifia namesake wake. Mlitakiwa mfukuzwe huku JF[emoji3] sorry nimetania tu.
 
One man show
Tumepigwa tena kama tulivyopigwa kwenye Mv Dar es salaam
Kama tulivyopigwa kwenye ishu ya wale samaki nknk
Zilipowekwa taratibu za kiongozi kufanya kazi na Wasaidizi huru, washauri huru na timu huru za kitaalam zenye weledi na uzalendo... Ilikuwa ni kwa ajili ya kuepusha kupigwa kama hivi
Sasa Kama timu za Wasaidizi washauri na wataalam hazipo huru na kigezo kikubwa ni kujua kusoma na kuandika tutegemee nini kama sio hasara na hasara zaidi?
Kwenye hili nani atawajibika je government procurement facility walishirikishwa kwa kiwango gani, bank kuu na hazina je?
Unapokuwa mbabe na mjuaji kuna wababe na wajuaji zaidi yako but in a very sophisticated way... And that's what happened kwenye Manunuzi ya dear bombardiers
Tulihoji sana sababu za kununua kwa cash, kitu ambacho sio cha kawaida lakini kuna timu zilikuwa zimeandaliwa kutetea kwa nguvu zote.. Lakini tulitimiza wajibu wetu
 
Mkuu upo? Pole kwa matatzo aisee!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…