Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

duh ee mungu kwanini ni ngumu kufuta kumbukumbu kichwani na kusahau mabaya? tungekua Computer bas tungefuta hard disk za ubongo wetu na kuinstall window mpya.

btw hiv hakuna dawa ya kuformat ubongo
 
Yaani hapo mama kubwa ni bora uchague moja kulipa kisasi ama kusamehe, kwani kwa kutosamehe kwa kisingizio cha kuogopa dini wakati bado limekukaa rohoni nahisi unadanganya nafsi yako pamoja na imani yako.
 
Nimesoma kwa makini andiko hili na nimetoka na jumuisho hili,Kwa kawaida kulipa kisasi ni rahisi kuliko kusamehe, hivyo mwanadamu wa kawaida atapenda kulipa kisasi kuliko kusamehe, lakini je kwa wale wanaonamini katika MUNGU -JEHOVA ndivyo inavyotakiwa kuwa? ulipe kisasi?

Kwa mtu anayetamani kuiona mbingu siku moja andiko hili linahitaji fikra ya ziada kwani tiyari Mungu amesema usiripe kisasi, na kisasi ni mali yake wala siyo ya mwanadamu. Waebrania 21.14 Mungu anawagiza mtu aishi na watu wote kwa amani, tunajua amani inakuja kwa msamaha na wala si kwa kisasi, ni rahisi mtu kujifunza ndani ya msamaha lakini kisasi kinaleta kisasi kingine uzao hadi uzao, kabila hadi kabila na taifa hadi taifa.

Mapigano tuliyo nayo leo na hayaishi ni kwa sababu watu wamejaribu kulipa kisasi, wameshindwa na mwisho wake wanarudi tena kwenye msamaha. Toka nimekuwa na akili, hakuna mgogoro ulioanza kwa kisasi ukaisha, ila nimeona migogoro imeanza kwa kisasi na ikaisha kwa msamaha, na hii ndiyo kanuni aliyoiumba Mungu kwamba wema utaushinda uovu. Hivyo kabla hujawaza kullipa kisasi kumbuka ipo siku mtakaa kwenye meza kupatana ili mmalize.

Kwa mkristo yeyote, kipimo chako cha msamaha kwa wengine ndiyo, msamaha wako kwa Mungu hivo usitegeme kusamehewa kama hukusamehe Marko 11:25,26. Na watu wajue, Mungu alitusamehe ili yeye awe na amani nasi, hivyo tunasamehe for our own sake, for our own well being, Msamaha kwa wengine ni upuzii lakini kwa mkristo ni afya ya moyo na uzima wa mifupa yetu, usije jaribu kumsamehe mtu ukafikiri ataona umefanya jambo la maana sana na anaweza kukudhihaki kuwa umemuogopa, lakini wewe jua unatengeneza nafsi yako na MUNGU wako.

Nashauri Mkrisro kusamehe ni lazima na sio ombi kama unatamani kuingia mbingu mpya siku moja. Ukikuta unashindwa kusamehe, jua kipawa cha roho mtakatifu kipo mbali nawe, kikija karibu utasamehe moyoni hata kabla mdomo hajasema kitu. Kumbuka kazi ya roho mtakatifu ni kutupatanisha sisi kwa sisi, pia wewe na mwili wako, lakini pia wewe na MUNGU wako, wala haesabu maovu.

Waza Mungu ange kuhesabia makosa yako ungekuwepo?, na kama watu wake MUNGU wakilipa kisasi je washetani watafanyaje? na tofauti kati ya hizi falme mbili itaonekanaje?
Thanks kwa andiko lako.
 
Kaniwekea sumu imeathiri kizazi siwezi kuzaa tena na sina mtoto naanzaje kumsamehe?

Pole sanaaa, sikuwa na nia ya kujua tatizo lako, ila nilitaka tupate mfano unaweza kutufanya tujifunze, juu ya kusahau na kusamehe. Hilo ni tatizo kubwa sana na kitendo husika kingeweza kukusababishia kifo pia, kwani kumuwekea mtu sumu ni kitendo cha kinyama na cha kiuwaji kabisa lakini Mungu mwena unaishi.

Shida kubwa ni kwamba sasa huwezi pata mtoto na mambo mengine yanayoweza tokana na tatizo lenyewe, lakini wapo wengine hawawezi pata watoto pia na hawana mtu wa kumlaum, ila wanatatizo sawa nawe. maumivu ya moyo wao ni sawa na wako yaani kukosa mtoto, japo yako yanaweza kuwa makubwa zaidi kwa sababu unaye wa kumnyoshea kidole, kwamba kama sio yule X ningekuwa na watoto.

Tutafakari je ambao hawana mtoto na hawajui nani aliyesababisha na pengine madaktari wamewaambie hawawezi kuzaa milele, watamnyoshea nani kidole juu ya hali yao? wengine wamefanikiwa kuzaa watoto hawajiwezi na ni mateso kwao watanyosha vidole vyao kwa nani?.

Tafaakri pia Maumivu unayopata kwa kumshikiria moyoni, huyo aliyekujeruhi, unafikiri naye anayapata? nani anayeumia kila siku kama sio wewe?, nakwa bahati mbaya sana kwa sababu mwili na moyo havikumbiwa kubeba baadhi ya mizigo, kama dhambi,chuki, hasira, visasi, wivu na husuda, kitakochotokea ni magonjwa mwilini. magonjwa ya tumbo(vidonda), pressure, magonjwa ya moyo, maumivu ya kichwa nk.

Hii ni kwa sababau mwili umetwishwa mzigo usioweza beba, Mungu hakuumba mwili kubeba hayo na ndiyo maana unapata maumivu. ili ujue hii ni kweli ukienda hosptal watakwambia unafikiri sana, sana sana watakwambia nenda kwa wanasaikologia sabababu umebaba kitu ambacho mwili hauwezi beba, sio orignal yake.

Ni kweli tunataka watoto lakini, wanatoka kwa Mungu na hutupa kwa imani, hata wewe unaweza kupata kwa imani.Ili uwe huru mwachile huyo mtu, sio kazi rahisi lakini ni kwa ustawi wako na yayobaki lia na MUNGU na atakwambia likopasalo.
 
Hatutakiwi kulipa kisasi bali kutoa adhabu. Ukishindwa kuwasamehe wanaokukosea wape adhabu inayostahili ili iwe fundisho kwao na kwa wengine pia!
 
Sikumbuki kama nimeshawahi katika maisha yangu kulipa kisasi, ila hata leo hii nimemsamehe dogo aliyekua ameniudhi toka juzi, roho nyepesiii
 
ea22182088793d94f7d1d66b1dddcb77.jpg
hii ya leo ni tofauti kidogo na mada zetu zile , hii inahusika na kulipa kisasi
Katika maisha bila kujali unaamini nini hakuna jambo jema kama kusamehe!msamaha hukusaidia mengi mpaka kifo na maisha yanayofuata baada ya kifo iwe reincarnation au rebirth nk !msamaha hukufanya uwe mwema mwenye furaha ya kweli usiye na makunyanzi rohoni na usoni
Mwenye msamaha ana nuru usoni , msamaha ni tiba, msamaha ni mafanikio msamaha ni amani na ni upendo
Lakini je kama huamini katika msamaha? Kama unayemsamehe hasameheki? Na je kama ni mbabe mjuaji na dhulumati mkubwa?je kama anakuletea dharau kwa hali yoyote ile hata uwe msamehevu kiasi gani? Usiishi na maumivu! lipa au lipiza..!
Msamaha wako usikushushe msamaha wako usikufanye kiumbe dhaifu na mnyonge, utu wako ni muhimu heshima na dhima yako ni vitu vya kulinda na kuzingatia mno...ukishindwa kabisa kusamehe ukizidiwa na viwango vya uvumilivu wa kibinadamu usiumize roho yako andaa kisasi
Kama ilivyo kwa msamaha ile nafuu unayoipata kwenye kusamehe basi ndivyo ilivyo hata kwenye kisasi! Kisasi humpa mtu faraja na amani ya moyo huridhika kuona amefanya jambo baya kwa mtu mbaya
Tunaishi na wajuaji wengi kwenye jamii tunaishi na watu wanaojiona wao ni bora kuliko wengine wao ni zaidi kuliko wewe...wao ndio wanaijua pesa kuliko wewe. . . . usimpe nafasi mtu wa namna hii atambe...ni lazima umfundishe ajue kuwa maisha yana pande nyingi...kisha mfundishe kwa maumivu makubwa maumivu atakayodumu nayo mpaka kifo
LAKINI maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua...Fanya kile kitakachokupa nafuu ya rohoni na afya ya akilini kwakuwa uamuzi ni wako na mwisho utabaki wewe kama wewe ....visasi misamaha na malipizi vitabaki kuwa uamuzi binafsi kutokana na imani yako hofu yako na huruma yako
Kwa knowledge yangu ndogo ya psychology we unatatizo na MTU umejaribu kusamehe umeshindwa au hutaki!! Na the only option you see is revenge!! Na unataka support ya hilo!! I'm out!! Bible inasema kisasi hakimalizi ugomvi au tatizo ila huleta machafuko zaidi hata mauti zaidi!! Kama unaona kisasi kitakusaidia Fanya ila jiandaae na lolote litalotokea as a consequences!! Maana msamaha huwa ni full stop!! Wewe unatafuta "DOs" au Go On"
 
Back
Top Bottom