Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

Mshana Jr Umeeleza Vyema Sana. Kwa Kuongezea, Ili Mtu Atoe Mzigo Uliomkaba Shingoni Basi Kina Mambo Mawili Hapa
1. Kusamehe,
2. Kisasi.

Lakn Lazma Tujue Kwmb Kusamehe Ni Jambo Gumu Sana Ambalo Wengi Wengi Tunalifanya Lakn Tunabaki Na Makandokando Na Hatuishi Kuelezea Tulilotendewa Huku Chuki Ikichukuwa Nafasi Kubwa Nyoyoni Mwetu.

Kusamehe Na Kusahau Si Jambo Rahis Kama Humtegemei Mungu.

Mshana Jr Watu Wangekuwa Wanakuelewa, Wangekuelewa Vizuri Sana Lakn Mlengo Wa Tafsiri Zao Kwao Ni Hasi.
Nguvu ya msamaha ni kubwa sana ikiwakilisha Nuru na nguvu ya kisasi pia ni kubwa ikiwakilisha utawala wa giza...binadamu wengi wana roho ya Kimungu ndani yao ndio maana hukinzana sana na nafsi zao linapokuja suala la kisasi au msamaha
 
Ni lazima uamue moja kati ya kusamehe ama kulipa kisasi ndipo amani itakujia.
Otherwise hutapata amani kamwe.
Nimeamua kuishi hivyo na maumivu sina jinsi jambo limetokea zaidi ya miaka 16 lkn maumivu yake utafikiri ni jana.Siwezi kwenda kinyume na imani yangu na nimejitahidi kusamehe nimeshindwa kabisa.
 
Mimi huwa nasamehe na kusahau hata kama ninayemsamehe anazidi kunitendea mabaya, katika mafundisho ya dini tumefundishwa Usilipize ubaya kwa ubaya bali baya kwa jema japo kuna watu ni wagumu kusamehe na kusahau.
 
Nimeamua kuishi hivyo na maumivu sina jinsi jambo limetokea zaidi ya miaka 16 lkn maumivu yake utafikiri ni jana.Siwezi kwenda kinyume na imani yangu na nimejitahidi kusamehe nimeshindwa kabisa.
Usiishi na maumivu wala usijiweke njiapanda bila sababu fanya moja kati ya mawili,
Ushauri mbaya; lipa kisasi kupunguza maumivu kisha tubu
 
Nimeamua kuishi hivyo na maumivu sina jinsi jambo limetokea zaidi ya miaka 16 lkn maumivu yake utafikiri ni jana.Siwezi kwenda kinyume na imani yangu na nimejitahidi kusamehe nimeshindwa kabisa.
Basi ni heri ukasamehe kama imani yako inavyokuelekeza kuliko uwe vuguvugu (between). Pole sana
 
Mimi huwa nasamehe na kusahau hata kama ninayemsamehe anazidi kunitendea mabaya, katika mafundisho ya dini tumefundishwa Usilipize ubaya kwa ubaya bali baya kwa jema japo kuna watu ni wagumu kusamehe na kusahau.
Mimi huwa nasamehe mara zote ila kusahau ndo nilishashindwa kabisaa. Hivi inawezekana kabisa kusahau baya alilokutendea mtu??
 
Kuna watu hawasameheki!
Ukimsamehe anakuona mjinga yeye mjanja sana yeye ndio ana akili za kutosha yeye ndio mtoto wa mjini.... Pipo kama hizi ni kulipiza tu kisasi kwenda nao sambamba tofauti na hapo utakufa umekunja sura
 
Msamaha ni kitu kigumu mno kuliko tunavyokifikiria au kukichukulia... kanuni ya msamaha inasema samehe na sahau? Kama huwezi kusahau msamaha wako unakuwa hauna maana yoyote

Mkuu naomba nitofautiane kidogo na wewe, nafikiri ni vyema tukajadili ni kiwango gani cha msamaha tunamaanisha.
Hata usamehe vipi hauwezi kusahau kilichotokea isipokua kama umesamehe kwa nia njema na kwa dhati, hata ukikumbuka inakua haikupi shida wala kukusumbua, huo kwa mtazamo wangu ndio msamaha wa kweli.

Kama leo umenifanyia jambo baya likaniumiza na nikaamua kukusamehe, sitaweza kusahau hilo tukio ila hata kama nikikumbuka halinipi kinyongo na wewe, na wala haliathiri mahusiano yetu. Nakubaliana na wewe kwamba hiyo hali sio kila mtu anaiweza.
 
Mkuu naomba nitofautiane kidogo na wewe, nafikiri ni vyema tukajadili ni kiwango gani cha msamaha tunamaanisha.
Hata usamehe vipi hauwezi kusahau kilichotokea isipokua kama umesamehe kwa nia njema na kwa dhati, hata ukukumbuka inakua haikupi shida wala kukusumbua, huo kwa mtazamo wangu ndio msamaha wa kweli.

Kama leo umenifanyia jambo baya likaniumiza na nikaamua kukusamehe, sitaweza kusahau hilo tukio ila hata kama nikikumbuka halinipi kinyongo na wewe, na wala haliathiri mahusiano na yetu. Nakubaliana na wewe kwamba hiyo hali sio kila mtu anaiweza.
Samaritan msamaha hauna kiwango ukiamua kusamehe unasamehe kabisa mtego unakuja kwenye kusahau na hapa ndio penye mtego kwakuwa tumefundishwa kidini kusamehe na kusahau
 
Samaritan msamaha hauna kiwango ukiamua kusamehe unasamehe kabisa mtego unakuja kwenye kusahau na hapa ndio penye mtego kwakuwa tumefundishwa kidini kusamehe na kusahau

Nimekupata mkuu, tatizo langu lipo hapo kwenye kusema unasahau. Hauwezi kusahau tukio hata siku moja, msamaha wa kweli ni ule ambao hata ukikumbuka tukio lililotokea halikupi shida au maumivu kama miss chagga

Mambo mengi yanayotusumbua yapo kichwani tu au kwenye mawazo hayana uhalisia, wakati mwingine unaweza tu ukabadili unavyoyachukulia mambo na kila kitu kikabadilika.
 
Nimekupata mkuu, tatizo langu lipo hapo kwenye kusema unasahau. Hauwezi kusahau tukio hata siku moja, msamaha wa kweli ni ule ambao hata ukikumbuka tukio lililotokea halikupi shida au maumivu kama miss chagga

Mambo mengi yanayotusumbua yapo kichwani tu au kwenye mawazo hayana uhalisia, wakati mwingine unaweza tu ukabadili unavyoyachukulia mambo na kila kitu kikabadilika.
mkuu kuna mambo ukiangalia impact iliyokuletea maishani na unaishi ndani ya hiyo hali aisee unashindwa kusahau kabisa .. a
 
Back
Top Bottom