Ni mchezo mchafu wa wanaotoza hela kwa wanaotaka kuingia Magufuli stendi, ni mara kadhaa kila nikifika pale ukiwa na sh. 500 au 1000 nk watakwambia hawana shilini 100 au 200.
Mara nyingi wanafaya mchezo huo wakati kukiwa na msongamano wa foleni wanakwambia uchukue chenji nusu au wakurudishie hela ukatafute chenji urudi kupanga foleni upya, na watu kwa kuona usumbufu wa kupanga foleni na kwenda kutafuta chenji wanakubali kuacha hizo 200 au 100.
Wanachofanya ukienda kwa mtu wa kwanza anakwambia hamia dirisha la pili ndio kuna chenji ukienda la pili anadai nenda la 3 wa mwisho anakwambia wa kwanza ndio anachenji au ukatafute mweyewe na wakati huo watu wana haraka.
Kwa nini kila siku wao hawana chenji? Kwa nini wasiende kutafuta chenji benki kwa ajili ya huduma yao wanayoitoa huku wakijua inahitajika chenji kila siku?
Nachoamini ni mradi wa wizi wameanzisha maana hizo hela wanabaki nazo wao.
Mamlaka wafuatilieni wanaibia abiria makusudi na watu wanaoingia kupata huduma mbalimbali humo stendi.
Mara nyingi wanafaya mchezo huo wakati kukiwa na msongamano wa foleni wanakwambia uchukue chenji nusu au wakurudishie hela ukatafute chenji urudi kupanga foleni upya, na watu kwa kuona usumbufu wa kupanga foleni na kwenda kutafuta chenji wanakubali kuacha hizo 200 au 100.
Wanachofanya ukienda kwa mtu wa kwanza anakwambia hamia dirisha la pili ndio kuna chenji ukienda la pili anadai nenda la 3 wa mwisho anakwambia wa kwanza ndio anachenji au ukatafute mweyewe na wakati huo watu wana haraka.
Kwa nini kila siku wao hawana chenji? Kwa nini wasiende kutafuta chenji benki kwa ajili ya huduma yao wanayoitoa huku wakijua inahitajika chenji kila siku?
Nachoamini ni mradi wa wizi wameanzisha maana hizo hela wanabaki nazo wao.
Mamlaka wafuatilieni wanaibia abiria makusudi na watu wanaoingia kupata huduma mbalimbali humo stendi.