Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 8,170
- 11,572
Wapendwa,
Kumeibuka kasumba na tabia isiyo ya kiungwana ya kuchepuka nje ya ndoa au uchumba hivi sasa.
Na inaonekana sasa jambo hili ni kama la kawaida tu. Hapana. Si sawa hata kidogo.
Tabia hii inahatarisha sana na kulegeza uhai na afya ya ndoa na uchumba katika jamii. Ndoa kadhaa zimeshasambaratishwa na zimwi hili.
Ni fedheha na aibu kwa watoto kushuhudia au kuskia wazazi wao wanachepuka upande ule au upande huu na wazazi wa familia nyingine, pisi kali mtaani au viBen 10.
Ni fedheha watoto, na majirani kushuudia mafarakano na mapigano yasioyoisha ya wazazi wana ndoa au wachumba, kudhihakiana na kudhalilishana hadharani kwa lugha kali za matusi na zisizo na staha, kisa kutuhumiana kuchepuka.
Gentlamans,
Baki njia kuu michepuko sio deal. Tafuta kwa bidii na maarifa sana, ladha kamili ya mwenzi wako kimwili na kiroho, na ukisha ijua na kubaini iliko utaenjoy sana maisha ya ndoa na uchumba.
Nakuhakikishia, hutachelewa kurudi nyumbani mapema, wala hutaweza kuvumilia kukaa masaa kadhaa bila kumsabahi au kutaka kuja yuko wapi mwenzi wako, anafanya nini, anajiskiaje au amekula nini.
Kunywa soda au gambe pekeyako mtaani itakua ni ngumu na karaha.
Utatamani sana unywe soda au gambe mkiwa pamoja na mwenzi wako.
Ndugu, hebu jitahidi sana ubaini ladha na utamu halisi wa mwenzi wako kimwili na kiriho, utainjoy mno nakuhakikishia.
Ukiijua ladha ya mwenzia wako kimwili na kiroho, hutaona ndoa au uchumba ni mzigo, adhabu, au karaha bali ni marashi adhimu matamu yasiyo koma kutoa harufu nzuuurii, laini na isiyochosha puani, rohoni, akilini wala moyoni...
Nakuombea Baraka na neema za Mungu, kwa maarifa na ubunifu ulojaaliwa na Mungu uweze kuibaini ladha mujarabu ya kimwili na kiroho ya mwenzi wako mahali iliko, Ili hatimae ndoa na uchumba wenu ukawe wa upendo furaha na amani daima.
Asante.
Kumeibuka kasumba na tabia isiyo ya kiungwana ya kuchepuka nje ya ndoa au uchumba hivi sasa.
Na inaonekana sasa jambo hili ni kama la kawaida tu. Hapana. Si sawa hata kidogo.
Tabia hii inahatarisha sana na kulegeza uhai na afya ya ndoa na uchumba katika jamii. Ndoa kadhaa zimeshasambaratishwa na zimwi hili.
Ni fedheha na aibu kwa watoto kushuhudia au kuskia wazazi wao wanachepuka upande ule au upande huu na wazazi wa familia nyingine, pisi kali mtaani au viBen 10.
Ni fedheha watoto, na majirani kushuudia mafarakano na mapigano yasioyoisha ya wazazi wana ndoa au wachumba, kudhihakiana na kudhalilishana hadharani kwa lugha kali za matusi na zisizo na staha, kisa kutuhumiana kuchepuka.
Gentlamans,
Baki njia kuu michepuko sio deal. Tafuta kwa bidii na maarifa sana, ladha kamili ya mwenzi wako kimwili na kiroho, na ukisha ijua na kubaini iliko utaenjoy sana maisha ya ndoa na uchumba.
Nakuhakikishia, hutachelewa kurudi nyumbani mapema, wala hutaweza kuvumilia kukaa masaa kadhaa bila kumsabahi au kutaka kuja yuko wapi mwenzi wako, anafanya nini, anajiskiaje au amekula nini.
Kunywa soda au gambe pekeyako mtaani itakua ni ngumu na karaha.
Utatamani sana unywe soda au gambe mkiwa pamoja na mwenzi wako.
Ndugu, hebu jitahidi sana ubaini ladha na utamu halisi wa mwenzi wako kimwili na kiriho, utainjoy mno nakuhakikishia.
Ukiijua ladha ya mwenzia wako kimwili na kiroho, hutaona ndoa au uchumba ni mzigo, adhabu, au karaha bali ni marashi adhimu matamu yasiyo koma kutoa harufu nzuuurii, laini na isiyochosha puani, rohoni, akilini wala moyoni...
Nakuombea Baraka na neema za Mungu, kwa maarifa na ubunifu ulojaaliwa na Mungu uweze kuibaini ladha mujarabu ya kimwili na kiroho ya mwenzi wako mahali iliko, Ili hatimae ndoa na uchumba wenu ukawe wa upendo furaha na amani daima.
Asante.