Ukibaraka wa gazeti la RAI

Martinez

JF-Expert Member
Aug 20, 2010
525
160
Ukweli gazeti la Rai la leo tarehe 26Aug2010 limeniboa sana. Kwamba ni mwendawazimu tu ndie atakayempigia kura upinzani. Hoja yenyewe sio ya kweli zaidi ya upotoshaji. Kwamba wapinzani wameshashindwa. Kisa hawana wabunge wa kutosha. Upotoshaji. Uingereza Labour walikuwa na wabunge wachache wakaunda mseto, ipo hapa kwetu na mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini sishangai kwa kuwa wanaoandikia gazeti hili ni vibaraka wa Rostam Aziz, mtu liyekuja kuchuma kiharamu TZ
 
Achana nao hao. Wamo kazini. Hujawaona mawakala wao wamejaa hapa JF?
 
Shilingi Mia Tano yako bora ununue andazi ule kuliko kununua Rai. Pole.
 
Hivi bado kuna watu wenye akili timamu wananunua gazeti la Rai na kulisoma????? Mimi hata kama nikipewa bure na wakanipa allowance ili nilisome bado SITALISOMA.
 
Ukimwita mtu mwenye akili timamu kuwa ni mwendawazimu, yamkini wewe mwenyewe ndiye mwendawazimu!:becky:
 
Huu ni wakati ambapo uchaguzi unatumiwa kama njia ya kujinufaisha, hilo gazeti limeandika habari hiyo ambayo nadhani ni mtazamo wa mwandishi/waandishi wa habari hiyo na vyanzo vyake kadhaa ambavyo ameita "wachambuzi wa mambo ya kisiasa". kwani ukitazama magazeti mengine yanayomilikiwa na watu wenye ushabiki na vyama fulani basi utakuta kuna magazeti yapo kuiponda na kuikosoa serikali tu hata ifanye zuri lipi.(yapo nisingependa kutaja majina) nadhani ulioandikwa ni mtazamo tu tena wa kikampeni japo hoja kadhaa za mwandishi zina ushawishi kutokana na ukweli wa hoja hizo mf sheria ya kuunda serikali lazima uwe na zaidi ya nusu ya wabunge. tunaweza kuiga mifano ya nje kuunda serikali ikiwa mpinzani yeyote atapata urais lakini. Nadhani uchaguzi wa maneno wa mwandishi ukawa umemkera mtu lakini si kila mtu anakasirishwa na kilichoandikwa kwani ile ni Biashara japo kitaaluma hakutakiwa kupendelea chama chochote ila kama yale ni maoni ya wachambuzi kama mwandishi alivyodai basi sioni tatizo na gazeti lile kuwa limepotosha umma.

Nadhani ukisoma vizuri habari hiyo utagundua kuna ukweli fulani ndani ya hoja za "wachambuzi" hao kwani ni kweli huwezi kupitisha muswada ambao wabunge watakaounga mkono kuwa wachache kwani tunajua siasa zetu zilivyo, hata kama kuna maslahi basi unaweza kupingwa na kundi la wabunge wapinzani wa walio madarakani. nadhani umefika wakati tuchambue mambo kimtazamo mpana zaidi kuliko kuona kama chama tunachoshabikia kinaonewa kwa kuwa kiko upinzani na kwakuwa hoja zilizotolewa zina ukweli basi iwe changamoto kwa upinzani kuliko kunung'unikia gazeti ambalo ni hiyari kusoma au kuliacha.,kama ilivyo TV na redio ambapo kipindi fulani mf taarifa ya Habari inaruka muda mmoja na tunachagua kusikiliza/kutazama kituo tunachokipenda.

Haijalishi habari inatoka kwa nani,maadamu kuna hoja basi nadhani ingekuwa busara kuichallenge hoja ya mwandishi kuliko kuliponda gazeti eti kuwa ni la Rostam so haliwezi kuwa na ukweli? naomba kama inawezekana mtoa hoja aweke baadhi ya hoja za mwandishi tuzijadili kuliko kulalamika kuwa gazeti limem-boa coz wako wengi wanalipenda na kuliamini kama chanzo chao cha habari.
 
Ndugu yangu achana na kusoma gazeti la rai, ni bora hiyo pesa ukawapa ombaomba waliopo barabarani kuliko kununua gazeti hilo.
 
Ukweli gazeti la Rai la leo tarehe 26Aug2010 limeniboa sana. Kwamba ni mwendawazimu tu ndie atakayempigia kura upinzani. Hoja yenyewe sio ya kweli zaidi ya upotoshaji. Kwamba wapinzani wameshashindwa. Kisa hawana wabunge wa kutosha. Upotoshaji. Uingereza Labour walikuwa na wabunge wachache wakaunda mseto, ipo hapa kwetu na mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini sishangai kwa kuwa wanaoandikia gazeti hili ni vibaraka wa Rostam Aziz, mtu liyekuja kuchuma kiharamu TZ
Martinez, nadhani sio sahihi kuliita Rai ni kibaraka wa CCM, ni sawa na kuliita gazeti la Uhuru ni kibaraka wa CCM, au Tanzania Daima ni kibaraka wa Chadema.

Kibaraka ni yule mtu ambae anadhaniwa kuwa siye, kumbe siye, hivyo magazeti yenye sifa ya kuitwa vibaraka, ni yale ambayo hayamilikiwa na wanazi wa CCM, ila yanajikomba komba ili angalau waambulie makombo.

Kwa vile Rai, linamilikiwa na fisadi mkuu wa CCM, na alilinunua kwa mabaki ya lile fungu la Kagoda, lazima alikuwa na malengo mpaka kulinunua gazeti hilo, hivyo kinachofanyika sasa ni kutimiza yale malengo makuu kusudiwa, hivyo huko sio kujikomba, ni kutimiza wajibu wake kulikopelekea likanunuliwas na kumilikiwa.

Katika kutimiza malengo hayo, issue ya fair, balance, objectivity, impartiality, right to privacy ambazo ni pillars muhimu kwa chombo cha habari, haziapply hapa ili kutimiza malengo yaliyokusudiwa

Nilishasema kwenye thread fulani kule nyuma, familia ya magazeti ya Habari Corp, yako mkao wa kifo. Baada ya uchaguzi, mtalishuhudia hili, wenye kumbukumbu mtakumbuka ilishawahi kusemwa hapa JF..

Kama Kulikoni limekufa kifo cha mende, na This Day linapumulia mashine, uwezo wa mmiliki wake unajulikana, itakuwa Habari Corp!, baada ya kutimiza malengo, yatakuwa ni what for?, yataachwa yajifie kifo cha mende!.
 
Naona tunashadidia kuwapa umaarufu mafisadi na tools zao.
Dawa ni kanyaga twende
Slaa for president 2010 tumpe kura zetu
 
Mhariri wa RAI anastahili kushitakiwa. Kauli kwamba ''ni mwendawazimu pekee ndiye anayeweza kuwapigia kura wapinzani'' ni ya uchochezi
 
Ukweli gazeti la Rai la leo tarehe 26Aug2010 limeniboa sana. Kwamba ni mwendawazimu tu ndie atakayempigia kura upinzani. Hoja yenyewe sio ya kweli zaidi ya upotoshaji. Kwamba wapinzani wameshashindwa. Kisa hawana wabunge wa kutosha. Upotoshaji. Uingereza Labour walikuwa na wabunge wachache wakaunda mseto, ipo hapa kwetu na mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini sishangai kwa kuwa wanaoandikia gazeti hili ni vibaraka wa Rostam Aziz, mtu liyekuja kuchuma kiharamu TZ
huo ni mtizamo wako, yule anayesoma Tanzania daima hua anaona linambore kama wewe unavyoboreka kusoma rai, kwa hiyo haina haja ya kulalamika, kama unaona litakubore, just buy tanzania daima. So acha kulalamika mtu mzima wewe.
 
Tunaomba Picha za hao VIBARAKA wa RA ...tuanze kuwatenga kwenye jamii ya KItanzania
 
Back
Top Bottom