Ukiachwa achika

Ukiachwa achika

Ni ngumu kuachwa hasa na mtu unaempenda. Wengine wanakuambia tumefika mwisho wa barara, gari yetu ya mapenzi haiendelei na safari. Kuna wanaotoa visingizio, unakuta miezi mitatu hamjaonana wala kuwa na maongezi ya kueleweka. Kila siku atadai yuko busy. Mmh huu u busy mbona unapata muda wa kuoga kula na kulala kama mimi bado ni wa muhimu kwako.

Awe mwanamke au mwanaume. Kama amefikia hatua hiyo, ingawa ni ngumu lakini kubali matokeo. Kumbuka yeye ni mtu mzima ana sababu zake katika maamuzi hayo.

Sasa kuna wale wa binafsi wanaotishia kunywa sumu, kulia, kujiumiza. Mpenzi wewe unafarijika kuwa nae lakini ukumbuke kuwa uwepo wako kwake si faraja tena.
 
Nimejitahidi kusoma kwa umakini lakini nimeshindwa kuelewa.
 
Duh mambo ya kuachana haya yanaumiza muda mwingine. Nilikuwa na mwanamke wangu aisee sikumpenda sana ila nilichoka nae sasa kila nikimuacha analia ananibembeleza namrudia nikanogewa nikamzoea sasa kuna siku akaniudhi nikakasirika sana nikamtamkia bora mapenzi yaishe kila mtu aishi kivyake sasa, yule bint alinijibu sawa kama umeamua hivyo.. Daah ikapita siku tatu mwanamke kakaza wiki kakaza mnh nilikosa raha mimi nilieacha aisee kila nikimuingia labda aniombe msamaha lakini wapi hana time mikausho dadeki ikapita mwezi miezi mwaka miaka mpaka sasa sijui yuko wapi pumbavu zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ndo inaitwaga ego? Ungeomba msamaha wewe ingekuaje? Ukaamua kufa na tai shingoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo yalikua yananipa shida hapo zamani.. Siku hizi nkiona hivo namtafuta nimuulize kulikoni.
Kama hana jibu la maana tayari naziamini hisia zangu then anakula block maisha yanaendelea
Imagine nakutana na wengi wanaohitaj kuwa nami nawakataa sababu ya huyo boya mmoja..
Nimekomaa kwakweli.. Sjpelekeshwi zama hizi

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua rafiki zake wanafikiri ninakuza mambo nimpe jamaa time hata ndugu zangu lakini mimi niliyevaa viatu ninajua vina nibana kuasi gani
Mambo mengine yanaumiza na kukera sana hapa duniani, wakimtizama wanajua hawezi fanya mambo kama hayo kumbe huko ndani ni moto, pole sana watu tunabeba misalaba jamani Mungu akupe wepesi best

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom