UKAWA waeleza sababu za kuzomea Bungeni

UKAWA waeleza sababu za kuzomea Bungeni

Magufuli ni raisi mzuri ila ni kazi Sana kubadilisha system hiii tumechoka
 
Wameshindwa kuvumilia ama walipanga acheni kaukauli za kinafiki walipanga kufanya vile hotuba ya pombe imefunika tukio lao asilimia kubwa tumewaona ni nyumbu
 
Watawala hawana uhakika wa kosa la maalim ndio maana hadi leo bado hawajamshika na kumpeleka mahakamani

Wewe kama unajiamini nenda kampeleke mahakamani kama unoana ni rahisi hivyo.

kama ndivyo hivi basi ifikie hatua kusiwe na katiba kwa sbb hakuna maana yake sasa kama watu wanavunja katiba kwa tamaa zao za madaraka bado tunashangilia na tunaona sawa ifikie hatua msiwe mnapiga kelele bila sbb za msingi ccm wakila rushwa na kupitisha vitu vya ajabu ajabu tukae kimya tu maana hakuna wa kumfunga paka kengere siyo ccm wala cuf wote ni nyoka wa makengeza
 
Kwani kelele zao zimesaidia nini.amiri jeshi mkuu na raisi alitoa hotuba yake ambayo ni mwaka na kuipa dira uongozi wake wakiwemo hao ukawa ambao kwa hotuba yake amewamaliza ukawa.watanzani tumuunge mkono raisi wetu kupasua majipu

Hatuwezi kudanganywa kirahisi hivyo angeanza kupasua majipu ya Escrow, hapo ningeona dhamira ya kweli?????
 
Bado haijaeleweka,kuzomea zomea ni ulimbukeni na haitoi taswira ya watu civillised,afterall sio mara ya kwanza na ndio sababu tendo lenyewe la kuzomea wala halikuwa na punch kwa wananchi kwani waliona hakuna jipya na kwamba UKAWA NI ILE ILE.nilikuwa nimekaa na mwanangu wa miaka minne wa chekechea akawa ananiambia "baba waone wale wanafanya kama sisi shuleni" NIMEMNUKUU.

shame on you!
 
Me walinichekesha sana, kwa speed ile waliyoanza nayo nikadhan hata km wangeambiwa watoke nje wangegoma, ila kauli ya kwanza, ya pili haoooo wakaongoza nje km siafu, hahahahaha
 
Ndugai kafanya la maana kuwaondoa malofa ukumbini! Mpumbavu ni mpumbavu tuuu! Mi ukawa wamenikera pamoja na kwa niliwapankura yangu. They are morons!

Wewe no NG'ONYI tu na haujawapa UKAWA kura na nini.
Ya UKAWA hayakuhusu nenda ukajadili hotuba ya mwenyekiti wenu wa chama mtarajiwa.
 
Wabunge wa Ukawa wameelezea sababu zilizowafanya kuchukua uamuzi wa kupiga kelele baada ya Rais wa Zanzibar, Dkt Ali Mohamed Shein kuingia Bungeni hali iliyopelekea kutolewa nje ya Bunge hilo.

Mbunge wa jimbo la Hai ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe alieleza kuwa walishindwa kuvumilia kuona ujio wa Dkt Shein akiingia Bungeni hapo pamoja na msheshimiwa Pandu Kificho ambaye alidai hivi sasa sio Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa kuwa Baraza hilo lilikwisha vunjwa.

Tumeshangaa kuona Pandu Kificho anaingia kama Spika wa Baraza la Wawakilishi wakati Baraza limeshavunjwa, tulishangaa kuona Dkt Shein anaingia kama Rais wa Zanzibar wakati huo kipindi chake cha kukaa madarakani miaka mitano kimekwisha kikatiba, alisema Mbowe.

Naye mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alisisitiza kuwa wataendelea kuonesha msimamo wao huku akimlalamikia Spika wa Bunge hilo kuwa anaendesha Bunge kibabe.

Leo hii askari wenye uniform, mae-FFU askari wa fujo wameingia ndani ya ukumbi wa Bunge. Sasa kwa wasiofahamu, ukumbi wa Bunge katika nchi kama za kwetu na nchi zinazofuata utaratibu kama wa kwetu, ukumbi wa Bunge huwa haingii mtu yoyote asiyekuwa Mbunge. Ndio maana ili Makamo wa rais na wale wakubwawakubwa tuliokuwa tunawapigia kelele? waingie, ilibidi tutengue kanuni ili kuwaruhusu waingie, alisema Tundu Lissu.

Mwenyekiti wa wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), Juma Hamad Omary alimtaja Maalim Seif Sharif Hamad kuwa kiongozi anayepaswa kuigwa kwa kuwa aliwahi kukubali kushindwa mara kadhaa licha ya mapungufu kuonekana na kwamba hata alipokuwa Makamu wa Kwanza wa rais na kisha wawakilishi wa CCM kukataa asuhudhurie kwenye sherehe za kufunga Baraza la Wawakilishi, aliamua kutohudhuria.

Chanzo: Dar 24

Wapo sahihi kabisa 100%

Nawapongeza mmeitendea haki kura yangu.

Hii tabia si ya kiungwana na wala inayowapasa watu wazima. Kuzomea hadharani kwa sababu eti hawakubaliani na jambo fulani. Sio ustaarabu, uungwana wala weledi.
Na hawa ni watu wazima, viongozi wa kitaifa, na waliokula kiapo takribani siku moja tu iliyopita.

Nawauliza maswali haya ili mjipime wenyewe mnaojiita waheshimiwa wabunge wa ukawa.

1. Je mwanao nyumbani asipokubaliana na wewe katika maamuzi yako, akaamua kupiga kelele na kukuzomea wewe mzazi wake; utamchukuliaje mtoto huyo? Na baada ya hapo utamchukulia hatua gani?

2. Ukiwa mwalimu shuleni (wa ngazi yoyote ile) wanafunzi wako wakawa hawajaridhishwa na jambo au utaratibu fulani...nao wakaamua kukupigia kelele na kukuzomea; je utawachukuliaje? Kisha utawachukulia hatua gani?

Nimetoa mifano hii rahisi ya kuwaonyesha upumbavu wa kitendo cha wabunge.

Kuna njia nyingi rasmi, za kiungwana na zenye matokeo bora zaidi kisheria na kiutaratibu lakini sio kuzomea kama watoto watutuku au walevi.

Hii ni aibu na upumbavu. Afu leo mnataka tuwaite waheshimiwa. Uheshimiwa wenu uko wapi kama mnaoiga kelele, na kuzomea kama magenge ya wahuni?
Tena ndani wa bunge (muhimili wa dola) katika kikao rasmi huku mkionyeshwa dunia nzima.

By the way wake zenu na watoto waliwaona mkitumia "busara" zenu kuzomea...nao watakuja kuwazomea tu siku moja.
 
Bado haijaeleweka,kuzomea zomea ni ulimbukeni na haitoi taswira ya watu civillised,afterall sio mara ya kwanza na ndio sababu tendo lenyewe la kuzomea wala halikuwa na punch kwa wananchi kwani waliona hakuna jipya na kwamba UKAWA NI ILE ILE.nilikuwa nimekaa na mwanangu wa miaka minne wa chekechea akawa ananiambia "baba waone wale wanafanya kama sisi shuleni" NIMEMNUKUU.

Civilization ya KIPUM,ABU ndo akili za MAGAMBA.
Yaani mtu afanye uhaini kwa ukurunzinza watu wamchekee tu.

Akili za CCM ni akili za maiti kabisa.
 
Maalim alisha sema kama halitenda kosa wakamshitaki na pili sheria haisemi kuwa ukijitangaza uchaguzi unafutwa.
Tundu Lissu atusaidie kufafanua hili. Je, ni kosa ama si kosa?? Enyi nyumbu, semeni basi!!
 
Tume ilishamaliza kutoa matokeo ndio maana maalim akayapata yake na ya sheni na kuona ameshinda kwa kura zisizopungua elfu 25

Lakini kosa la kujitangazia matokeo ni kosa la jinai ambalo likisibitishwa na mahakama adhabu yake ni milioni 5 au kifungo au adhabu zote mbili.

Kufuta uchaguzi sio hukumu ya kujitangazia matokeo.
Kama tume ilimaliza kutangaza matokeo mshindi alitangazwa nani? Nyumbu mna ufahamu mdogo sana. Ni aibu kupinga facts kwa uongo. Tabia ya kulishwa uzushi mkauamini ni mbaya sana.
 
Ile Sinema ya UKAWA ya Jana ni watanzania wachache sana ndio wameielewa!

Ukawa lazima watambue uungwaji mkono toka kwa wananchi umeshuka sana, hasa kutokana na siasa zao figisufigisu.

Na kwa mwendo wa Magufuli. Wasipobadili siasa zao za matukio ndio wamejimaliza kabisa!

Kuna uwezakano mkubwa umeathirika na utapiamlo ulivyokuwa mdogo.Suala la Zanzibar ni tete hata JPM ameakiri kuwa ni tatizo.Aliyeshinda kiuhalali na apewe mamlaka.
 
Kitendo cha wajumbe wa UKAWA kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge kwa ajili ya kupinga uwepo wa Dr, Shin kama Rais wa Zanzibar na kusindikizwa na aliyekuwa Spika wa baraza la wawakilishi na makamu wa pili wa Rais Balozi Self Ally Idd ni kitendo sahihi na kinastahili kuungwa mkon na kila mtu anayependa demokrasia,

Ni upuuzi usio na mashiko kufanya uhuni wa wazi eti kwa kuwa tu hakuna mtu wa kupinga kile mnachoamua ninyi.
Kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ni dalili za wazi kuwa ccm waliona kuwa wameshindwa na kama wangekuwa wameshinda hiki kinachoendelea Zanzibar kisingekuwapo.
Dr, Shein akubali kushindwa na kuruhusu ZEC kuendelea na mchakato kwa kutangaza mshindi badala ya kufanya mabo ya ajabu kama yanavyoendelea sasa.
 
Back
Top Bottom