UKAWA waeleza sababu za kuzomea Bungeni

UKAWA waeleza sababu za kuzomea Bungeni

Makofuli aonyeshe uungwana kwa vitendo,yeye kama rais anajua matokeo halisi ya zanzibar,kama anataka kuwa kipenzi cha watu aanze na kumtambua maalim seif kama rais,aache kishabikia chama cha mapinduzi.isije ikawa HAPASTORY TU,HAKUNA KAZI#

Urais siyo Magufuli tu, ni zaidi yake binafsi! Ndiyo sababu anahitaji kuombewa na anatamka mwenyewe hitaji hilo la maombezi! Nguvu ya mamba iko majini!
 
Kitendo cha wajumbe wa UKAWA kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge kwa ajili ya kupinga uwepo wa Dr, Shin kama Rais wa Zanzibar na kusindikizwa na aliyekuwa Spika wa baraza la wawakilishi na makamu wa pili wa Rais Balozi Self Ally Idd ni kitendo sahihi na kinastahili kuungwa mkon na kila mtu anayependa demokrasia, Ni upuuzi usio na mashiko kufanya uhuni wa wazi eti kwa kuwa tu hakuna mtu wa kupinga kile mnachoamua ninyi. Kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ni dalili za wazi kuwa ccm waliona kuwa wameshindwa na kama wangekuwa wameshinda hiki kinachoendelea Zanzibar kisingekuwapo. Dr, Shein akubali kushindwa na kuruhusu ZEC kuendelea na mchakato kwa kutangaza mshindi badala ya kufanya mabo ya ajabu kama yanavyoendelea sasa.
 
Katiba ndio muhimili wa nchi na kila mtu lazima aheshimu katika

VIVA UKAWA
 
Wabunge wa Ukawa walikuwa na haki na sababu za kuchukua hatua waliyochukua. In fact, deservingly, they should have gone much farther than that. Huwezi kukaa kimya wakati unashughudia katiba ikichezewa na mchakato halali wa kidemokrasia ukivurugwa kihuni kihuni. We,as members of a greater community of world's civilised people, have settled for constitutional governance and democratic processes as our avowed principles. We are bound to live by them!

deservingly mwenyeweee
 
Tume ilishamaliza kutoa matokeo ndio maana maalim akayapata yake na ya sheni na kuona ameshinda kwa kura zisizopungua elfu 25

Lakini kosa la kujitangazia matokeo ni kosa la jinai ambalo likisibitishwa na mahakama adhabu yake ni milioni 5 au kifungo au adhabu zote mbili.

Kufuta uchaguzi sio hukumu ya kujitangazia matokeo.

Uchaguzi Zanzibar umefutwa kwasababu ya kosoro zilizojitokeza, haukufutwa kwasasabu Maalim kujitangazia matokeo.
 
Wanamueleza nani sasa,si wawaite wanachama wao kule kinondoni,wafanye kikao cha ndani na kuwaeleza?
 
Wapo sahihi,...hii nchi ni ya chama kimoja japo inatembea chini ya mwamvuli wa vyama vingi,Ili uwe Raisi ni mpk tume na marais wastaafu wakukubali,sio kura za wananchi,....demokrasia inabakwa
 
Nadhani chama cha mapinduzi kina watu wenye busara ambao wanaweza kuwashauri ili mgogoro wa Zanzibar uishe kwa usalama na kumwapisha Maalim Seif kuwa rais
 
Mi nafikiri wangekuwa hawaonekani kwenye tv basi wasingefanya vile.

Nakubalina na we maana jioni hiyo hiyo walitaka kulazimisha kuingia kwenye dhifa halikuwa wanaowakata wamo, wakijua hakuna live coverage hatutawaona.
 
Nilikuwa namuona magufuli kama mtu mzuri na mwenye busara sana, lakini kwa kitendo hiki cha kuruhusu uvunjwaji wa katiba kwa maslahi ya chama chake, naanza kumuona kama kiongozi mbabe na mvunja haki.
Aliposema atafanya kazi bila kuangalia itikadi za vyama nilimsifu sana, ila kwa kitendo cha kuhutubia bunge kibababe bila maridhiano simuungi mkono kabisa.
Nchii hii ni ya watu wote, namshauri raisi asidharau wapinzani kwasababu wanawakilisha wananchi wengi sana, kitendo cha kuwapuuza na kuwadharau ni sawa na kutupuuza sisi tuliowaamini na kuwachagua.
Unatutaka tukuombee lakini usipoondoa roho ya udharimu Mungu hawezi kuwa upande wako kwasababu yeye ni Mungu wa haki wakati wote.
 
Back
Top Bottom